Envaya
Uru rupapuro ruragaragazwa mu rurimi rw'umwimerere Icyongereza. Edit translations


 

TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI

 

 Wawezeshaji wa Vikundi vya Walezi wa Watoto Wanaoishi katika Mazingira Hatarishi Zaidi

 

(01 Mei 2013)

WORTH ni mpango wa kuwawezesha wanawake, unaolenga kuwaelimisha ili waweze kujiwekea akiba na kuanzisha miradi/biashara zitakazowasaidia kujikwamua kiuchumi kwa manufaa yao na  Watoto Wanaoishi katika Mazingira Hatarishi zaidi,.

Mpango huu uko chini ya Kilio Cha Waathirika na Waathiriwa wa UKIMWI Tanzania (KIWWAUTA) na unatekelezwa  katika kata tano za wilaya ya Mbarali: Lugelele, Imalilo Songwe, Mapogoro, Ihahi na Ubaruku.

Asasi ya KIWWAUTA  inatangaza nafasi za kazi (Wawezeshaji wa Vikundi)  kwa watanzania  wenye sifa zifuatazo:-

Sifa za mwombaji:

  • Awe mwanamke mwenye umri usiopungua miaka 18
  • Awe amemaliza elimu ya msingi au sekondari na  mwenye uwezo wa kufanya mahesabu. Mwenye cheti cha mafunzo yoyote ana nafasi kubwa zaidi
  • Awe na uzoefu wa kufanya kazi za uhamasishaji jamii kwa kipindi kisichopungua miaka miwili
  • Awe mwenye uwezo wa kusoma na kuandika 
  • Awe tayari kufanya kazi katika mazingira ya vijijini na kutumia usafiri uliopo
  • Awe tayari kujifunza kuendesha baiskeli
  • Awe tayari kufanya kazi wakati wowote bila kufuatiliwa
  • Awe na uwezo wa kuongoza wengine kufanya kazi kwa pamoja kama kikundi
  • Awe ni mwenyeji wa eneo analo omba kufanya kazi.

Kazi za kufanya:

  • Kutembelea vikundi 10 - 12 vya wanawake walezi. Kila kikundi atakitembelea mara mbili au zaidi kwa kila mwezi
  • Kutoa taarifa ya maendeleo ya vikundi kwa msimamizi na mwajiri wake
  • Kuelimisha na kutoa ushauri kwa wanawake katika vikundi kuhusu maswala ya kibiashara na uwekaji wa akiba
  • Kuendesha semina mbalimbali kwa vikundi  kulingana na taratibu za mpango
  • Kushirikiana na  uongozi wa serikali katika utekelezaji wa mpango
  • Kuendesha shughuli nyingine zozote zinazoendana na mpango kama atakavyopangiwa na uongozi uliopo.

Mkataba na Mshahara:

Mwombaji mwenye sifa zilizotajwa hapo juu na atakayefaulu usaili  ataajiriwa kwa mkataba wa  miezi minne  na mshahara wa laki moja na nusu (150,000/=) kwa mwezi, pia atapatiwa baiskeli  moja kwa shughuli za mradi na ataruhusiwa  kurejea mkataba iwapo pesa za mradi zitakuwepo na kama ataonyesha ufanisi  mkubwa wa kazi.

Maombi yawasilishwe kwenye ofisi za Kata husika yakiambatanishwa na nakala za vyeti, historia fupi ya habari binafsi kuhusu masomo na kazi ulizowahi kuzifanya pamoja na nambari yake ya  simu ambayo anaweza kupatikana kwa urahisi kabla ya tarehe 20 Mei 2013.

 

Kwa mawasiliano na ufafanuzi zaidi.

Tafadhali usisite kwa kupiga namba hizi:-0763679590 au 0752029094.

 

 

 

28 Mata, 2013
Ahakurikira »

Tanga igitekerezo

Izina ryawe:
Aho uherereye
Your email:
(optional)
Your email address will not be published.