Asema hata akifaulu shule ya Kata hasomi:
Mwanafunzi wa shule ya msingi Mvumi Makulu Elia Mkwila (13) amesema hayuko tayari kusoma katika shule za serikali za kata kutokana na elimu inayotolewa katika shule hizo kuto kukidhi mamhitaji ya elimu bora nchini. Kijana Mkwila ayasema hayo alipofanya mahojiano mafupi na Mrartibu wa shirika la Marafiki wa Elimu Dodoma (MED) Bw. Davis Makundi wakati wa kukabidhi vitabu kwenye shule hiyo iliyoko katika Tarafa ya Mvumi.
Hali inaonyesha wazi kuwa kwa sasa hata wanafunzi wenyewe wanaona kuwa hawata kuwa tayari kuona juhudi zao zikiishia katika shule zinazokosa vigezo vya kutoa msaada wa kuwafanya waendelee kuwa bora katika elimu yao. Kutokuwa kuwa kwao tayari kusoma katika shule za kata ni sawa na mtu anaye amua kujitoa mhanga maisha yake kama njia mojawapo ya kuonyesha kutorizika na jambo fulani.
Mwanafunzi huyo mlieleza kuwa katika masomo yake ya darasa la saba amekuwa akifanya vizuri kwenye masomo mengi ila kazi kubwa iko kwenye masomo mawili ya Hisabati na Kiingereza ambayo hufanya vibaya kila mwaka.
Katika hatua nyinhgine mmoja wa walimu wa shule ya msingi Mvumi Makulu anakosoma kijana nElia ambaye hakutaka jina lake litajwe alieleza kuwa licha ya juhudi kubwa za walimu katika kufundisha, bado ana mashaka makubwa na hai itakavyokuwa kwa wanafunzi wa darasa la saba wakati wa mtihani. “watoto hawa wanahitaji kazi ya ziada katika kuwasaidia katika mtihani wao wa darasa la saba kutokana na masharti ya kutumia karatasi za (OMR)”.
MED YATOA SAADA WA VITABU.
Shirika la Marafiki wa Elimu Dodoma MED limetoa msaada wa vitabu vya kiada na kiongozi cha mwalimu vyenye thamani ya zaidi ya Sh. 397,363,300 kwa Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino kwa lengo la kuboresha Elimu katika Wilaya hiyo. Mdsaada huo wa vitabu vya masomo ya kiingereza, Hisabati na Jiografia utawanufaisha walimu na wanafunzi wa shule 82 za Halmashauri ya Chamwino iliyoko Mkoani Dodoma.
Akitoa shukrani kwa niaba ya wanafunzi wa shule ya msingi ya Handali ambayo ni moja kati ya shule zilizonufaika na msaada huo wa vitatu mwalimu Grace Mtani alisema msaada huo umekuja atika wakati muafaka hasa ukizingatia kuwa utakuwa ni msaada mkubwa hasa kwa wanafunzi wa darasa la saba ambao wapo kwenye maandalizi ya mtihani wa taifa. Akionyesha kuwa nia yao ni kutaka kusaidia jamii inayowazunguka kwa wakati mratibu wa shirika hilo la marafiki wa elimu mkoani Dodoma Bw. Davis Makundi amesema msaada huu ni mwanzo tu katika halmashauri hiyo ya Chamwino,kwani wamejipanga vizuri kwa kushirikiana na wadau wengine katika kuboresha elimu ya wanaChamwino.
Mbali na msaada huo wa vitabu katika wilaya hiyo, MED imeweza pia kushuhudia matatizo mengi yanayowakabiri wanafunzi wengi katika wilaya hiyo hasa likiwemo tatizo la ukosefu wa madawati kitu ambacho kimeonekana kama kuwa ni tatizo lililoanza kuzoeleka katika maeneo mengi katika wilaya hiyo, pia limejtokeza tatizo kubwa linalohatarisha afya za wanafunzi wengi katika shule nyingi katika wiaya ya chamwino ni ukosefu wa vyoo, vyumba vya madarasa, madawati, zana balimbali za lujifunzia na kufundishia pamoja na mafunzo ya walimu kazini.
MED KUGHARAMIA MITIHANI YA MAZOEZI IV KIKUYU SEKONDARI.
Shirika la Marafiki wa Elimu Dodoma MED litagharamia uchapishaji wa mitihani ya Mazoezi kwa wanafunzi wa kidato cha nne katika shule ya sekondari Kikuyu ili kuongeza maarifa kwa wanafunzi wa shule hiyo wanaotarajiwa kufanya mtihani wa kuhitimu kidato cha nne mwezi Novemba, 2013.
Uamuzi huo wa MED umetolewa katika kikao cha pamoja kati ya wazazi, wanafunzi na walimu wa kidato cha nne wa shule hiyo kilichoitishwa kwa lengo la kutathimini matokeo ya kidato cha Nne 2012 na kujipanga kwa ajili ya matokeo ya mtihani wa mwaka huu.
Akichangia katika kikao hicho Mratibu wa MED Bw.Davis Makundi Amesema kuwa ili kuhakikisha kuwa wahitimu wa mwaka huu wanafanya vizuri hapana budi jamii,walimu,wazazi,wanafunzi na wadau mbalimbali kuungana pamoja kuwawezesha wanafunzi kupata mazoezi ya mara kwa mara ya majaribio ya mitihani ya kujipima
Akiwasilisha taarifa ya maandalizi ya mtihani wa kidato cha nne 2013 kwa wazazi mwalimu wa taaluma shuleni hapo Francis Tumaini Wambura amesema kidato cha nne kwa mwaka huu kina wanafunzi 168 ambao wanatarajiwa kufanya mtihani wa kuhitimu kidato cha nne.
Kwa mujibu wa taarifa za idara ya taaluma shuleni hapo kati ya wanafunzi 168 wanaotarajiwa kufanya mtihani wa kidato cha nne mwaka huu wanafunzi 21 mpaka sasa hawaja sajiliwa kutokana na utoro.
Aidha taarifa zimeongeza kuwa zoezi la kulipia ada ya mtihani wa taifa linalotarajia kukamilika tarehe 28 mwezi huu wa pili inaonekana kusuasua ambapo wanafunzi 40 pekee ndio waliolipia ada hiyo hadi sasa.
Wanafunzi wa Shule ya Msingi ya Kambarage Wilayani Chamwino Mkoani Dodoma wakiwafurahia wafanyakazi wa shirika lisilo la kiserikali la Marafiki wa Elimu Dodoma hawako pichani walipokwenda kutembelea shule hiyo ikiwa ni mojAwapo ya ufuatiliaji wa mradi wa HAKI ZANGU SAUTI YANGU.
Afisa mipango wa MED Luhaga Makunja,kulia akimsikiliza mwalimu mkuu wa Shule ya Msingi Kambarage iliyopo katika Wilaya ya Chamwino Mkoani Dodoma mwalimu Emmanuel Ndepeka wakati wa ufuatiliaji wa utekelezaji wa mradi wa HAKI ZANGU SAUTI YANGU katika shule hiyo.
NDEBWE YALETA MABADILIKO KATIKA DEMOKRASIA.
Na. MED Information Unit
Shule ya Msingi Ndebwe iliyoko katika Halmashauri ya Wilaya ya Dodoma imeonesha matokeo mazuri katika uchaguzi wa kidemokrasia kwa kumchagua msichana kuwa Kiranja Mkuu wa shule hiyo na kuwashinda wavulana waliokuwa wapinzani wake wa karibu.
Rosemary Masaka (pichani) mwanafunzi wa darasa la sita katika shule ya Msingi Ndebwe alipata ushindi huo baada ya kuamua kugombea nafasi ya kiranja Mkuu kufuatia mafunzo ya elimu ya kidemokrasia katika kuwapata viongozi wa shule yaliyotolewa na shirika la Marafiki wa Elimu Dodoma (MED) kupitia mradi wake wa Haki zangu Sauti Yangu unaofadhiliwa na shirika la Oxfam GB.
Akiongea na maafisa wa MED mtoa habari hizi ambaye hakutaka jina lake litajwe alieleza kuwa hii ni mara ya kwanza shule yao kupata kiranja Mkuu mwanamke. “zamani tulikuwa tuna chagua viongozi sisiwenyewe walimu na kuwatangazia wanafunzi” alisema mtoa habari huyo.
Aliongeza kuwa awali shule ilikuwa zikichagua viongozi kwa cheo cha kaka Mkuu na Dada Mkuu ambapo sasa utaratibu umebadilika na kuwapata viongozi hao kwa cheo kipya cha kiranja Mkuu bila kujali jinsia.
Mradi wa My Rights My Voice ni mradi wa miaka mitatu (2012 – 2014) unaotekelezwa katika shule 16 za msingi na 4 za sekondari katika Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino kwa lengo la kuimarisha ari ya watoto kujifunza na kuanzisha mabaraza ya wanafunzi kwa kuendesha chaguzi za kidemokrasia katika kuwapata viongozi wake.
Mmoja wa washiriki wa mafunzo ya uanzishaji wa Mabaraza ya Shule kwa njia ya kidemokrasia yaliyotolewa katika kijiji cha Mvumi Misheni. Mafunzo hayo ni sehemu ya utekelezaji wa mradi wa Haki zangu Sauti yangu unaotekelezwa na mashirika yasiyo ya kiserikali ya Marafiki wa Elimu Dodoma (MED) na Women Wake Up (WOWAP) yote ya Dodoma kwa ufadhili wa Oxfam GB. Katika maoni ya washiriki hao waliomba suala la vifaa vya elimu hususan kwa wenye ulemavu lipewe kipaumbele.
WATAKA WABUNGE WAJITOKEZE KWENYE MIDAHALO.
Wananchi wa majimbo ya uchaguzi ya Mtera na Chilonwa katika Wilaya ya Chamwino Mkoani Dodoma wamewataka Wabunge wao kujitokeza katika mijadala inayowakutanisha ili wapate fursa ya kujadili juu ya matatizo yao. Wapiga kura hao waliyasema hayo katika mahojiano ya ufanisi wa mijadala ya Mahusiano baina ya Wabunge na wananchi inaypfadhiliwa na shirika la The Foundation for Civil Society na kuratibiwa na Asasi ya CHANGONET ya Wilaya ya Chamwino.
Wananchi hao wameeleza kuwa wanakabiliwa na kero mbalimbali ambazo Wabunge wao walipaswa kuzijadili pamoja na kuzipaia ufumbuzi lakini hawajitokezi kuwasikiliza na kuwasababishia usumbufu mkubwa. "hapa kijijini tunakabiliwa na matumizi mabaya ya ardhi na wakati mwingine wanakuja watu wanajifanya wawekezaji na kutudhulumu ardhi yetu, watetezi wetu hao wabunge hawaonekani" alisema Bibi. Kurwa Mkazi wa kijiji cha Manchali.
Wananchi hao walihoji sababu za baadhi ya viongozi wa kisiasa kushindwa kujitokeza katika mikusanyiko ya wananchi wakati wao ndio wahamasishaji wa maendeleo katika maeneo yao na kuwasimamia watendaji wa serikali.
Walimpongeza Mkuu wa Wilaya ya Chamwino Bi. Fatma Said Ally kutokana na juhudi anazozionesha kila wakati katika Wialya hiyo na kushauri viongozi wa kisiasa kuiga mfano wa kiongozi huyo. "Mkuu wa Wilaya ameteuliwa na Rais lakini anaonyesha kutujali na kushiriki kwenye mijadala; hao tuliowapigia kura wanajifanya wana kazi nyingi kila tukiwahitaji, kama hizo nafasi zina kazi nyingi waziache wapewe wengine"
Mijadala ya kuimarisha mahusiano na Wabunge katika Wilaya ya Chamwino imekuwa ikifanyika na kukosa ushirikiano wa karibu kutoka kwa Wabunge licha ya uongozi wa Wilaya na Halmashauri kutoa ushirikiano katika kufanikisha Mijadala hiyo.
Tangu mijadala hiyo ianze mwaka 2012 imekuwa ikihudhuriwa na viongozi wa ofisi za Mkuu wa Wilaya na Mkurugenzi wa Halmashauri ila Wabunge na Madiwani wamekuwa hawatoi ushirikiano wa kutosha.
MED YAANZISHA MFUKO WA ELIMU YA SEKONDARI CHIDACHI
Na. Barakaely Christopher
Shirika la Marafiki wa Elimu Dodoma (MED) kwa kushirikina na wananchi wa kata za Kikuyu Kusini na Mkonze Manispaa ya Dodoma wameanzisha mfuko wa kuwalipia ada na michango mingine wanafunzi wote watakaofaulu mtihani wa darasa la saba na kujiunga na elimu ya sekondari kutoka shule ya msingi Chidachi.
Lengo la mfuko huo ni kuwahamasisha wanafunzi wa shule ya msingi chidachi kuongeza juhudi kwenye masomo yao na kuwa na uhakika wa kuendelea na elimu ya sekondari.
Muasisi wa mfuko huo Bw. Davis Makundi ambaye pia ni Mlezi wa shule ya Msingi Chidachi na Mratibu wa Shirika la Marafiki wa Elimu Dodoma (MED) alianza kampeni ya kuanzisha mfuko huo Septemba mwaka jana katika mahafali ya nne ya darasala la saba ambapo mgeni rasmi alikuwa Meneja wa Benk ya Posta Tanzania Bw. Emmanueli Gyumi aliyemwakilisha Mkurugenzi Mkuu wa Benki ya Posta Tanzania.
Katika mkutano huo wazazi wa wanafunzi wa shule ya msingi Chidachi uliofanyika shuleni hapo wameomba mfuko huo uanze haraka na kuazimia kuwa wazazi wote wenye watoto katika shule hiyo wahusike kuchangia uendelevu wake ili kupunguza mzigo wa kusomesha watoto pasi na uhakika kutokana na kipato duni walichonacho. Akaunt ya Mfuko huo itafunguliwa katika Benki ya Posta Tanzania Tawi la Dodoma.
Katika mkutano huo wazazi walipokea jumla ya madawati 15 na seti moja ya bendi ya shule vyote vikiwa na thamani ya zaidi ya sh. 1,200,000 fedha ambazo zimetokana na michango ya wadau wa elimu, wazazi na wanafunzi kupitia kazi za mikono kwenye somo la Elimu ya Kujitegemea (EK).
Mwalimu Mkuu wa Shule ya hiyo Bi. Ashura Mhoji alieleza kuwa shule yake imekuwa ikifanya vizuri kwa kufaulisha wanafunzi kwa kati ya 80% hadi 100% kutokana na mwamko na ushirikiano uliopo baina ya walimu, wazazi, wanafunzi na wadau mbalimbali wa Elimu. Aidha alilishukuru shirika la MED kwa mchango wake mkubwa ambao limekuwa likitoa mara kwa mara katika shule hiyo. MED katika mkutano huo imechangia kiasi cha sh. 150,000 kwa ajili ya madawati na mfuko wa Elimu.
Meneja wa Mradi wa MRMV Bi Rehema Mwakajila akiwa na maafisa wa Asasi ya Marafiki wa Elimu Dodoma (MED) alipofanya ziara Mkoani Dodoma kwa ajili ya ufuatiliaji wa Mradi.