Base (Swahili) | English |
---|---|
4. UZINDUZI WA MAKTABA YA JAMII YA WEMA - MKALAPA Tarehe 11 Julai 2009 iliambatana na tukio muhimu na la kihistoria katika kijiji cha Mkalapa. Kijiji cha Mkalapa kipo katika wilaya ya Masasi mkoani Mtwara. Kikundi cha Wanaharakati wa Elimu, Mazingira na Afya-WEMA walizindua rasmi Maktaba yao ya Jamii ya WEMA ambayo ina vitabu na machapisho zaidi ya 750. Vitabu vilivyomo kwenye maktaba ya WEMA vimechangiwa na wafuatao; HakiElimu (machapisho na vitabu zaidi ya 150), Mratibu na mshauri wa kikundi Mr. Mussa P.M. Kamtande (amechangia vitabu na machapisho zaidi ya 450), pamoja na taasisi kama; Chuo cha Ualimu Mtwara (K), na Chuo cha Ualimu Mtwara (U), ambao kwa pamoja wamechangia machapisho yapatayo 150. Katika picha hapa chini anaonekana Mwenyekiti wa Kikundi cha WEMA Mr. Fidelis Milanzi akiwa na mgeni rasmi Mr. Richard Lucas wakiangalia vitabu kwenye maktaba hiyo. |
4. UZINDUZI THE LIBRARY OF THE SOCIETY OF KINDNESS - MKALAPA On July 11, 2009 was here accompanied by an important and historic event in the village of Mkalapa. Village of Mkalapa is in Masasi district in Mtwara. A group of activists of Education, Environment and Health-KINDNESS officially launched their Community Library, which has good books and more than 750 publications. The books in the library of the good that is capital formation contributed to the following: HakiElimu (books, publications and more than 150), coordinator and advisor of the group Mr. Mussa PM Kamtande (books and has contributed over 450 publications), as well as institutions, Mtwara Teachers College (K), and Mtwara Teachers College (U), which together have contributed almost 150 publications. In the picture below looks good Group Chairman Mr. Fidelis Milanzi with special guest Mr. Richard Lucas watched the books in the library. |
Translation History
|