MED Hewani Kuanzia Mach 2011.
Asasi ya Marafiki wa Elimu Dodoma (MED) inatarjia kuanza kuendesha vipindi vyake vya Radio kuhusu Elimu kuanzia mwezi Machi, 2011. Wanachama wa MED na wadau wote wa Elimu wanakaribishwa kushiriki kwenye vipindi hivyo.
Hayo yameelezwa na Mratibu wa MED Bw. Davis Makundi alipkuwa akiongea na mwandishi wa habari hizi ofisini kwake. Bw. Makundi amesema vipindi hivyo vitaendeshwa kwa udhamini wa mashirikaya HakiElimu na Uwezo.net yote ya jijini Dar Es salaam
"Vipindi hivi vitakuwa vya moja kwa moja kutoka studio (Live) na vitaruhusu wasikilizaji walio nje ya studio kupifa simu au kutuma SMS kwa lengo la kuchangia mada au kuuliza maswali alisema" Bw. Makundi.
Vipindi hivyo vitakavyosikika kwa muda wa nusu saa (dk. 30); vitakuwa vikisika kwenye Radio Kifimbo 89.8 inayorusha matangazo yake kwenye masafa ya FM Mkoani Dodoma. Bw. Davis Makundi
Comments (2)