HISIA CULTURAL TROUPE-HCT
February 8, 2017 Iringa
HCT ni asasi iliyosajiliwa na Baraza la sanaa la Taifa (BASATA) kwa usajili namba BST/2365 na inajishughulisha na uelimishaji wa jamii kwa njia ya sanaa za maonyesho. Sanaa hizo ni kama vile maigizo shirikishi, vichekesho, utambaji wa hadithi na ushairi.
Aidha asasi yetu inaelimisha jamii katika maeneo mbalimbali kama vile kinga dhidi ya UKIMWI, athari za madawa ya kulevya, afya ya uzazi na ujinsia, utawala bora, utafiti, ukuzaji wa vipaji, michezo, elimu rika, utunzaji wa mazingira na uhamasishaji wa utalii wa ndani.
Sasa Asasi yetu inapokea vijana kwa ajili ya kufanya field. Vijana hao wawe na sifa zifuatazo:-
- Awe na ujuzi wa kutumia kompyuta
- Awe na uwezo wa kuandika proposal
- Awe na umri kuanzia miaka 18 hadi 35
- Awe na nidhamu, mwaminifu na mbunifu
Kwa mawasiliano zaidi piga namba zifuatazo:-
0754 439740
0786 439740
0715 474527
0652 600002
hisiaone@gmail.com
HISIA CULTURAL TROUPE-HCT IMEFUNGUA OFISI MPYA YA KUDUMU BAADA YA KUWA KATIKA HEKA HEKA ZA KUHAMA MARA KWA MARA
TUPO MAKUTANO YA MTAA WA JANGWANI NA MTWA, IRINGA MJINI
KARIBUNI SANA
KONGAMANO LA SANAA
WASANII wote mnaalikwa katika kongamano la sanaa za maonesho linalotarajiwa kufanyika Juni 15, 2013 hapa mkoani Iringa kuanzia saa 2:30 asubuhi hadi saa 11:00 jioni.
Kongamano litakuwa la siku moja na washiriki wanaomba kujigharamia kwa 100%. Pamoja na mada, kongamano litapambwa na burudani za sanaa za maonesho.
Watakaopenda kujitolea kuendesha mada na wale watakaopenda kuonesha sanaa zao katika kongamano hilo wajiandikishe mapema kabla ya Februari 2012.
Uratibu wa kongamano utagharamia chai na chakula cha mchana kwa washiriki wote katika siku ya kongamano.
Wasanii wote mnakaribishwa!
Limeandaliwa na:-
Hisia Cultural Troupe
S.L.P 436 Iringa
0754439740
Hisia tumehudhuria workshop ya wadau wa VVU/UKIMWI iliyofanyika manispaa ya Iringa. Pamoja na mambo mengine tumeweza kubadilishana uzoefu na asasi nyingine. Ni fursa nzuri za kujifunza ambazo tunazihitaji sana!