Log in
Wanaharakati wa Elimu Mazingira na Afya (WEMA)

Wanaharakati wa Elimu Mazingira na Afya (WEMA)

Mkalapa, Ndanda-Masasi, Tanzania

Parts of this page are in Swahili. Edit translations

5. NAMNA WANA-WEMA WALIVYOWAKUMBUKA WANAFUNZI YATIMA SIKU YA MJADALA WA WAZI - NDANDA

Tarehe 03 Mei 2010 kikundi cha Wanaharakati wa Elimu, Mazingira na Afya-WEMA waliendesha mjadala wa wazi katika mji mdogo wa Ndanda. Wana-WEMA waliitumia siku hiyo kukabidhi misaada kwa wanafunzi watatu ambao ni yatima kutoka katika shule tatu za msingi. Wanafunzi hao ni Genofever Kavili mwanafunziwa darasa la IV kutoka shule ya msingi Mtunungu, Fatuma Hassani wa darasa la VI kutoka shule ya msingi Mkalapa, na Moshi Raphael pia wa darasa la III kutoka shule ya msingi Liputu.

Moja ya majukumu ya WEMA katika elimu ni kuwabaini na kuwasaidia wanafunzi yatima, waliofiwa na wazazi wao na ambao wanashindwa kuendelea na masomo kwa kukosa vitu muhimu kama ada na vifaa vingine kama daftari. Lengo la baadaye la WEMA ni kuwafikia na kuwasaidia wanafunzi yatima wengi zaidi wenye matatizo na ambao wanashindwa kupata msaada kutoka kwa ndugu zao.

Hata hivyo uwezo wa kikundi kuwahudumia watu wengi zaidi itategemea uwezo wa kifedha wa kikundi. Kwa sasa misaada hiyo hutokana na michango ya wanakikundi wenyewe.

 

 

 

 

 

Katika picha inayoonekana hapa juu, anaonekana Mratibu Elimu Kata wa Kata ya Mwena; mama Clara Maona akimkabidhi kifurushi mwanafunzi Genofever Kavili wa darasa la VI kutoka shule ya msingi Mtunungu. Ndani ya kifurushi hicho mna sare ya shule (shati na sketi). Wanafunzi wenzake pia walipewa msaada kama huo.

October 12, 2010
Next »

Add a comment

Your name:
Your location:
Your email:
(optional)
Your email address will not be published.