Injira
Temeke Youth Development Network

Temeke Youth Development Network

Temeke/Chang'ombe, Tanzania

Uru rupapuro ruragaragazwa mu rurimi rw'umwimerere Igiswayire. Edit translations

TEYODEN yajiandaa kuendesha mafunzo ya uanzishaji wa VICOBA Temeke

Katika kupambana na umaskini TEYODEN itaendesha mafunzo kupitia midahalo ya kila wiki kwa vijana wake juu ya uanzishaji wa benki za kijamii,maarufu kama VICOBA.

Mafunzo hayo yataendeshwa kwa njia ya midahalo na  mwezeshaji Gabriel Gesine aliyehudhuria mafunzo ya uanzishaji wa VICOBA yaliyoendeshwa na WWF ofisi ya Tanzania pale Maili Moja,Kibaha.

Mafunzo hayo yalihusisha juu ya uanzishaji wa vikundi,uongozi katika vikundi hivyo,uchaguzi huru,kanuni  na taratibu za ununuzi wa hisa na jinsi ya kukopa,mfuko wa jamii,uundaji wa katiba ya kikundi,utunzaji wa kumbukumbu za mahesabu,ununuzi wa hisa kwa mara ya kwanza,utoaji wa mikopo,ulipaji wa mikopo na jinsi ya utunzaji wa kumbukumbu za kila siku.


 


11 Ukuboza, 2010
« Inyuma Ahakurikira »

Ibitekerezo (1)

J Stern bavuzeko
Hongera kwa kazi njema kabisa!
12 Ukuboza, 2010

Tanga igitekerezo

Izina ryawe:
Aho uherereye
Your email:
(optional)
Your email address will not be published.