Envaya

HISIA CULTURAL TROUPE-HCT

February 8, 2017 Iringa

HCT ni asasi iliyosajiliwa na Baraza la sanaa la Taifa (BASATA) kwa usajili namba BST/2365 na inajishughulisha na uelimishaji wa jamii kwa njia ya sanaa za maonyesho. Sanaa hizo ni kama vile maigizo shirikishi, vichekesho, utambaji wa hadithi na ushairi.

Aidha asasi yetu inaelimisha jamii katika maeneo mbalimbali kama vile kinga dhidi ya UKIMWI, athari za madawa ya kulevya, afya ya uzazi na ujinsia, utawala bora, utafiti, ukuzaji wa vipaji, michezo, elimu rika, utunzaji wa mazingira na uhamasishaji wa utalii wa ndani.

Sasa Asasi yetu inapokea vijana kwa ajili ya kufanya field. Vijana hao wawe na sifa zifuatazo:-

  • Awe na ujuzi wa kutumia kompyuta
  • Awe na uwezo wa kuandika proposal
  • Awe na umri kuanzia miaka 18 hadi 35
  • Awe na nidhamu, mwaminifu na mbunifu

Kwa mawasiliano zaidi piga namba zifuatazo:-

0754 439740

0786 439740

0715 474527

0652 600002

hisiaone@gmail.com

 

large.jpg

Mwonekano wa cover ya "Mchunga ng'ombe"

large.jpg

Cover ya Filamu yetu "Mchunga Ng'ombe"

large.jpg

Wasanii wa Hisia wakiwa tamashani, Morogoro...

HISIA CULTURAL TROUPE ipo katika mchakato wa kuboresha shughuli zake na kuongeza shughuli za uelimishaji rika na nyinginezo za kijamii. Ukiwa kama mwanajamii tunahitaji sana ushauri wako katika kuboresha hilo ambapo kama jina litapitishwa itajulikana kwa jina

HISIA MEDIA AND COMMUNICATION ORGANIZATION--HIMCO

Ofisi yetu mpya imeshafunguliwa eneo la Mshindo iringa mjini. Mnakaribishwa sana kutuma maoni yenu kupitia

0754439740
hisiaone@gmail.com

KARIBUNI SANA MTUSHAURI....

large.jpg

Mashirikiano na mdau wa peace Corps

large.jpg

Maonesho ya uelimishaji vIJIJINI

HISIA CULTURAL TROUPE-HCT IMEFUNGUA OFISI MPYA YA KUDUMU BAADA YA KUWA KATIKA HEKA HEKA ZA KUHAMA MARA KWA MARA

TUPO MAKUTANO YA MTAA WA JANGWANI NA MTWA, IRINGA MJINI

KARIBUNI SANA

KONGAMANO LA SANAA

WASANII wote mnaalikwa katika kongamano la sanaa za maonesho linalotarajiwa kufanyika Juni 15, 2013 hapa mkoani Iringa kuanzia saa 2:30 asubuhi hadi saa 11:00 jioni.

Kongamano litakuwa la siku moja na washiriki wanaomba kujigharamia kwa 100%. Pamoja na mada, kongamano litapambwa na burudani za sanaa za maonesho.

Watakaopenda kujitolea kuendesha mada na wale watakaopenda kuonesha sanaa zao katika kongamano hilo wajiandikishe mapema kabla ya Februari 2012.

Uratibu wa kongamano utagharamia chai na chakula cha mchana kwa washiriki wote katika siku ya kongamano.

Wasanii wote mnakaribishwa!

Limeandaliwa na:-

Hisia Cultural Troupe

S.L.P 436 Iringa

0754439740

hisiaone@yahoo.com

www.envaya.org/hct

Hisia tumehudhuria workshop ya wadau wa VVU/UKIMWI iliyofanyika manispaa ya Iringa. Pamoja na mambo mengine tumeweza kubadilishana uzoefu na asasi nyingine. Ni fursa nzuri za kujifunza ambazo tunazihitaji sana!