Fungua
Marafiki wa Elimu Dodoma (MED)

Marafiki wa Elimu Dodoma (MED)

Dodoma, Tanzania

Maeneo ya ukurasa huu yametafsiriwa toka (unknown language) kwa Kiswahili. Ona asili · Hariri tafsiri

MCT YAAHIDIWA MSAADA KUHAMIA DODOMA              Na. MED Media Unit

Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Dk. Rehema Nchimbi amelishauri Baraza la Habari Tanzania (MCT) kuhamia Dodoma na kuahidi kusaidia juhudi za baraza hilo ili lihamishie makao yake Mjini Dodoma.

Dk. Nchimbi alitoa ahadi hiyo wakati wa ufunguzi wa maadhimisho ya Siku ya Redio Duniani yaliyo adhimishwa kitaifa Mkoani Dodoma. Mkuu huyo wa Mkoa wa Dodoma alisema kuwa Dodoma si makao makuu ya Chama na Serikali tu bali pia ni Makao Makuu ya Vyuo Vikuu kutokana na Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) kuwa ni chuo kikubwa kuliko vyote katika ukanda wa Afrika Mashariki na Kati.

Katika hotuba yake ya ufunguzi wa maadhimisho hayo Dk. Nchimbi alisema kuwa redio ni chombo muhimu na chenye ufanisi wa haraka katika kufikisha habari kwa umma. Alisema redio haihitaji msomi, tajiri wala maskini na haina gharama kubwa wala kutumia muda katika kumfikishia habari mwananchi. "Redio ni chombo pekee cha habari kinachowafikia wananchi wengi kwa haraka hata wale wasiojua kusoma wala kuandika" 

Aliongeza kuwa kutokana na umuimu wa redio ni vyema maadili yazingatiwe katika redio ili kuielimisha jamii zaidi badala ya redio kutumika kama sehemu ya burudani na kurushana roho. 

Maadhimisho ya siku ya Redio Duniani yamefanyika kwa mara ya tatu tangu yaanzishwe rasmi na UNESCO mwaka 2012; kauli mbiu ya mwaka huu ni TUSHEREHEKEE USHIRIKI WA WANAWAKE KATIKA REDIO NA WOTE WANAO WAWEZESHA.

 

large.jpg

Mtaa wa One Way maarufu kwa biashara mbalimbali ukiwa kimya kutokana na maduka kufungwa kuhusiana na mgomo wa wafanya biashara.

large.jpg

Mgomo wa mashine za TRA wazidi kuathiri wakazi wa Dodoma

large.jpg

Baadhi ya washiriki wa mafunzo ya utawala bora kwa wanafunzi wa shule za Wilaya ya Chamwino yanayoendeshwa na MED kwa uhisani wa Oxfam.

large.jpg

Mgeni rasmi katika mahafali - Chidachi alkimpa mkono wa pongezi mmoja wa wahitibu wa darasa la saba katika shule ya msingi Chidachi.

large.jpg

Mratibu wa Shrika la Marafiki wa Elimu Dodoma (MED) Bw. Davis Makundi (aliye vaa shada) akiwa kwenye mahafali ya nane ya shule ya Msingi Chidachi.

large.jpg

Uendelezaji wa Mji wa Dodoma unaozingatia ujenzi wa nyumba bora za kuishi unafanyika na kuufanya mji wa Dodoma kuwa nadhifu na wa kuvutia, Mamlaka ya Ustawishaji Makao Makuu CDA hainabudi kushughulikia suala la miundombinu ya barabara kwa haraka ili kukidhi mahitahi ya wakazi wa mji huu.

large.jpg

Mandhari ya mji wa Dodoma inazidi kubadilishwa kwa kuboreshwa na wawekezaji mbalimbali kama ambavyo eneo hili la Independence Square linavyoonekana baada ya uboreshwaji uliofanywa na Benki ya Biashara ya Akiba (ACB.