Envaya
Uru rupapuro ruragaragazwa mu rurimi rw'umwimerere Igiswayire. Edit translations

Katika kufanya ufuatiliaji wa mradi na tathimini ya ndani ya mradi ambao umefadhiriwa na The Foundation For Civili Sciety  viongozi wa asasi yetu ya KIOO wakifuatilia matokeo ya mradi wa ufuatiliaji wa matumizi ya umma ikiwa ni  pamoja namna wanajamii wanavyoshiriki katika kupanga mipango na namna wanavyofanya maamuzi juu ya hatima ya  vijiji vyao. Katika kile ambacho hakikutazamiwa na wafuatiliaji hawa wa mradi ni kule kupatikana kwa maelezo juu ya namna ambavyo mabaraza ya kata na vijiji yanayohusika na utatuzi wa migogoro kijijini ambavyo wametumia mwanya huo kujinufaisha kimapato.

Wakitolea mfano wananchi waliohojiwa na wafuatiliaji wetu walipopata habari hiyo wakiwa katika kijiji cha Mwandiga waliambiwa kuwa mabaraza hayo yamekuwa yakitoza hadi elfu hamsini (50,000) kwa kila mdaawa yaani mlalamikaji na mlalamikiwa jambo ambalo linaonesha kwamba barza hilo la kata lilikuwa limepokea migogoro 40 ambayo ni sawa na  shilingi 4,000,000/= zilizopatikana kutokana na migogoro hiyo lakini hakuna karatasi wala faili katika ofisi hiyo na mara zote wananungunika kukosekana kwa vitendea kazi.

Alipoulizwa juu ya hilo mtendaji wa kata hiyo Ndugu Mandari alikiri kuwapo kwa tukio hilo na kusema kwamba hii imetokana na ukweli kwamba watendaji wengi wakiwamo hao wanaotoza hela hizo hawana uelewa juu ya hilo.

Wakati huo huo pia wafuatiliaji wetu waligundua kuwa Halmashauri ya wilaya ya Kigoma ilikuwa imeanza kutekeleza wito wake kwa vitendo kwa kusambaza taarifa mbalimbali zikiwamo zile za mapato na matumizi kama zilivyokutwa kwenye mbao za matangazo katika kata mbalimbali zinazounda Halmashauri hii. Hatua hii kwa mradi wetu imekuja muda mwafaka na inatia matumaini na wito wetu katika hili ni kuendeleza juhudi hizi kila mwaka.

24 Gashyantare, 2011
« Inyuma Ahakurikira »

Ibitekerezo (0)

[Siba igitekerezo]

Tanga igitekerezo

Izina ryawe:
Aho uherereye
Your email:
(optional)
Your email address will not be published.