Fungua
Marafiki wa Elimu Dodoma (MED)

Marafiki wa Elimu Dodoma (MED)

Dodoma, Tanzania

Maeneo ya ukurasa huu yametafsiriwa toka (unknown language) kwa Kiswahili. Ona asili · Hariri tafsiri

MED Yaomba Wastaafu Kufundisha kwa Mikataba.

Asasi ya Marafiki wa Elimu Dodoma MED imemwomba Mkuu wa Wilaya ya Dodoma Mjini ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Ushari ya Wilaya (DCC) Bw. John Tuppa; kuishauri kamati yake ili iwatumie walimu wastaafu kufundisha shule za sekondari za kata.

Barua ya MED yenye maombi hayo iliwasilishwa kwa Mkuu wa Wilaya kwa lengo la kusaidia kupunguza tatizo la uhaba wa walimu katika shule za kata katika Wilaya ya Dodoma.

Kwa mujibu wa barua hiyo; MED imemuomba Bw. Tuppa kuwatumia walimu wastaafu kufundisha katika shule za kata ambazo wastaafu hao wanaishi badala ya kuendelea kuwasubiri vijana wadogo wanaohitimu masomo na kwenda kufundisha kwenye shule hizo bila kuzaa matunda tarajiwa.

Barua hiyo ilieleza kuwa; licha ya nia ya serikali kuwatumia wahitimu wa kidato cha sita kuziba pengom la walimu; wahitimu hao wamekuwa wakituhumiwa kuwa sehemu ya chanzo cha ongezeko la mimba kwa wanafunzi wa shuleni wanazo fundisha.

Baadhi ya wadau wameipongeza MED kwa hatua hiyo ya uthubutu waliyo ichukua  kwa Mkuu wa Wilaya na kuongeza kuwa; wastaafu wengi wenye taaluma ya ualimu wana maadili ya kazi hiyo hivyo wanaweza  kusaidia sana kupunguza tatizo la uhaba wa walimu kwenye shule za kata kama wastaafu hao watatumika ipasavyo na kupewa stahili zao.

Mratibu wa MED Bw. Davis Makundi amekiri kumwandikia Mkuu wa Wilaya barua hiyo na kusema; hiyo ni haki ya msingi kwa mtu binafsi, taasisi au kikundi chochote cha kijamii kwani barua hiyo ni ya kumshauri na si ya amri kwa kiongozi huyo wa Wilaya.

 

27 Februari, 2011
« Iliyotangulia Ifuatayo »

Ongeza maoni

Jina lako:
Mahali ulipo:
Email yako:
(sio lazima)
Anwani yako ya email haitachapishwa.