Envaya

/ndanda/projects: English: WI0005481A35869000003859:content

Base (Swahili) English

KAZI NA SHUGHULI ZINAZOSHUGHULIKIWA NA KIKUNDI CHA "WANAHARAKATI WA ELIMU, MAZINGIRA NA AFYA" (WEMA)

1. Kikundi cha WEMA kinaendesha Maktaba ya Jamii ambayo ipo katika kijiji cha Mkalapa kilichopo wilaya ya Masasi. Maktaba ya WEMA ina vitabu vinavyokidhi mahitaji ya watu wa viwango mbalimbali vya kitaaluma kuanzia elimu ya watu wazima, elimu ya Awali, elimu ya Msingi, Sekondari, hadi chuo kikuu. Sababu kubwa iliyokichochea kikundi cha WEMA hadi kufanya maamuzi ya kuanzisha maktaba ya jamii ni hali halisi ya uhaba wa vitabu katika shule nyingi za Awali, Msingi, na Sekondari katika wilaya ya Masasi.

Kikundi cha WEMA kinadhani kwa kuanzisha maktaba hiyo ya jamii katika kata ya Mwena, kutawasaidia wanafunzi wanaosoma katika shule mbalimbali zilizo jirani na maktaba hiyo kupata fursa ya kuitumia maktaba kwa lengo la kuinua kiwango chao cha taaluma.

2. Kikundi cha WEMA kimeanzisha pia shughuli za kiufundi na kiuchumi chini ya kitengo kinachojulikana kama; "WEMA ART AND CARPENTRY SKILLS PROMOTION" kwa kifupi kitajulikana kama WACS-Promotion.

Lengo la WACS-Promotion ni kuwapatia ujuzi na utaalamu vijana watakaopenda kujifunza fani za useremala, sanaa za uchoraji na uchongaji vinyago. Kwa upande mwingine kikundi kitakuwa ni chanzo kingine cha mapato. WACS-Promotion watakuwa chini ya usimamizi na uratibu wa WEMA kama ambavyo shughuli nyingine za WEMA hufanyika.

WACS-Promotion kama kikundi cha ujasilia mali na mafunzo,kwa ujumla wake watajishughulisha na mambo yafuatayo; i/ Kutoa mafunzo ya ufundi wa seremala kwa vijana chini ya usimamizi wa mtaalamu kutoka chuo cha VETA Ndanda, ambaye pia ni Mwana-WEMA. ii/ Kufanya kazi za kiufundi zikiwemo; utengenezaji wa samani pamoja na shughuli za ujenzi kwa watu wa kawaida wanaohitaji huduma hiyo zikiwamo shule, zahanati, n.k. kwa gharama nafuu. iii/ Kuanzisha shughuli za uchongaji wa vinyago, uchoraji n.k. kwa kuwashirikiisha wataalamu mabingwa wa kazi hiyo ili baadaye waweze kutoa ujuzi huo kwa vijana watakaopenda kujifunza fani hizo.

3. Wanaharakati wa Elimu, Mazingira na Afya - WEMA, wameanzisha pia kitengo kinachojishughulisha moja kwa moja na maswala yanayowahusu wanawake. Kitengo hicho kinajulikana kama; "WEMA WOMEN EMPOWERMENT GENERATION," kwa kifupi kitajulikana kama WEMA Women-EG.

WEMA Wommen-EG wanaamini kwamba mwanamke akijengewa uwezo na uelewa wa kutosha katika mambo ya elimu, mazingira, uchumi, michezo na afya atakuwa na uwezo wa kukabiliana na maisha, hatimaye kujijengea uwezo utakaomwezeshya kujikwamua kiuchumi, na kuwa tegemeo katika familia. Aidha, WEMA Women-EG wanaamini kuwa mwanamke mmoja akielimika katika familia, basi familia nzima imepata kukombozi unaoihakikishia familia hiyo maisha bora.

WEMA Women-EG katika kumletea mwanamke changamoto ya maendeleo watajishughulisha na mambo yote yaliyoainishwa ndani ya katiba ya WEMA, ambayo ni; Elimu, Mazingira, Afya, Uchumi pamoja na Michezo.

Katika elimu watawahamasisha wasichana ili watilie mkazo elimu kwa mtazamo kwamba kila msichana anayeandikishwa shule, asiishie njiani. Katika mazingira wamejipanga kuhakikisha wanaifikisha elimu sahihi kwa wanawake wote juu ya namna ya kutunza vyanzo vya maji, na kuwaelimisha ubaya wa kukata miti ovyo, bila kupanda mingine. Aidha watawahamasisha wanawake wenzao juu ya umuhimu wa kutumia majiko yasiyotumia kuni nyingi pamoja na utunzaji wa mazingira kwenye makazi wanayoishi. Kwa upande wa afya watashirikiana na asasi nyingine za kijamii na kiraia katika kampeni mbalimbali zinazohusu afya mfano; mapambano dhidi ya malaria, kunawa mikono, usafi wa mazingira, VVU na kinga dhidi ya UKIMWI.

Aidha, watajihusisha pia kuwapatia elimu wasichana wadogo waliopata mimba katika umri mdogo, ya namna ya kutunza mimba ili kuwawezesha kujifungua salama. Pia watatumia nafasi hiyo kukemea tabia ya kuendekeza vitendo vya ngono wangali bado wadogo. Kwa upannde wa uchumi watawatumia wataalamu wanaopatikana katika maeneo yao ili wapatiwe elimu ya usindikaji matunda na uhifadhi, utengenezaji wa vyungu vya kupandia maua, utengenezaji wa batiki, ususi, ubanguaji wa korosho, pamoja na elimu ya biashara. Kwa upande wa michezo WEMA Women-EG watawaunganisha wasichana wa rika tofauti tofauti kwa lengo la kuunda vikundi vya michezo ili kwa pamoja waweze kucheza michezo mbalimbali kama sehemu ya mazoezi. Kila baada ya mazoezi watapatiwa ujumbe unaohusu jambo lolote; mfano, Wachezaji msidanganyike, UKIMWI bado ni tishio.

4. Shughuli nyingine zitakazofanywa na WEMA ni pamoja na kukusanya kazi za sanaa za zamani kutoka kwa makabila manne ya mikoa ya Mtwara na Lindi ambayo ni; Wamakuwa, Wayao, Wamwera na Wamakonde kwa lengo la kuzihifadhi ili kizazi kilichopo na kijacho waweze kuona na kujifunza sanaa za wazee wao ambazo kwa sasa zimetoweka machoni pa watu wengi.

WORK AND ACTIVITIES ZINAZOSHUGHULIKIWA by a group of "activists EDUCATION, ENVIRONMENT AND HEALTH" (EMA)

1. Group houses conduct EMA Community Library which is located in the village of Masasi District Mkalapa located. The library has good books vinavyokidhi needs of people from different levels of academic adult education, education, Primary education, Secondary, to the university. The main reason iliyokichochea group of EMA to make decisions to establish a community library is a situation of shortage of textbooks in many schools of Early, Primary and Secondary in Masasi District.

Do you think of the good group to introduce the library community in the county of Menna, will help students who study in nearby schools and libraries that are getting the opportunity to use the library in order to raise their level of professionalism.

2. EMA also has set up a group of technical and economic activities under the unit known as, "good ART AND CARPENTRY Skills Promotion" for short kitajulikana as ACS-Promotion.

The goal of ACS-Promotion is giving young people the skills and expertise who would like to learn the profession of carpentry, the art of painting and sculpture. On the other hand the group will be a source of income. ACS-Promotion will be under the supervision and coordination of activities that are good as other good deeds done.

ACS-Promotion as a group of ujasilia resources and training, generally are concerned with the following: i / Provide vocational training of the carpenter for youth under the supervision of a specialist from the College of VETA Ndanda, who is also son-good. Ii / To technical work, including: manufacture of furniture and construction activities for ordinary people who need the service zikiwamo schools, dispensaries, etc.. affordable. iii / Develop activities sculpture of toys, painting, etc. kuwashirikiisha champions of working professionals in order to later be able to provide the skills for youth who want to learn the profession.

3. Activists of Education, Environment and Health - good, they have also formed a unit kinachojishughulisha directly with issues that affect them women. The unit known as: "Goodness Generation Women Empowerment," for short kitajulikana as good Women-EC.

EMA Wommen-EC believe that a woman was structured ability and understanding enough in matters of education, environment, economy, sports and health will be able to cope with life, eventually building capacity will kaomwezeshya get rid economically, and that the staff in the family. Moreover, good-EC Women believe that one woman was educated in the family, then the whole family has gained redemption is oihakikishia family a better life.

EMA-EC Women in development to bring her challenge will be engaged in everything outlined in the constitution of the EMA, which are: Education, Environment, Health, Economics and Game.

In education will encourage girls to pay special emphasis on education for the view that every girl who is enrolled in school, not to stop along the way. In the circumstances are lining up to make sure they ifikisha education appropriate for all women on how to protect water sources, and educating the evil of cutting trees carelessly, without planting another. Either you will encourage other women about the importance of using stoves yasiyotumia fuel and environmental conservation in homes they live. In terms of health shall collaborate with other institutions of society and society in the campaign range relating to the health model, the fight against malaria, wash hands, clean the environment, HIV and AIDS prevention.

Moreover, they also engaged in providing education little girls who get pregnant at a young age, how to preserve the pregnancy to enable safe delivery. It also will use the opportunity of denouncing the behavior of adapted sexual acts are still young. In upannde the economy will use expertise available in their areas to receive schooling of processing fruits and storage, manufacture of pots with planting flowers, making bless, sewing, ubanguaji of cashews , with knowledge of the business. In terms of games EMA Women-EC will united girls age...


In order to edit translations, you need to log in. Log in · Register

Translation History

Google Translate
March 21, 2011
WORK AND ACTIVITIES ZINAZOSHUGHULIKIWA by a group of "activists EDUCATION, ENVIRONMENT AND HEALTH" (EMA) – 1. Group houses conduct EMA Community Library which is located in the village of Masasi District Mkalapa located. The library has good books vinavyokidhi needs of people from different levels of academic adult education, education, Primary education, Secondary, to the university. The...