Log in
Wasaidizi wa kisheria Masasi

Wasaidizi wa kisheria Masasi

Masasi, Tanzania

Yale mafunzo ya ufahamu wa sheria kwa jamii yameanza 1/4/2016 kwenye kata ya Mwenge Mtapika ambako washiriki 25 toka mitaa ya Mbonde na Mayula wanashiriki. Mafunzo haya yamelenga kutoa ufahamu wa sheria za msingi: Sheria ya ardhi no 4&5 ya 1999, sheria ya mtoto na malezi, sheria ya ndoa ya 1971, sheria ya mirathi, sheria ya jinai na kazi na ajira. 

Kwa ujumla maendeleo na mahudhurio ni mazuri sana licha ya changamoto za hali ya hewa, mwingiliano wa shughuli za kijamii na sikukuu. Programu iliyopo ni ya kukutana kila alhamisi kuanzia saa 8 mchana hadi saa 11 na yatadumu kwa miezi 3 hadi mwezi Juni 2016.

Wawezeshaji ni WAKIHABIMA wenyewe kwa kutumia stadi walizofundishwa na ujuzi walionao katika masuala ya usaidizi wa kisheria na haki za binadamu.  

May 10, 2016
« Previous Next »

Add a comment

Your name:
Your location:
Your email:
(optional)
Your email address will not be published.