Injira
VITONGOJI ENVIRONMENTAL CONSERVATION ASSOCIATION

VITONGOJI ENVIRONMENTAL CONSERVATION ASSOCIATION

chake-chake, Tanzania

Uru rupapuro ruragaragazwa mu rurimi rw'umwimerere Igiswayire. Edit translations

Vitongoji Environmental Conservation Association ni jumuia isio ya kiserikali inayojihusisha na uhifadhi wa mazingira. Ilianzishwa mwaka 1996 kufuatia tokeo  ambalo lilisababisha  watu 35  kupoteza maisha yao kwa ajili ya kula  nyama ya kasa  aliyesadikiwa kuwa na  sumu Tokeo hilo baya  ndio chanzo kikubwa cha kuanzishwa  kwa Jumuia hii.

 

Jumuiya hii  imepata usajili wake  mwaka 1997 na ina hati ya  usajili  no.33 chini ya sheria  no.6 ya Zanzibar ya mwaka.Miongoni mwa mafanikio yake  ni pamoja na :

  • Uhifadhi wa mazingira  ya  ukanda wa  pwani  mashariki ya  Kisiwa  cha Pemba
  • uhifadhi wa mikoko na mazalio ya viumbe vya baharini.
  • kuweza kuwapatia taaluma  ya uhifaadhi wa mazingira wananchi katika jimbo la  wawi na Wilaya ya Chake kwa ujumla  u oteshaji wa vitalu vya miti na upandaji  wa miti
  • kutambulika na jamii,serikali kuu na baadhi ya  mashirika
  • imeweza kufanya kazi na  mitandao ya mazingira (mfano ) MTAMAZA
  • tumeweza kufanya kazi  katika jimbo na wilaya wakati mwanzoni ilikuwa  ni viitongoji tu
  • tumeweza kupata watendaji  katika asasi na mafunzo mbali mbali ya uandaani  wa miradi na usimamizi wa fedha.