Injira
Marafiki wa Elimu Dodoma (MED)

Marafiki wa Elimu Dodoma (MED)

Dodoma, Tanzania

Uru rupapuro ruragaragazwa mu rurimi rw'umwimerere Igiswayire. Edit translations

 

                UJIRA WA WALIMU UZINGATIE MAZINGIRA WANAYOPANGIWA

Imekuwa ni kama kawaida kusikia ya kuwa wapo walimu wengi  wanaoshindwa kulipoti kwaenye vituo vya kazi kutokana na sababu mbalimbali ikwemo ugumu wa mazingira ya kufanyia kazi, vitendea kazi na hata uhakika wa maslai yao kuwafikia kwa wakati.

Hayo yamezungumzwa na wadau wa elimu  mkoani Dodoma wakati wakiwa kwenye shughuli za ugawaji wa msaada wa vitabu katika wilaya ya chamwino mkoani humo. Akiongea na mratibu wa shirka lisilo la kiserikali la marafiki wa elimu mkoani Dodoma Mwl Abinery Malogo wa shule ya msingi Wiliko alisema wamekuwa wakipata shida sana hasa pale wanapojikuta asilimia zaidi ya 25% ya mishahara  yao inatumika katika nauli katika kipindi kinapofika cha kwenda kuchukua mishahara yao. Aidha mwl malogo alilalamikia pia kuona walimu waliopo mijini waapewa kiwanngo sawa na wale wanaoishi vijijini.                                                                                            

                                                                                                                                                  (Moja kati ya ofisi ya walimu kama inavyoonekana katika shule ya msingi Mzula iliyopo wilayani Chamwino)

 kitu ambacho amedai  kuwa  hali hiyo imekuwa ni tatizo kubwa na linaloonekana kama ni uonevu kwani kwa wao kukubali kutumikia maeneo ya vijijini.

Hakika kama walimu waliopo vijijini wangekwa wanapatiwa kiwango kikubwa tofauti na wanachopewa sasa hakika walimu wengi wengi ambao wamekuwa wakipangiwa katika maeneo ya vijijini wangekuwa wanaripoti kwa wakati na kufanya kazi kwa moyo mmoja na kuwa na uhakika wa kuwa na maisha bora na ya mfano kwa wote wanaopenda kuwa walimu.

Mbali na ugumu wa mazingira pia baadhi ya vitu vilivyoonyesha kuhatarisha maisha ya wlimu hao ni pamoja na uchakavu wa majengo, kama vile ofisi za walimu,vyoo kutokuwa na madarasa ya kutosha kitu kinachowalazimu baadhi ya wanafunzi kufundishiwa sehemu zisizo kidhi matakwa yao, pia ukosefu wa madawati ya kukalia wanafunzi imeonekana ni kikwazo katika maeneo mengi wilayani humo. Mbali na ukosefu wa madawati lakini pia wapo wanafunzi wanaosomea chini ya miti kitu ambacho kinaonekana kama ni hadithi za kale, lakini ukweli ndivyo ulivyo kwenye maeneo mengi ya vijijini mkoani Dodoma.

25 Gashyantare, 2013
« Inyuma Ahakurikira »

Tanga igitekerezo

Izina ryawe:
Aho uherereye
Your email:
(optional)
Your email address will not be published.