Envaya
Parts of this page are in Swahili. Edit translations

TEYODEN wafanya mkutano na wadau wa maendeleo ya vijana manispaa ya Temeke

Katika kujiandaa na  utekelezaji wa mradi wa kuongeza ari ya uwajibikaji wa vijana katika ushiriki na ushirikishwaji katika shughuli za kijamii na kimaendeleo ,leo TEYODEN imeanza utekelezaji huo kwa kufanya kikao na wadau wa maendeleo ya vijana katika manispaa ya Temeke,ambapo jumla ya washiriki 26 waliotakiwa kuhudhuria kikao hicho wote walihudhuria.Kulikuwa na maafisa wanne kutoka manispaa ya Temeke,maafisa watendaji 12 kutoka kata 12 za mradi huu na maafisa maendeleo ya jamii ngazi ya kata walioalikwa miongoni mwa kata  hizo za mradi,walikuwa 4.

Mradi huu utatekelezwa katika kipindi cha miezi 12 na jumla ya shughuli 10 zitatekelezwa,ambazo ni pamoja na kikao hiki ambacho tayari kimefanyika  leo,mafunzo kwa vijana 40 kutoka katika kata 12 juu ya stadi za maisha na sera ya maendeleo ya vijana ya mwaka 2007,ufuatiliaji na ukusanyaji takwimu za matokeo ya mradi,kutengeneza majukwaa 12 ya vijana,kuendesha midahalo 4 ya vijana ambayo itaibua changamoto zinazowakabili,kufanya ufatiliaji wa  shughuli hizona ukusanyaji wa matokeo ya mradi,uanzishwaji wa kizio cha kumbukumbu(database),utengenezaji na usambazaji wa vipeperushi elimishi,uendeshaji wa matamasha 4 ya wazi(road show) juu ya ushiriki na ushirikishwaji wa vijana katika masuala ya kijamii na kimaendeleo na ufanyaji wa tathmini ambayo itafanywa na mtathmini wa nje (external evaluator).

December 30, 2010
« Previous Next »

Add a comment

Your name:
Your location:
Your email:
(optional)
Your email address will not be published.