Log in
Wasaidizi wa kisheria Masasi

Wasaidizi wa kisheria Masasi

Masasi, Tanzania

Washema imeendelea na shughuli zake za kutoa huduma za usaidizi wa kisheria na haki za binadamu. Wanachama wake wamesaidia jamii kwa kutoa elimu juu yamasuala ya kisheria katika kata za Nanganga, Chiungutwa, Mchauru, Namalenga, Mkomaindo na Lukuledi. Aidha kwa sasa inafanya utafiti wa kubaini makundi ya wanawake, vijana na walemavu ambao wanakosa fursa ya kugombea katika chaguzi mbalimbali. Utafiti na uibuaji huo umelenga kata za Chiungutwa, Nanganga na maeneo ya Mji wa Masasi. Baada ya utafiti huo kutaandaliwa mpango mkakati wa kuwezesha walengwa hao kujengewa uwezo ili waweze kushiriki na kugombea nafasi za uongozi wa serikali za mitaa Dec 2014 na udiwani na ubunge kwenye uchaguzi mkuu wa 2015 na kuongeza idadi ya wale wachache waliopo. Katika mradi huo Washema itahusisha asasi zingine zinazoshiriki katika masuala ya kujengea uwezo na utoaji wa elimu ya uraia.

October 31, 2014
« Previous Next »

Add a comment

Your name:
Your location:
Your email:
(optional)
Your email address will not be published.