Envaya

/jeanmedia/news: English: WI0000C9C806B33000011021:content

Base (Swahili) English

Mtweve: Kujitolea damu hakuna madhara.

Na ASIA KILAMBWANDA, Mtwara Community media

Meneja wa mpango wa uchangiaji damu salama kanda ya kusini, Mtweve Vincent amesema kuwa hakuna madhara yeyote yanoyoweza kutokea endapo mtu atachangia au kutoa damu kwa njia iliyo salama.

Mtweve amesema hayo wakati akiongea na mwandishi wa habari hii ofisini kwake juu ya tathmini ya mwamko wa jamii katika uchangiaji wa damu kwa hiari katika mikoa ya kusini inayaojumuisha mikoa ya Mtwara na Lindi pamoja na maeneo machache ya mikoa ya nyanda za juu kusini (BIG FOUR) ambayo ni maeneo ya Namtumbo na Tunduru.

“Hali ya hamasa ya uchangiaji wa damu kwa wananchi wa mikoa ya kusini imeshuka kutoka asilimia 60 hadi kufikia asilimia hamsini kwa mahitaji ya kanda na asilimia 65 hadi asilimia 35 kwa mahitaji ya lengo la kitaifa kutokana na imani iliyojengeka kwa jamii kuwa ukitoa au kuchangia damu unaweza kupata madhara ikiwa pamoja na magonjwa na kuongezeka kwa damu mara kwa mara”,Mtweve alisema.

Mbali na hali hiyo ya ushukaji wa uchangiaji wa damu salama lakini mpango huu umeonesha faida na hatua zilizofikiwa katika kupunguza idadi ya vifo vya kina mama na watoto katika kanda ya kusini na Taifa kwa ujumla.

Aidha kutokana na harakati zinazofanya na mpango huu,Hospitali ya Mkoa wa Mtwara (Ligula hospitali) imeripotiwa kutokuwa na idadi ya vifo vinavyotokana na wagonjwa wa upungufu wa damu kutokana na kupewa asilimia mia moja(100%) ya damu zinazochangiwa na jamii chini ya usimamizi wa Mpango wa uhamasishaji uchangiaji Damu salama kanda ya kusini.

Akielezea changamoto zinazosababisha kiwango cha uchangiaji damu katika mikoa ya kusini Mtweve amesema, hali ya makusanyo ya damu katika mikoa ya kusini imeshuka kutokana na asilimia kubwa ya wachangiaji kuwa wanafunzi ambao mara nyingi wengi wao hawana makazi ya kudumu jambo ambalo linasababisha kutofikia lengo.

“Kuanzia Januari hadi machi mwaka huu ni asilimia 35 tu za makusanyo ya damu yaliyopatikana katika mikoa ya kusini(Southern zone), makusanyo ambayo ni chini ya lengo la ukusanyaji wa damu lililowekwa kitaifa, hali hii inatokana na wachangiaji wakubwa kuwa ni wanafunzi,uelewa mdogo wa lengo la uchangiaji damu, mila potofu na umasikini hasa katika maeneo ya vijijini”,Mtweve aliongeza.

Kwa upande wa vikwazo vilivyoko mashuleni ni pamoja na wanafunzi wengi kutofikia vigezo vya utoaji wa damu ambavyo ni kuwa chini ya umri uliopangwa yaani miaka 18 na kuwa chini ya uzito wa kilogramu hamsini(50) ambapo mlinganyo wa waliofikia vigezo kuwa wachachezaidi ya wasio na vigezo.

Mbali na changamoto zinazoukabili uchangiaji wa damu kanda ya kusini, mpango huo umepanga kuhuisha uchangiaji damu kwa kujenga kituo kidogo(Satelite Centre) katika mkoa wa Lindi ambacho kitafanya makusanyo katika wilaya ya Lindi Mjini, pia umeanzisha Vikundi 35 vya vijana(Clubs) vinavyolenga kuhamasisha vijana katika uchangiaji wa damu.

Kwa upande wa taarifa iliyotolewa na Afisa Utawala wa mpango wa uhamasishaji uchangiaji damu salama Kanda ya kusini, Baraka Mfunguo Novemba 11, 2009 alitaja changamoto zilizopo mahospitalini kuwa ni pamoja na wagonjwa kuuziwa damu jambo ambalo ni kinyume na taratibu na lengo la mpango huo.

Hivyo kutokana na hali hiyo Mfunguo amewaomba baadhi ya watumishi wanaouza damu mahospitalini kutambua haki za watu wanaochangia damu kwa kutoa ushirikiano ili kazi ziende kwa ufanisi na kutoa hamasa kwa wananchi ili ongezeko la uchangiaji damu lipande.

Aidha aliwataka wananchi watakaoombwa rushwa ama kuuziwa damu kutoa taarifa katika vyombo vya sheria , taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa(PCCB), uongozi wa Hospitali na hata ofisi za uchangiaji damu salama watasaidiwa kwa kuwa kuongezewa damu bila malipo ni haki yao.

Mpango wa uchangiaji damu salama kanda ya kusini ulizinduliwa mnamo June 14, 2007 ambapo hivi sasa umeweza kupiga hatua ya kuokoa maisha ya watu waliokuwa wakipoteza maisha kutokana na upungufu wa damu hasa kinamama wajawazito na watoto jambo ambalo mwanzoni ilikuwa hadi ndugu wachangie damu tofauti na sasa.

Mtweve: Giving blood is no harm.

And Asia KILAMBWANDA, Mtwara Community Media

Manager of safe blood program of cost sharing of the southern region, Mtweve Vincent has said that no harm yanoyoweza occur if any person shall contribute or to give blood for a safe way.

Mtweve He said this while talking to the author of this information in his office on the assessment of awareness of the community in cost sharing of blood voluntarily in the regions south inayaojumuisha regions of Mtwara and Lindi with few areas of the provinces of Southern Highlands (BIG Four) which is Namtumbo and Tunduru areas.

"The impetus for cost sharing of blood to the people of the region of the south has fallen from 60 percent to fifty percent of the needs of the region by 65 percent to 35 percent for the needs of the target of national due to the belief iliyojengeka to the community that you give or donate blood, you can get effects, including diseases and increased blood regularly, "said Mtweve.

Besides the situation of ushukaji of cost sharing of safe blood, but this program has proved profitable and stage reached in reducing the number of deaths of mothers and children in the southern region and the nation as a whole.

Either from movements that make the program, Provincial Hospital of Mtwara (Ligula hospital) reported not having a number of deaths due to cerebral anemia due to be one hundred percent (100%) of blood zinazochangiwa and society under the supervision of Blood mobilization plan cost sharing safe zones in the south.

Referring to the challenges that cause the level of cost sharing of blood in the provinces of south Mtweve has said, a collection of blood in the regions of southern dropped due to a large percentage of contributors were students who often many of them do not have residence which leads to Little access to target.

"From January to March this year is only 35 percent of collections of blood found in regions of the south (Southern zone), collections which are below the target of collection of blood set nationally, this situation arises and contributors older that are students, limited understanding The goal of cost sharing blood, traditions and practices of poverty particularly in rural areas ", Mtweve added.

In terms of barriers existing schools include many students Little access criteria for the delivery of blood that is being under the age set for the 18 years and under the weight of a kilogram fifty (50) where the equation of who reached the criteria to be wachachezaidi of non-criteria.

Apart from the challenge zinazoukabili cost sharing of the blood region in the south, the plan is planned to streamline the cost sharing of blood to create the center bit (satellite Centre) in the region of Lindi which both the collections in the district of Lindi Urban, has also formed groups 35 youth (Clubs) vinavyolenga encourage young cost sharing in the blood.

In the case of a statement issued by the Administrator of the mobilization plan cost sharing zone south safe blood, Baraka key November 11, 2009 cited challenges that include hospitals and patients kuuziwa blood which is contrary to the procedures and purpose of the program.

So as the situation has to invoke some key ministers who sold blood in hospitals recognize the right of the people who donated blood to provide cooperation to go to work efficiently and provide impetus for both countries to increase cost sharing lipande blood.

Furthermore he urged people who be asked to corruption or kuuziwa blood provide information on media law, institutions of preventing and fighting corruption (PCCB), management of hospitals and even offices of cost sharing safe blood will be assisted by a blood transfusion without charge is their right.

Programme cost sharing blood safe zones in the south was launched on June 14, 2007 and now has been able to make progress to save the lives of people who had lost their lives due to anemia, especially Women pregnant women and children, which initially was to the brothers share their blood different from now.


In order to edit translations, you need to log in. Log in · Register

Translation History

Google Translate
April 15, 2011
Mtweve: Giving blood is no harm. – And Asia KILAMBWANDA, Mtwara Community Media – Manager of safe blood program of cost sharing of the southern region, Mtweve Vincent has said that no harm yanoyoweza occur if any person shall contribute or to give blood for a safe way. – Mtweve He said this while talking to the author of this information in his office on the assessment of awareness of the community in cost...