UTANGULIZI
001-Wazee kata ya ndugumbi wilaya ya kinondoni mkoa wa dar es salam,wameanzisha umoja wao tarehe 01/01/2012 ukiwa na wanachama 53 kwa jina la UMOJA WA WAZEE NA MAENDELEO TANZANIA.
002-Umoja wa wazee na maendeleo umesajiliwa kisheria na msajili wa vyama tarehe 11/02/2013 namba ya usajili ni S.A.18539.
003-Umoja huu pia umefungua benki akaunti katika benki ya wananchi dar es salaam (DCB) tawi la magomeni dar es salaam.
004-Umoja wa wazee na maendeleo Tanzania unamadhumuni mbalimbali ikiwemo kufanyashughuli mbalimbali za kiuchumi na maendeleo za kujikimu kimaisha,sisi wazeekufanya shughuli mbalimbali za kiuchumi,kijamii za kimaendeleo kusaidia yatima,walemavu .nk.
005-Umoja wa wazee Tanzania ni umoja wa kitaifa Tanzania wa jinsia zote wanaume na wanawake kuanzia umri wa miaka 50 na kuendelea.Tanzania bara na visiwani kwa raia wa Tanzania tu.
006-Umoja wa wazee na maendeleo Tanzania kwa wakati huu unajiendesha kwa michango ya wanachama wake.
007-Kwa hivi sasa tumeanzia biashara ya kuuza soda na maji ya kunywa ya chupa.
008-Ofisi yetu na duka letu lipo KAGERA MIKOLOSHINI KATA YA NDUGUMBI WILAYA YA KINONDONI,MTAA WA NGUGU/KITEGA(TEXAS).
NYUMBA NA.03
ANUANI
UMOJA WA WAZEE NA MAENDELEO TANZANIA
MTAA WA NDUGU/KITEGA H/S NA O3
S.L.P 16340
DAR ES SALAAM
TANZANIA
e-mail:wazeetanzania@hotmail.com
Tovuti:www@envaya.org/uwt.
simu:0713 332660-Mwenyekiti
0716 584403-Makamu mwenyekiti
0715 072651-Katibu1
0715 287526-Mweka hazina