Tatizo la maji katika Mtaa wa Chidachi Manispaa ya Dodoma linawafanya wakazi wa eneo hilo kutumia zaidi ya saa 5 kwa siku kwa ajili ya kutafuta maji.
USALAMA KAZINI UZINGATIWE Na MED Media Unit.
Suala la usalama kazi ni lisipopewa kipaumbele tunaweza kujikuta tukipoteza nguvukazi kutokana na uzembe wa kutokufuata taratibu za usalama wa wafanyakazi. Mpiga picha wa MED amekutana na hali hii ya kutishia maisha ya wafanyakazi ambao kampuni husika haijajulikana wakiendelea na kazi katika jengo la ghorofa la Mackay House ambao wanatumia vitendeakazi duni katika kazi hiyo.
Wafanyakazi wanne wote wanaume wanafanya kazi ya kuwangua rangi ya zamani katika jengo hilo kwa kutumia ngazi za mbao na wao bila kuvaa mikanda maalum itumikayo kwa ajili ya kujizuia endapo itatokea hatari ya kuteleza.
Picha na Marafiki wa Elimu Dodoma.
Kitaifa
Waliofeli kidato cha nne waula, ufaulu sasa waongezeka
Share bookmark Print Email Rating
Na Fredy Azzah, Mwananchi (email the author)
Posted Jumapili,Mei26 2013 saa 18:59 PM
Kwa ufupi
- Habari ambazo gazeti hili imezipata zinasema matokeo hayo ambayo yamewezesha kiwango cha ufaulu kupanda na kufikia asilimia kati ya 54 na 57, huenda yakatangazwa wiki hii pamoja na yale ya kidato cha sita ambayo pia yamechelewa kutangazwa.
SHARE THIS STORY
Dar es Salaam. Idadi ya watahiniwa waliofaulu mtihani wa kidato cha nne mwaka jana imeongezeka kwa kati ya asilimia 20 na 23 baada ya Baraza la Mitihani la Taifa (Necta), kufanya marekebisho alama za viwango vya ufaulu, Mwananchi limebaini.
Habari ambazo gazeti hili imezipata zinasema matokeo hayo ambayo yamewezesha kiwango cha ufaulu kupanda na kufikia asilimia kati ya 54 na 57, huenda yakatangazwa wiki hii pamoja na yale ya kidato cha sita ambayo pia yamechelewa kutangazwa.
Chanzo cha habari kutoka Necta kimesema matokeo hayo mapya yanaonyesha kuwa, ufaulu wa kuanzia daraja la kwanza hadi la nne umeongezeka kutoka asilimia 34.5 kwa matokeo yaliyotangazwa awali na huenda yakafikia asilimia 57. Hii inamaanisha kwamba watahiniwa wapatao 82,000 ambao awali walikuwa wamepata sifuri katika matokeo ya awali sasa wamepanda na kupata madaraja ya ufaulu katika matokeo mapya.
Kwa matokeo hayo, watahiniwa wa mwaka 2012 watakuwa wamefanya vizuri kuliko wa mwaka 2011, ambao watahiniwa 225,126 sawa na asilimia 53.37 ya 349,390 waliofanya mtihani huo walifaulu.
Msemaji wa Necta, John Nchimbi alisema upangaji wa matokeo hayo ulikuwa bado unaendelea. “Ninachojua kwa sasa ni kuwa mchakato unaendelea na matokeo yatatangazwa mapema tu ili watoto waweze kujiunga na shule mapema,” alisema Nchimbi.
Pia alisema usahihishaji wa mitihani ya kidato cha sita umekamilika.
Matokeo ya awali
Matokeo ya awali yaliyotangazwa na Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Dk Shukuru Kawambwa yalionyesha kuwa kati ya watahiniwa 367,756 waliofanya mtihani wa kidato cha nne mwaka jana, waliokuwa wamefaulu kwa daraja la kwanza mpaka la tatu walikuwa 126,847 sawa na asilimia 6.4. Waliopata daraja la nne walikuwa ni 103,327 sawa na asilimia 28.1.
Katika matokeo hayo, watahiniwa 240,909 sawa na asilimia 65.5 walipata sifuri, hesabu ambayo imebadilika katika matokeo mapya ambayo yanaonyesha kuwa sasa waliopata daraja hilo ni 158,100 ambayo ni asilimia 43.
Hata hivyo, habari kutoka Necta zinasema kuwa licha ya kuwezesha kuongezeka kwa waliofaulu, matumizi ya kanuni mpya ya kukokotoa matokeo hayo yalisababisha zaidi ya wanafunzi 2,500 kushuka ufaulu ikilinganishwa na awali.
Maofisa mbalimbali wa Necta pamoja na wale wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi na taasisi zake, walikutana mwishoni mwa wiki iliyopita kukubaliana masuala mbalimbali juu ya matokeo hayo pamoja na suala la matokeo ya wanafunzi hao 2,500 kabla ya kutangazwa wiki hii.
“Baada ya wajumbe kujadili suala lile, busara ilibidi itumike kwa hiyo hakuna mwanafunzi ambaye alama yake itashuka, kwa kawaida isingewezekana mtoto ambaye matokeo yalitoka akiwa amefaulu leo umwambie ameshuka,” kilieleza chanzo chetu.
Chanzo Mwananchi Mei 27, 2013
WASICHANA NA CHANGAMOTO KATIKA MABARAZA YA WANAFUNZI
Ikionekana kama ilishazoeleka ya kuwa viongozi wengi wanaopaswa kuongoza kundi au vikundi vya watu ni lazima awe mwanaume na hivvyo kuchangia kwa kiasi kikubwa kuendelea na ile dhana ya mfumo dume katika jamii zetu.
Hili limeanza kuwa tofauti na mazoea hayo yanayoonekana kama kupitwa na wakati hasa kwa kile kinachoonekana kama ni mapinduzi ya amani na yenye changamoto ya kuleta mabadiliko hayo kuanza kuchukua nafasi kuanzia katika Nyanja mbalimbali zikiwemo mashuleni.
Katika hali isiyo ya kawaida katika shule nyingi za msingi katika Wilaya ya Chamwino zimekuwa na mabaraza mengi ya wanafunzi ambayo kwa sasa yanaongozwa na wasichana nahii imeonyesha kuwa kwa sasa mapinduzi makubwa ya kuondoa ile dhana ya mfumo dume huenda ikapotea kabisa na kuwa na usawa pasipo na ubaguzi.
Hizo ni moja ya juhudi za Shirika lisilo la kiserikali la Marafiki wa Elimu Dodoma (MED) linalotekeleza mradi wa Haki Zangu Sauti Yangu chini ya ufadhili wa Shirika la kimataifa la Oxfam GB tawi la Tanzania,katika Shule 20 zikiwemo 16 za Msingi na 4 za Sekondari.
Aidha awali ya yote wakati wa kuendesha mafunzo yake katika shule hizo kuna baadhi ya wadau walionyesha wasiwasi wao katika kudhani ya kuwa elimu hiyo ingeweza kuwa na matokeo tofauti ya uelewa wa kudai haki zao kama wanafunzi kwa kuwa na usumbufu kwa baadhi ya wanafunzi na walimu wao jambo ambalo limeonekana kuwa tofauti na lenye msaada mkubwa kwa walimu wenyewe.
“mwanzo nilikuwa na wasiwasi mkubwa juu ya haya mafunzo kwani niliamini kuwa ni kama tunaanza kuwajengea chuki wanafunzi dhidi ya walimu wao pindi watakaposhindwa kuelewa kile wanachofundishwa, lakini imekuwa tofauti na ni msaada mkubwa sana kwa sisi walimu kwani kwa sasa kazi nyingi zinafanywa na wanafunzi wenyewe’, alisema Mwalimu Hamisa Chama.anae fundisha shule ya Msingi Chalula iliyopo Wilayani Chamwino Mkoani Dodoma.
Akiongea na maofisa wa MED mwanafunzi Given Mbaigwa wa Shule ya Msingi Mkapa iliyopo wilayani Chamwino Mkoani Dodoma alisema ya kuwa mwanzo alikuwa na woga wa kutaka kugombea nafasi hiyo lakini alijipa moyo na kuamua
WAKETI KWENYE UDONGO DARASANI KWA UHABA WA MADAWATI
Wanafunzi katika shule ya msingi Chalula iliyopo Mvumi Makulu Wilaya ya Chamwino mkoani Dodoma wanakabiliwa na uhaba wa madawati na kusababisha kuketi chini huku baadhi ya madarasa yakiwa hayana sakafu.
Hayo yalibainika hivi karibuni wakati wa ziara iliyofanywa na shirika la Marafiki wa Elimu Dodoma (MED) ambapo lengo lilikuwa kufuatilia mradi wa ‘Haki zangu Sauti yangu’ unaotekelezwa katika shule 20 zikiwemo shule 16 za Msingi na 4 za Sekondari zilizopo wilaya ya chamwino pamoja na ufuatilaji wa matumizi ya maendeleo ya vitabu walivyotoa msaada katika shule hizo.
Kwa mujibu wa Mwalimu mkuu wa shule hiyo, Amina Mohamed, hali ya madawati katika shule hiyo ni mbaya kwani imefikia hatua wanafunzi wa darasa la tatu kuketi chini kwenye udongo kutokana na darasa kutokuwa na sakafu na kuwepo kwa msongamano wa wanafunzi 150 katika darasa moja.
Licha ya kuishukuru MED kwa kutoa msaada wa vitabu 1015 vya kiingereza, Hisabati na Atlasi katika shule hiyo, mwalimu huyo alisema kuwa mahitaji ya vitabu bado ni makubwa. Changamoto nyingine katika shule hiyo ni hali mbaya ya uchakavu wa majengo yasiyo na milango.
Tatizo la upungufu wa madawati imewakumba pia wanafunzi wa shule ya Msingi Mvumi Makulu kutokana idadi ya madawati 100 waliyo nayo kati ya madawati 407 yanayohitajika.
Mwalimu mkuu wa Shule hiyo, Mary Mabichi alisema wanakabiliwa na upungufu wa madawati 307 na vyumba vya madarasa ni vidogo hali inayosababisha wanafunzi kuketi kwa kusongamana. Alisema kuwa walijitahidi kushirikisha jamii ili kuweza kupunguza ukubwa wa tatizo hilo na waliweza kuchangia madawati 40.
Mabichi alisema wanafunzi wengi wanakaa wakiwa wamesongamana na madawati hayo yako katika madarasa mawili kati ya saba yaliyopo ambapo dawati moja hukaliwa na wanaafunzi watatu hadi wanne.
Alisema kuwa darasa la sita na saba huketi kwenye madawati huku madarasa yaliyobaki wanafunzi wanakaa chini. Pia alisema wanafunzi wa chekechea wamepewa madawati 10 ili wasione taabu kuja shuleni kwani wakati mwingine kukaa chini kunasababisha baadhi ya wanafunzi kuchukia shule.shule hiyo ilipokea jumla ya vitabu 1036 kutoka shirika la Marafiki wa Elimu Dodoma.(MED)
MIAKA SABA SHULE HAINA MWALIMU WA HESABU
Wakati serikali ikiwa imeunda tume ya kuchunguza chanzo cha matokeo mabaya ya kidato cha nne kwa mwaka 2012, zipo sababu nyingi zinazoonyesha dalili za awali za majibu yatakayoletwa na tume hiyo mara baada ya kukamilika kwa uchunguzi wake.
Hivi karibuni yalitangazwa matokeo ya watahiniwa wa kidato cha nne kwa mwaka wa masomo wa 2012 na kuonyesha ya kuwa 60.1% ya wanafunzi waliofanyamtihani huo walishindwa kufikia vigezo vya kuendelea na masomo. Hali hiyo ilionekama kama kuishitua jamii na wadau wa Elimu nchini.
Pamoja na kuwa na walimu wengi waliopo vyuoni na hata wale walipangiwa vituo vya kazi shule ya sekondari ya Buigiri iliyopo katika Wilaya ya Chamwino haijawahi kupangiwa mwalimu wa hesabu kwa mika saba sasa. Hali hii imesababisha kuwepo na mwenendo wa kusuasua katika somo hilo, kwani imelazimika kwa shule kuajili walimu wa muda wa kuweza kutoa msaada wa Huduma hiyo kwa wanafunzi wake.
Akiongea na Marafiki wa Elimu Dodoma (MED) katika ofisi yake Makamu Mkuu wa shule ya Buigiri sekondari Mwl. Razalo Njamasi alisema ya kuwa tatizo la kutokuwa na mwalimu wa hesabu katika shule yake ni la muda mrefu ambalo mpaka sasa hawajapangiwa mwalimu wa hesabu katika shule hiyo, ‘Tunalazimika kutafuta mwalimu wa muda kwa ajili ya kusaidia watoto wetu lakini serikali kama serikali haijawahi kutupangia mwalimu wa hesabu na tuna mwaka wa saba sasa tangu shule hii imeanza kufundisha’, alisema mwalimu Njamasi.
Aidha tatizo la kutokuwa na mwalimu wa somo hilo linalounganisha masomo ya sayansi limeonekana kama kuwa ni janga kwa wilaya ya Chamwino limeikumba pia Shule ya sekondari ya Chamwino ambayo yenyewe ina mwalimu mmoja tu wa hesabu ambaye hutoa huduma hiyo kwa zaidiya wanafunzi 472, hayo yalibainishwa na Mkuu wa shule hiyo Bwana Fedinand Komba alipokuwa akitoa taarifa fupi juu ya maendeleo ya Mradi wa Haki zangu Sauti yangu mradi unaoendeshwa na Shirika la Marafiki wa Elimu Dodoma kwa ufadhili wa shirika la kimataifa la Oxfam GB ya Uingereza tawi la Tanzania.
Bwana Komba alibainisha kuwa kwa kawaida mwalimu hupaswa kuwa na vipindi 40 kwa muhula lakini kutokana na tatizo la uhaba wa walimu analazimika kuwa na vipindi visivyopungua 60 kwa muhula, kitu ambacho kinamfanya hata yeye mwalimu mwenyewe kushindwa kuwamudu wanafunzi wote kwa wakati,’badala ya kufundisha vipindi 40 mwalimu huyu analazimika kufundisha vipindi zaidi ya 60 kwa muhula kitu ambacho inakuwa si rahisi kwa mwalimu huyu kuwamudu wanafunzi kwa wakati’, alisema mwl. Komba.
Lakini pia pamoja na hayo yote katika shule nyingi kumeonekana kuna changamoto ya kutokuwa na walimu wa masomo ya sayansi kama vile katika masomo ya Chemistry na Physics kitu ambacho kwa mujibu wa baadhi ya walimu walidai inasababishwa na kutokuwa na vifaa vya kufundishia kwa vitendo katika maabara za shule.’walimu wengi wanashindwa kuja kwanza unakuta vifaa vya kufundishia hakuna na kama unavyojua masomo haya mwanafunzi anapaswa kujifunza kwa vitendo zaidi kuliko kusiliza na kuandika tu’, alisema mmoja wa walimu wa Sekondari ya Chamwino.
Kuna haja kwa serikali kukaa na kujipanga upya katika kuhakikisha ya kuwa mgawanyo wa walimu unazingatia na uhitaji wa masomo yanayokuwa hayana kabisa walimu tena kwa kuyapa kipaumbele masomo ya sayansi ambayo mara nyingi ndio huonekana wanafunzi wengi hawafanyi vizuri katika mitihani yao ya mwisho kwenye masomo haya.
Katika utekelezaji wa kweli wa maendeleo ya Tanzania tunahitaji viongozi wachapakazi wenye moyo wa kutumikia wananchi na kukubali ushauri bila kujali nyadhfa zao. Bi.Fatma Said Ally ambaye ni Mkuu wa Wilaya ya Chamwino ni miongoni mwa viongozi ambao wanapongezwa na wananchi kutika juhudi zake za kuwa karibu na wananchi,taasisi pamoja na wadau katika Wilaya yake kwa lengo la kuwaletea maendeleo. MED inampongeza kiongozi huyu na kumtakia kila la kheri katika kutimiza azma yake ya kuifanya Wilaya ya Chamwino kuwa Wilaya zenye maendeleo chanya.(Pichani aliye simama ni mkuu wa Wilaya ya Chamwino Bi.Fatma Said Ally,kulia ni Bw. Baltazar Ngowi Afisa utumishi mkuu wa halmashauri ya Wilaya ya Chamwino na kushoto ni Bw.Davis Makundi mratibu wa shirika la Marafiki wa Elimu Dodoma.)(MED).
Hili ni jengo la choo cha Shule ya Msingi Ndebwe iliyopo Wilayani Chamwino Mkoani Dodoma choo ambacho wanafunzi hukitumia wawapo shuleni hapo.
Hili ni moja ya tundu la choo hicho kinachotumiwa na wanafunzi wa Shule ya Msingi Ndebwe Wilayani Chamwino Mkoani Dodoma.