Fungua
Temeke Youth Development Network

Temeke Youth Development Network

Temeke/Chang'ombe, Tanzania

Maeneo ya ukurasa huu ni kwa Kiingereza. Hariri tafsiri
Kamati ya Utendaji TEYODEN yajipanga kutekeleza mradi wa Utetezi wa Mabinti wanaofanya kazi kwenye baa

Katika ile hali ya kuwajali wasichana wanaofanya kazi kwenye baa mbalimbali hapa jijini Dar Es Salaam,TEYODEN imeonelea ni vema ikajitahidi kuwatafutia suluhu ya maonevu wanayofanyiwa na wamiliki wa baa.

Katika kikao cha kamati ya utendaji kilichofanyika jumamosi ya tarehe 12 Juni 2010 katika ofisi za TEYODEN,kikihudhuriwa na mwakilishi kutoka Taasisi ya Maendeleo Shirikishi kwa vijana Arusha ( TAMASHA) yenye makao yake makuu katika jiji la Arusha,kaka Churchill Winston ambao ndio watakaokuwa wafadhili wa mradi huo na TEYODEN wakiwa ni wataalamu watafanya utafiti katika kata nne za manispaa ya Temeke ambazo ni Kurasini,Azimio, Keko na Mbagala katka baa zote zilizopo katika katika kata hizo ili kbaini ni changamoto zipi wanazokabiliana nazo mabinti hawa na jinsi ya kuzitatua wakiwashirikisha wamiliki wa baa hizo,wadau wa maendeleo katika manispaa ya Temeke na vijana mbalimbali.

Kabla ya kuingia katika mchakato huu kwanza yatakuwepo mafunzo ya namna ya kufanya utafiti huo.Mradi huo utakuwa ni wa mwaka mmoja.Kinachosubiriwa kwa sasa ni kibali kutoka wizara ya Sayansi naTeknolojia ambacho huenda kinatarajiwa kupatikana ndani ya mwezi huu.

TEYODEN itaendelea kushirikiana na mashirika mengine ikiwa ni katika kuimarisha mahusiano yake na asasi nyingine ndani na nje ya nchi.
19 Juni, 2010
« Iliyotangulia Ifuatayo »

Maoni (1)

Abdi Yazidu (Kata ya Toangoma) alisema:
Mimi naomba semina kama hizi zikitokea kila tawi litowe mtu mmoja.
21 Agosti, 2011

Ongeza maoni

Jina lako:
Mahali ulipo:
Email yako:
(sio lazima)
Anwani yako ya email haitachapishwa.