Log in
Wasaidizi wa kisheria Masasi

Wasaidizi wa kisheria Masasi

Masasi, Tanzania

Wakihabima imebahatika kuwa moja ya asasi zilizotoa waangalizi wa uchaguzi wa ubunge jimbo la Masasi uliokuwa umeahirishwa wakati wa uchaguzi mkuu Oktoba 20 kutokana na kufariki kwa mmoja ya wagombea Dr. Emmanuel Makaidi wa NLD. Kazi hii waliifanya kwa mwamvuli wa TACCEO chini ya kituo cha Sheria na haki za Binadamu LHRC. Walioshiriki walikuwa; Noel Mwembere, Tanmoza Fungafunga, Donald Simonje, Mwanaafa W. Malenga, Irene Liyumba, Frank Liweta, Monica Mzula, Damas Mlaponi, Mwinda Mkwamba, Maurice Ng'hitu, Edna Ngasiwa, Sekioni Joseph, Yakobo Yohana na Anjelina Saidia. Hawa waliungana na jopo laTACCEO/LHRC lililoongozwa na Dr. Geoffrey Chambua. Uchaguzi huo ulifanyika Disemba 20/2015 na mgombea wa CCM alipata ushindi.
December 25, 2015
« Previous Next »

Add a comment

Your name:
Your location:
Your email:
(optional)
Your email address will not be published.