Envaya
Uru rupapuro ruragaragazwa mu rurimi rw'umwimerere Igiswayire. Edit translations

Taarifa kwa Waumini

BARAZA KUU LA WAISLAM TANZANIA {BAKWATA} – OFISI YA SHEIKH {w}

KAMATI YA MIPANGO NA FEDHA {w}

OFISI YA SHEIKH WA WILAYA YA SERENGETI-TEL:-+255 756 229 093/+255 713 417 921
E-mail:-
sheikhwaser@gmail.com Website: www.envaya.org/bakwataser


13/May/2013 = 3/Rajabu/1434

Utangulizi

                KAMATI YA MIPANGO NA FEDHA {w} ni kamati iliyoundwa na Sheikh wa wilaya mnamo tarehe 06/07/2012 sawa na terehe 15/Shaaban/1433h, zamani ilikuwa ikijulikana kama kamati ya maendeleo ya waislam Serengeti ili kuharakisha maendeleo ya Waislam Wilayani Serengeti.

                Fikra hizi zilipatikana baada ya kikao cha Kaimu Sheikh wa wilaya SHEIKH JUMA A. SIMBA alichokifanya mnamo tarehe 8/Muharam/1433h sawa na 2/12/2011 katika Msikiti wa FORT IKOMA kwa ajili ya maadhimisho ya mwaka mpya wa Kiislam. Miongoni mwa masuala yaliyojadiliwa siku hiyo ni pamoja na uimarishaji wa Uongozi, uimarishaji wa Uislam wilaya nzima na maendeleo ya Uislam Serengeti.

                Kamati hii imeanza shughuli zake rasmi tarehe 21/04/2013 sawa na 10/Jamadu Than/1434 baada ya kupata Uongozi wake rasmi, M/kiti wa kamati hii ni Ismail Nyamarege, Katibu wa kamati ni Abdallah M. Mgonja na mweka Hazina ni Muzammilu Kharid. Kamati imefanikiwa kufungua Akaunti katika Bank ya NMB tawi la Mugumu

Jina la Akaunti :- MFUKO WA MAENDELEO YA WAISLAM WILAYA YA SERENGETI

Namba ya Akaunti :- 30210001780

               

                Kamati inawaomba waumuini wote wenye NIA njema katika kuleta Maendeleo katika jamii ya Kiislam watoe michango yao kupitia akaunti hiyo, na ikumbukwe kuwa hiyo ni akiba isiyooza ambayo wataikuta mbele za Mungu baada ya umauti wao.

Miongoni mwa mambo ambayo kamati hii itakuwa ikiyafanya

  • Kupanga mikakati ya maendaleo katika wilaya na kutoa ushauri wa namna ya kupata njia/vyanzo vya mapato.
  • Kufatilia utekelezaji wa mikakati ya maendeleo kwa kushirikiana na Halmashauri ya BAKWATA {w}, kamati za misikiti, na kamati zinazotambulika.
  • Kutoa fedha kwa shughuli za maendeleo pale inapohitajika kwa ajili ya maendeleo na pia kufuatilia matumizi ya fedha zilizotolewa na kamati hii.
  • Kubuni vyanzo vya mapato vya kudumu.
  • Kupokea michango ya fedha/ maoni/ ushauri/ mapendekezo toka kwa waumini/ jumuiya yoyote ya Kiislam na Asasi/Kampuni itakayoguswa jitihada hizi za Kamati.

Mtume MUHAMMAD {S.A.W} anasema:-

“UMOJA NI REHMA NA UTENGANO NI ADHABU”

Tushikamane kwa pamoja kuleta Maendeleo Tanzania.

13 Gicurasi, 2013
« Inyuma Ahakurikira »

Ibitekerezo (7)

[Siba igitekerezo]
faida hassan potea njerekera (fourseasons safari lodge serengeti(bilila)) bavuzeko
nijambo jema sana pale mwenyezi mungu anapo waamusha watu kama nyie kuweza kuacha mambo yenu na kutuhimiza katika kufata misingi ya uislamu, na kukuza uislamu,ni jambo rakumshukuru mungu sana. ukizigatia na eneo halisi lenye mitiani mingi kuliko miko yote tanzania sisi tuko pamoja katika kuhakikisha umoja na undugu wetu unaimalika bila ya kubaguana alakini pia kunahaja yakutafuta jia mbadala za kuigiza kipato ,kama vile kumbuni jiya za ufugaji kilimo uchomaji tofali nk .katika kuogeza kipata,kwani lazimu tutambue ya kuwa mjini wa serengeti unapanuka kwa kasi sana kwahiyo inatupasa kuaza kutafuta maeneo ya kumiliki ili kuweza kuwa na kama shule hospita nk.
mungu abariki katika hili nami nauga mkono kwa dhati
asalamu
16 Gicurasi, 2013
Sheikh {W} Serengeti (Mugumu) bavuzeko
Wa alaykum salaam warahmatullah wabarakaatuh.
Bw, Faida Hassan,,, nimefurahi sana kupata maoni yako, kwanza tumuombe mola sote tuwe na afya, hekima na busara ktk kuimarisha dini.
pili tushikamane kwa pamoja wala tusifarakane.
16 Gicurasi, 2013
Sheikh {W} Serengeti (Mugumu) bavuzeko
na tatu maoni yako tutayafanyia kazi, japo yapo yaliyo ktk utekelezaji nayo mtafahamishwa yakiwa vizuri.
Tunaomba zaidi ushauri wenu kwa ajili ya ALLAH.
16 Gicurasi, 2013
Hassan De credo Mohamed (kampala) bavuzeko
Asallam Alleykum. Inapendeza sana kuona mawazo ya kuujenga mfuko wa mapato kwa waislam wa mugumu,ilihali faida yake sio kwa waislam wa wilaya ya serengeti tu.ila tunaomba moyo wa kuitumikia dini kwa mapato hayo.na isiwe ni mfuko wa kukusanya mapato kwa ajili ya watu wachache,na sio waislam. Malumbano yawekwe pembeni,waislam hueleweshanapale mtu anapokosea.na sio kugawanyika nakulumbana
17 Gicurasi, 2013
Sheikh {w} Serengeti (Mugumu) bavuzeko
Wa alaykum salaam,
bwana De Credo wa Kampala
napenda kukuhakishia kuwa hatufanyi maskhara, tupo hapa kwa ajili ya kutafuta radhi za ALLAH na si vinginevyo.
17 Gicurasi, 2013
[Siba igitekerezo]
Faida Potea (via email) bavuzeko
nashukuru sana kwakuchukua mdawako nakuweza kutufahamisha kinachoedelea wasalamu
f.hassan
18 Gicurasi, 2013
Omari Lusonzo (ASB (Bilila)) bavuzeko
Assalam alaykum,
Jazaq llahu kheir, Inshallah Allah abariki na kujaalia kila mipango tuliojiwekea iwe kwenye mafanikio. Pia na nyie wenzetu mliojitolea kulianzisha na kulisimamia jambo hili, Allah akujazeni kheir zake. Na sisi wengine ambao tupo nyuma yenu Allah atukunjulie nafsi zetu ili tuwe wamoja na wenye mshikamano katika kuipeperusha bendera ya Laa ilaha illa llah.
Na msichoke kutukumbusha kila wakati Inshallah.
Kwa ufupi tu kila kitu kimekaa vizuri humu na kinatia moyo, suala la kuboresha zaidi na hatimae kufikai kwenye malengo, hili ni jukumu lote sote sisi ka Waislam, Inshallah.
11 Kamena, 2013

Tanga igitekerezo

Izina ryawe:
Aho uherereye
Your email:
(optional)
Your email address will not be published.