Parts of this page are in Swahili. Edit translations
tarehe 25/04/2010
kulitokea msakowa wafanya biashara ndogo ndogo katika manispaa ya dodoma .Hii ilikuwa imelengwa kwa watu wote ambao wanafanya biashara katika kituo cha mabasi ya usafirishaji mjini (Daladala)
Miongoni mwa waathirika katika zoezi hili walikuwepo wanachama wa kikundi chetu ambao wanafanya biashara ya samaki,nguo,viatu na mapambo ya nyumbani.
Waachama wetu wamepoteza baadhi ya mali zao ambazo zimekuwa zikiwasaidia katika kujikimu kimaisha na kuwapatia mahitaji yao yote ikiwemo lishe.
27/04/2010
Wanaachama walipita mitaani kuomba msaada ili kumnusuru mwanachama mwenzetu ambaye alipata ajali ya kuanguka na pikipiki na kuvunjika mguu pamoja na majeraha makubwa usoni.
Michango hiyo ilikuwa ni kwa ajili ya kumfanya apate matibabu sahihi,, tunatoa shukurani zetu kwa watu wote waliotuwezesha kwa michango mbalimbali
28/05/2010
Wanakikundi walihudhuria semina iliyoandaliwa na Halmashauri ya Manispaa ya Dodoma katika ukumbi wa Mambo Poa
Semina hiyo ilikuwa ni kuhusu lishe bora na matumizi sahihi ya ARV. Kwa kuwa kuna mahusiano makubwa kati ya chakula na dawa kwa waathirika wa VVU/UKIMWI na KIFUA KIKUU(TB).
Katika semina hiyo tulijifunza na kufahamu mambo mapya kuhusu VVU na Lishe bora. Pia ilikuwa nafasi nzuri ya kufahamiana na wenzetu wanaoishi na VVU, Katika semina hii tulianzisha mtandao unaoitwa WAVIU ili kufarijiana,kupeana moyo na mshikamano miongoni mwetu.
29/05/2010
Mwenyekiti wa kikundi chetu alihudhuria mkutano wa kila mwezi wa kamati ya maboresho ya huduma za CTC, Katika Hospitali kuu ya Mkoa kwakua yeye ni mjumbe wa kamati hiyo.
05/06/2010
Mwekiti wa TUPENDANE alihudhuria semina iliyoandaliwa na ENVAYA ili kuyawezesha mashirika kuwa na tovuti zao.
Wakufunzi wa ENVAYA walitufundisha namna ya kuweka habari zetu katika tovuti ili kufanya shirika letu kufahamika zaidi .
Wakufunzi wa ENVAYA akiwemo Bi.Radhina Kipozi walituelekeza vizuri namna ya kufungua tovuti na namna ya kuweka habari. Na kwamba huduma hii ni bure
Tunawashukuru ENVAYA kwa msaada mkubwa waliotupa kwa kuwa tusingeweza kuwa na tovuti yetu kutokana na ukubwa wa gharama za kuendesha tovuti.
kulitokea msakowa wafanya biashara ndogo ndogo katika manispaa ya dodoma .Hii ilikuwa imelengwa kwa watu wote ambao wanafanya biashara katika kituo cha mabasi ya usafirishaji mjini (Daladala)
Miongoni mwa waathirika katika zoezi hili walikuwepo wanachama wa kikundi chetu ambao wanafanya biashara ya samaki,nguo,viatu na mapambo ya nyumbani.
Waachama wetu wamepoteza baadhi ya mali zao ambazo zimekuwa zikiwasaidia katika kujikimu kimaisha na kuwapatia mahitaji yao yote ikiwemo lishe.
27/04/2010
Wanaachama walipita mitaani kuomba msaada ili kumnusuru mwanachama mwenzetu ambaye alipata ajali ya kuanguka na pikipiki na kuvunjika mguu pamoja na majeraha makubwa usoni.
Michango hiyo ilikuwa ni kwa ajili ya kumfanya apate matibabu sahihi,, tunatoa shukurani zetu kwa watu wote waliotuwezesha kwa michango mbalimbali
28/05/2010
Wanakikundi walihudhuria semina iliyoandaliwa na Halmashauri ya Manispaa ya Dodoma katika ukumbi wa Mambo Poa
Semina hiyo ilikuwa ni kuhusu lishe bora na matumizi sahihi ya ARV. Kwa kuwa kuna mahusiano makubwa kati ya chakula na dawa kwa waathirika wa VVU/UKIMWI na KIFUA KIKUU(TB).
Katika semina hiyo tulijifunza na kufahamu mambo mapya kuhusu VVU na Lishe bora. Pia ilikuwa nafasi nzuri ya kufahamiana na wenzetu wanaoishi na VVU, Katika semina hii tulianzisha mtandao unaoitwa WAVIU ili kufarijiana,kupeana moyo na mshikamano miongoni mwetu.
29/05/2010
Mwenyekiti wa kikundi chetu alihudhuria mkutano wa kila mwezi wa kamati ya maboresho ya huduma za CTC, Katika Hospitali kuu ya Mkoa kwakua yeye ni mjumbe wa kamati hiyo.
05/06/2010
Mwekiti wa TUPENDANE alihudhuria semina iliyoandaliwa na ENVAYA ili kuyawezesha mashirika kuwa na tovuti zao.
Wakufunzi wa ENVAYA walitufundisha namna ya kuweka habari zetu katika tovuti ili kufanya shirika letu kufahamika zaidi .
Wakufunzi wa ENVAYA akiwemo Bi.Radhina Kipozi walituelekeza vizuri namna ya kufungua tovuti na namna ya kuweka habari. Na kwamba huduma hii ni bure
Tunawashukuru ENVAYA kwa msaada mkubwa waliotupa kwa kuwa tusingeweza kuwa na tovuti yetu kutokana na ukubwa wa gharama za kuendesha tovuti.
June 9, 2010