Base (Swahili) | English |
---|---|
HABARI ZINAZOHUSU WANAKIKUNDI WA WEMA - MKALAPA, WILAYA YA MASASI 1. WANAHARAKATI WA ELIMU, MAZINGIRA NA AFYA - WEMA, WAENDESHA MJADALA WA WAZI KATIKA MJI MDOGO WA NDANDA, MASASI Tarehe 03 Mei 2010, Wanaharakati wa Elimu, Mazingira na Afya-WEMA, waliendesha mjadala wa wazi uliofanyika katika mji mdogo wa Ndanda uliopo katika wilaya ya Masasi. Katika mjadala huo watu mbalimbali wakiwamo; wadau wa elimu, wazazi, wanafunzi pamoja na wanaharakati wa Elimu, Mazingira na Afya, walishiriki katika mjadala huo. Mada katika mjadala huo ilikuwa; "Namna disco toto na kumbi za starehe zinavyoathiri watoto na wanafunzi kujifunza." Mjada huo uliongozwa na Mchungaji Joseph Mwanga ambaye pia ni Mtunza Fedha wa kikundi cha WEMA, pamoja na Mr. Allyi K. Kamtande, Katibu wa kikundi cha WEMA. Washiriki wote waliohudhuria walikubaliana na mada ambayo iliwasilishwa kwa ustadi mkubwa na waongoza mjadala. Waongozaji wa mjadala walitoa mifano mingi ya jinsi "disco toto" zinavyowapawisha watoto kiasi kwamba hawasikilizi makatazo ya wazazi wao. Kwa upande wa pili waongozaji wa mjadala walielekeza lawama kwa baadhi ya wazazi ambao hutoa fedha na kuwapatia watoto wao ili waende kwenye "disco toto" ama kuangalia picha kwenye kumbi za video, wakidhani kuwa kufanya hivyo wanaonesha mapenzi kwa watoto wao. Katika kuunga mkono hoja hiyo, wapo waliosema kuwa kukithiri kwa kumbi za video vijijini ndiyo kichocheo kikubwa cha matendo ya ngono, na hatimaye kuongezeka kwa mimba za wanafunzi. Aidha, wengine walisema kitendo cha mtoto kwenda kwenye kumbi za starehe kunawakutanisha watoto wenye tabia nzuri, na watoto wenye tabia mbaya kama ile ya uvutaji bangi. Matokeo yake, watoto wazuri hujikuta wakijiingiza katika matendo ya uvutaji bangi pamoja na unywaji wa pombe. Wachangiaji wengine walienda mbali zaidi kwa kuhusisha swala la kuendekeza starehe na taaluma. Walielezea kuwa, hali ya morali ya usomaji (kujisomea) kwa wanafuzi siku hizi haipo kabisa. Walibainisha kuwa hakuna mwanafunzi anayerudi shuleni akachukua daftari ama kitabu na kujisomea. Matokeo yake ni kushuka kwa taaluma. Washiriki walibainisha wazi kuwa hali ni mbaya zaidi vijijini ambako walimu ni wachache na pia kuna upungufu mkubwa wa vitabu. Washiriki walipendekeza kuwa mijada ya aina hii ni muhimu na kwamba inafaa ifanyike mara kwa mara na katika maeneo tofauti kwani inasaidia kuleta changamoto kwa wananchi. Mjadala huo ulifadhiliwa na shirika la hiari la HakiElimu. Wanaoonekana kaktika picha ni watoto (wanafunzi) wakisasambua kiduku (aina mojawapo ya uchezaji) kama walivyokutwa na mpiga picha katika moja ya kumbi zilizopo katika mji mdogo wa Ndanda. (Taarifa hizo za mjadala wa wazi zimechapishwa katika magazeti mbalimbali likiwemo gazeti la Mwananchi Na. 03629 la tarehe 25 Mei 2010 uk.10 na Mwananchi Na. 2 linalozungumzia 'Maarifa' uk.2, mada maalumu inayohusu ELIMU.)
|
Members related NEWS OF KINDNESS - MKALAPA, Masasi District 1. Activists EDUCATION, ENVIRONMENT AND HEALTH - good, run of opening a debate in the small town of Madanda, Iqaluit On May 3, 2010, activists of Education, Environment and Health-good, they run an open debate held in the small town of Ndanda located in Masasi District. In the discussion they are different people, the stakeholders of education, parents, students and activists of Education, Environment and Health, participated in the debate. Topic of the debate was: "How toto disco and entertainment venues affect children and students learn." Jada was led by Pastor Joseph Mwanga, who is also treasurer of the group of good, with Mr. Allyi K. Kamtande, secretary of the group of good. All participants and attendees agreed that the subject was presented with great skill and led the discussion. Directors of the debate gave many examples of how "disco toto" zinavyowapawisha so that children do not listen to the prohibition of their parents. On the other directors of the debate focused blame for some parents who spend money and give their children to go to the "disco toto" or looking at pictures in the halls of the video, they think that doing so they show love for their children. In support of this argument, there are some who say that the conditions get the video halls in rural areas is the catalyst for sexual acts, and ultimately increased student pregnancy. Moreover, some said the practice of child comfortable going into venues kunawakutanisha children with good character, and children with bad behavior like that of smoking marijuana. Consequently, the good kids are finding themselves involved in acts of smoking marijuana and alcohol. Other contributors were going to involve far more comfortable and adapted the concept of professionalism. Explaining that the morali of reading (reading) to shoulder these days do not exist at all. Walibainisha that no student who returned to school and took a notebook or a book to read. The result is a decline in professionalism. Participants were clear that the situation is worse in rural areas where teachers are scarce and there is also a serious shortage of books. Participants suggested that this kind Jada is important and that should be done regularly and in different places because it helps bring challenges to the public. The debate was sponsored by a voluntary organization of HakiElimu. Wanaoonekana kaktika pictures are children (students) were sasambua duiker (a form of play) as they vyokutwa and photographer in one of the venues available in the small town of Ndanda. (These reports are for discussion obviously been published in various magazines including newspaper The Citizen And. 03,629 dated May 25, 2010 by The Citizen and uk.10. 2 linalozungumzia 'knowledge' p. 2, specific topics relating to education.) |
Translation History
|