Fungua
Temeke Youth Development Network

Temeke Youth Development Network

Temeke/Chang'ombe, Tanzania

Maeneo ya ukurasa huu ni kwa Kiingereza. Hariri tafsiri

MDAHALO WA VIJANA WARUDI KWA KASI MPYA NA MAARIFA ZAIDI.

Timu iliyoundwa kufanya uzinduzi wa mdahalo wa vijana uliobadilisha vikao vyake kutoka kila jumamosi na kuwa mara moja kwa mwezi ilifanya vizuri kwa kufikia 60% ya malengo yaliyowekwa katika kikao cha kamati ya utendaji cha TEYODEN cha hivi karibuni.Mdahalo huu uliohudhuriwa na vijana wapatao 70 na kuwezeshwa na bwana Ismail Mnikite ulifana sana ingawa ulichelewa kidogo kuanza.Mada ya mdahalo ilikuwa ni Ushiriki na ushirikishwaji wa vijana katika masuala ya kijamii na kimaendeleo na mada ndogo juu ya masuala ya katiba.Katika mada ya ushirikishwaji vijana waliweza kubungua bongo,kukubaliana na kujifunza maana ya ushiriki,ushirikishwaji na maana ya uwajibikaji.Pia walifunza masuala ya msingi ambayo vijana wanapaswa kushiriki ipasavyo,stadi za kujenga ili kuimarisha ushiriki wenye tija na wenye matokeo.

Mwisho wa Mada washiriki na mwezeshaji walikubaliana kuhairisha mada ya katiba ili irudiwe katika mdahalo wa mwezi wa 3(machi)

mdahalo ulitanguliwa na ufunguzi wa mwenyekiti taratibu za kushiriki na masuala ya utangulizi kutoka kwa kamati ya maandalizi na katibu wa TEYODEN.

7 Februari, 2012
« Iliyotangulia Ifuatayo »

Ongeza maoni

Jina lako:
Mahali ulipo:
Email yako:
(sio lazima)
Anwani yako ya email haitachapishwa.