Centre for Children and young people Development linaungana na dunia pamoja na watanzania wote kusheherekea siku ya wanawake duniani March 2012. Siku hii pekee inatupa nafasi ya kutambua mchango wa wanawake katika harakati ya kumkomboa mwanamke. Centre for Children a Young people and Adult Development linapenda kuadhimisha siku hii kwa kuikumbusha jamii ushiriki wa pamoja kwa kupinga unyanyasaji na ukatili kwa wanawake na watoto ambayo huadhimishwa kila mwaka mwezi December. Asasi inatambua mchango wa akina baba , vijana , watoto katika nguvu za pamoja katika kuleta mabadiliko na maendeleo ya kisasa.
Asasi inaungana na mashirika mengine kutambua mchango wao katika kutetea na kupigania haki ya mwanamke. Mwanamke wa leo ni shupavu , jarisi na ameonesha anao uwezo wa kufanya mambo mengi bila kuwa tegemezi . Wanawake wa Tanzania ni mhimili wa Taifa letu ambalo ndilo linajenga maendeleo ya nchi yetu. Daima tusonge mbele.