Log in
Temeke Youth Development Network

Temeke Youth Development Network

Temeke/Chang'ombe, Tanzania

Parts of this page are in Swahili. Edit translations

VIJANA WATOA MAONI JUU YA UBORESHAJI WA SHUGHULI ZA VIJANA HASA UJASIRIAMALI.

 

Masuala ya msingi yaliyozungumziwa.

-Nini vikwazo vya wajasiriamali vijana wa Temeke?

-Tutawafundishaje vijana jinsi ya kuweka mafunzo wanayopata kwenye vitendo?

Maoni kutoka kwa vijana.

Vaijana walisema kuwa,Semina zinazotoleewa ni za kubabaisha na huwa zinatolewa bila kufuata mfumo maalum ambao utawawezesha vijana kupata elimu inayokusudiwa. Kwa mfano kama semina ni ya siku mbili huwa inatolewa kwa siku moja ili kubana matumizi.Kwa mfumo huu vijana hawezi kuelewa na kuona semina kama sehemu ya mafunzo mabadala yake ni sehemu ya kujipatia fedha.

Vijana walipendekeza kuanza na vitu vidogo kwa uwezo uliopo na kwa wakati huu ili shughuli za ujasirimali zikue taratibu na kwa uhakika.

 Ili kukuza shughuli za mtandao na kuufanya uwe na vijana wengi,ungeafanyika ufuatiliaji wa shughuli za vijana ikiwemo Asasi ngapi za Temeke zinafanya kazi za vijana tuzialike kuleta vijana katika vikao vya mtandao.

 Hata hivyo kuna haja ya kubadilisha mtazamo wa mafunzo badala ya kufanya mafunzo ili vijana wapate pesa ni vyema kufanya mafunzo ili kuwafanya vijana wenye mahitaji waelimike na wajitegemee.

Mmoja wa wachangiaji alitoa angalizo kuwa hakuna maendeleo yanayoanzwa na watu 100, watu/vijana wachache wenye moyo na waliotayari ndio watakaoweza kuwaonyesha vijana wengine kama maendeleo yanawezekana.

Ni vyema sasa kubadilisha mfumo uliopo na Kukubali mifano iliyopo na kuitumia ili kupenyeza ujumbe kwa vijana katika vitu wanavyovipenda: Mfano sanaa, michezo,jogging,picnic mashindano ya mpira na masuala mengine.

August 7, 2012
« Previous Next »

Add a comment

Your name:
Your location:
Your email:
(optional)
Your email address will not be published.