Envaya
Uru rupapuro ruragaragazwa mu rurimi rw'umwimerere Igiswayire. Edit translations

MCHAKATO WA KUPATA WAJUMBE WA BODI YA MED WAANZA.  Na. Bentez Fares.

Asasi ya Marafiki wa Elimu Dodoma (MED) imeanza mchakato wa kutafuta Wajumbe wa Bodi yake kwa ajli ya kusimamia shughuli za Asasi hiyo. Mchakato huu umeanza siku chache baada ya MED kuwasilisha Katiba na vielelezo muhimu kwenye Ofisi ya Msajili wa Asasi za Kiraia katika Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto na kuahidikwa kupata hati ya usajili ifikapo Ijumaa ya tarehe 10 Februari; 2012.

Katiba ya MED inaelekeza kuwa kutakuwa na Bodi ya Ushauri ya MED ambayo itasimamia Sekretarieti ya MED katika utekelezaji wa wa majukumu na kuwasilisha taarifa yake kwenye Mkutano Mkuu wa Wanachama.

Bodi ya MED itakutana mara nne kwa mwaka katika vikao vyake vya kawaida na pia inaweza kuitisha mkutano wa Bodi wa dharura wakati wowote itakapoonekana inafaa kufanya hivyo.

Ili kuwepo na uwiano wa kijinsia katika Bodi hiyo; Katiba ya MED inaelekeza kuwa wajumbe watakuwa tisa na kati yao lazimama watatu kati yao wawe wanawake. Kwa mujibu wa katiba hiyo; wanawake wanaweza kuchaguliwa kwa idadi yoyote kuingia kwenye Bodi hiyo.

Kwa mujibu wa taarifa za ndani ya MED wajumbe wa Bodi wanapaswa kuomba kupata nafasi hizo. Asasi ya MED ni miongoni mwa asasi chache za Mkoa wa Dodoma zinazo juihusisha na Elimu, Demokrasia, Utawala Bora na utetezi wa Haki za Wanafunzi.

7 Gashyantare, 2012
« Inyuma Ahakurikira »

Tanga igitekerezo

Izina ryawe:
Aho uherereye
Your email:
(optional)
Your email address will not be published.