Envaya
Uru rupapuro ruragaragazwa mu rurimi rw'umwimerere Igiswayire. Edit translations

4. UZINDUZI WA MAKTABA YA JAMII YA WEMA - MKALAPA

Tarehe 11 Julai 2009 iliambatana na tukio muhimu na la kihistoria katika kijiji cha Mkalapa. Kijiji cha Mkalapa kipo katika wilaya ya Masasi mkoani Mtwara. Kikundi cha Wanaharakati wa Elimu, Mazingira na Afya-WEMA walizindua rasmi Maktaba yao ya Jamii ya WEMA ambayo ina vitabu na machapisho zaidi ya 750.

Vitabu vilivyomo kwenye maktaba ya WEMA vimechangiwa na wafuatao; HakiElimu (machapisho na vitabu zaidi ya 150), Mratibu na mshauri wa kikundi Mr. Mussa P.M. Kamtande (amechangia vitabu na machapisho zaidi ya 450), pamoja na taasisi kama; Chuo cha Ualimu Mtwara (K), na Chuo cha Ualimu Mtwara (U), ambao kwa pamoja wamechangia machapisho yapatayo 150.

Katika picha hapa chini anaonekana Mwenyekiti wa Kikundi cha WEMA Mr. Fidelis Milanzi akiwa na mgeni rasmi Mr. Richard Lucas wakiangalia vitabu kwenye maktaba hiyo. Mgeni rasmi katika shughuli hiyo ni mwakilishi wa shirika la HakiElimu kutoka makao makuu Dar es Salaam. Anayeonekana kwa nyuma ni Mr. Boniventura Godfrey ambaye pia ni miongoni mwa wageni waliowakilisha shirika la HakiElimu siku hiyo ya uzinduzi wa maktaba. Maktaba ya WEMA ina vitabu vinavyokidhi viwango vyote vya kitaaluma kuanzia; elimu ya Awali, Msingi, Sekondari hadi chuo kikuu.Hivi sasa maktaba hiyo inatumia jengo la kuazima, lakini jukumu lililopo mbele yao ni ujenzi wa jengo la kudumu la WEMA kwa ajili ya maktaba. (Taarifa za uzinduzi wa maktaba ya jamii ya WEMA zilichapicha na magazeti mbalimbali yakiwemo gazeti la "The Citizen" la tarehe 17 Julai 2009 na Mwananchi la tarehe 15 Julai 2009)

12 Ukwakira, 2010
« Inyuma Ahakurikira »

Tanga igitekerezo

Izina ryawe:
Aho uherereye
Your email:
(optional)
Your email address will not be published.