Log in
CHAMA CHA MAENDELEO YA KIUCHUMI NA KIJAMII VUGA

CHAMA CHA MAENDELEO YA KIUCHUMI NA KIJAMII VUGA

LUSHOTO, Tanzania

Parts of this page are in Swahili. Edit translations

large.jpg

WANANCHI WA KIJIJI CHA KIDUNDAI WAKIWA KATIKA MKUTANO ULIYOANDALIWA NA CHAMAKIVU

March 13, 2012
« Previous Next »

Comments (12)

moses v moses (Dar) said:
Nafurahi nikiwaona wenzangu wa Kidundai,lakini mimi ni mkazi wa Vuga tumekuwa na wakati mgumu sana japo kuwa tuna zalisha matunds lakini tunauza kwa bei ndogo sana ambayo haikidhi mahitaji ya familia zetu.Mimi nimekulia mjini lakini kila wmaka lazima niende kusalimia wazee.Nokuomba kama inawezekana tufanyie swala la maji na umeme kwetu ili lisiwe kama ndoto kwani mama,bibi na ndugu zetu wengine wamekuwa na tatizo hili mpaka wamezoea.thanks
Its me moses v moses.
June 29, 2012
Jumaa dhahabu (ndolwa) said:
hasante sana bw: Moses kwa ushauri wako wako lakini ningependa kukwambia kuwa Asasi za kiraia zipo kwa ajiri ya kutoa ufahamu/uelewa kwa wananchi juu ya maswala ya kiuchumi na kijamii na muishauri serikali juu ya kuchukuwa maoni kwa wananchi na kuweka vipaumbele mpaka sasa chamamkivu imetoa mafunzo ya kilimo kwanza,uandaaji wa miradi ya kiuchumi na kijamii,usimamamizi wa maswala ya fedha na jinsi ya kuandaa mpango mkakati kwa vikundi vya bazo,vuga,kuluai na baghai kuhusu swala la umeme mpaka sasa mbunge wetu Januari makamba amezidia kuendelea na atua iyo mpaka sasa tayari majengo yameshachimbiwa vuga bazo na kumeanza kwa mradi wa umwagiliaji katika kijiji cha kishewa lakini tunaamini vuga itajengwa kwa ushirikiano na wadau mbalimbali ukiwemo ww pia bw: moses na kuitangaza kwa wadau wa maendeleo ukizingati ni mji wa kiistoria kwa chifu mtemi kimweli na kiunguni mrima kwa mongo n.k
July 19, 2012
moses moses (via email) said:
OK! NIMEKUPATA SANA KAKA NA NIMEIPENDA SANA HIYO MI PIA NAPENDA NIONE SIKU MOJA WAZEE WETU WANA RUKARUKA KWA FURAHA KATIKA SUALA HILI PIA WANA PATA HUDUMA NZURI ZA KAIFYA.OK! KWENYE CHAMA HICHO KUNA KUJIANDIKISHA AU NDO INAKUJAE.PIA MIMI NI MKAZI WA HUKO TENA VUGA KIHITU.
THANKS
July 20, 2012
Jumaa dhahabu (vuga bazo) said:
katika kata ya vuga kuna vikundi vingi ambavyo vinachangia katika kuakikisha vuga inabadilika kwa namna mmoja au nyingine kuna kikundi cha mazingira,ambacho kinajishughulisha na maswala ya upandaji miti. kuna kikundi cha vijana cha mwela vuga ambacho kina jishughulisha na maswala ya utawala bora ususani kufahamu umuhimu wa wananchi kushiriki katika mikutano ya serikali za vijiji na kudai/kuoji taalifa za mapato na matumizi na kufatilia rasilimali za umma pia kuna kikundi cha upendo group kinajishughulisha na maswala ya kilimo cha chai na mpaka sasa tuna miche mingi ya chai, kuna kikundi cha ufugaji sasa sijui ww unaitaji kikundi gani kati ya hivi sababu Chama cha maendeleo ya kiuchumi na kijamii vuga wanachama wake ni vikundi sio mtu binafsi na sasa kama livyokueleza tupo kwenye atua ya kuvijengea uwezo wa maswala mbalimbali mf: jinsi ya kutengeneza bajeti.katiba.ubunifu wa miradi na nk karibu sana tuje kuijenga vuga karibu sana tuje kuijenga Bumbuli karibu sana tuje kuijenga Lushoto karibu sana tuje kuijenga Tanga na Tanzania kwa ujumla
July 20, 2012
zulfa adam (dar) said:
nami niko pamoja nawe kaka moses la kuongeza ni kwamba suala la maji pia lipewe kipaumbele kwani wakumbuke kwamba kisima kimetoka kihitu lakini still kihitu hatuna maji.zulfa adam
June 11, 2013
moses v Moses (Dar) said:
Nikitaka kuwa member nifanyeje
June 12, 2013
zulfa adam (dar) said:
mm ni mzaliwa wa kihitu, tatizo langu kubwa ni kuhusu shule ya sekondari kihitu,ijapokuwa baadhi ya wazazi wamekuwa na muamko wa kupeleka watoto wao sekondari lakini nadhani bado wanahitaji kuelimishwa nini maana ya kusoma,kwani kwa mfano tunauona wamefeli lakini hawajarudi tena shule,wameamua kufanya wajuayo.tafadhali kama tatizo ni walimu tunaomba waongezwe kama ni wazazi basi wapatiwe mafunzo maalum.
June 12, 2013
Moses (Dar es salaam) said:
Zulfa kumbe wewe ni jirani angu its true,Nimeona watu wanaenda Bazo lakini cjui kama wanajua umuhimu wa kusoma
June 14, 2013
Zulfa adam (dar) said:
asante ndugu yangu kwa kulitambua nawe je tunadhani kwa njia hii elimu kwetu itaboreshwa,je siku moja tutakuja kukuta wanaosoma sayansi wana maabara,wanaoacha shule wanachukuliwa hatua,wanaozalisha wanafunzi wanachukuliwa hatua?Mm natamani siku moja kijiji chetu kiwe mfano kwa vingine.Asante.
June 21, 2013
Moses V Moses (Dar es salaam) said:
Pia itakuwa furaha sana nikiona umoja ambao wana Vuga na vitongoji vyake bila kujali itikadi za dini wala kabila tunadumisha umoja wetu.Pia watoto wetu wanasoma vizuri nimetembea sana hakuna mahali pazuri kama hapo kwetu kama kweli tutapata shule nzuri ya boarding na walimu ukweli tutakuwa the best
June 24, 2013
Zulfa (dar) said:
je tufanye nn ili wanakiji pamoja na vitongoji vyake tuwe pamoja katika kufanikisha zoezi hilo,kwani nafahamu kwamba viongozi wanatambua, je kuna uwezekano gani unaweza kufanyika kuhikisha uboreshaji wa elimu na asasi nyingine unakuwa imara?
June 24, 2013
Zulfa (dar) said:
vipi kuhusu umeme mbona nguzo tu mpaka leo,jamani,mia mitano inaisha mbona hata jambo moja bado,umeme nguzo tu,maji ndio kwanza hata mitalo bado.Mpaka lini jamani.
August 21, 2013

Add a comment

Your name:
Your location:
Your email:
(optional)
Your email address will not be published.