Base (Swahili) | English |
---|---|
UCHUNGUZI ZAIDI WA MAENEO YALIYOATHIRIKA NA MAFURIKO UNAHITAJIKA. Baada ya mafuriko yaliyotokea tarehe 20/12/2011 kuacha familia zaidi ya 1800 zikiwa hazina makazi,upotevu wa mali na vifo vya watu zaidi ya 41,imebainika kuwa kuna haja ya kufanya uchunguzi akinifu ili kubaini madhara zaidi yaliyopatikana kutokana na ukweli kuwa kuna watu na nyumba zaidi ziliharibika lakini hazikubainika. Uchunguzi uliofanywa na jeanmedia umebaini kuwa maeneo mengi yaliathirika na mafuriko hayo hayakuweza kubainishwa katika zoezi la kubaini maeneo yaliyoathirika,hali ambayo imepelekea malalamiko kwa viongozi wa ngazi za chini hususani wenyeviti wa mitaa,watendaji na madiwani,kwa kutokufuatilia nyumba zilizo pata madhara kutokana na mafuriko hayo. Wakazi hao kutoka maeneo mbalimbali ya jiji la Dar es salaam wamesema kuwa nyumba zao pamoja na mali zao zilisombwa na maji lakini cha ajabu huduma ikatolewa kwa baadhi ya wananchi.Wameeleza kuwa mpaka sasa hakuna kiongozi yeyote wa serikali aliyejaribu kwenda kuwapa hata pole ya maneno hali ambayo inaonesha kutokujaliwa wanapopata matatizo,isipokuwa wakati wa uchaguzi tu ndio wanaonekana wana wajali. Wananchi hao wa maeneo ya kimara kilungule,ubungo rombo,gide, kibangu na msewe wamezidi kueleza kuwa karibu maeneo yote yaliyopitiwa na mifereji ya maji yalipata madhara ya kubomokewa kwa nyumba na kupotea kwa vyombo vya ndani.Kutokana na hali hiyo,wameiomba serikali kufanya tathimini upya ili kubaini maeneo ambayo yamepata madhara ili kupunguza usumbufu unaoweza kujitokeza siku za mbeleni. Ni vema tukaamini kuwa lisemwalo lipo na kama halipo basi laja,hivyo basi kabla madhara zaidi hayajatokea inabidi hatua za makusudi zichukuliwe kuhakikisha kuwa makazi ya watu na mali zao zinakuwa salama.Elimu ya utunzaji wa mazingira inabidi ipewe kipaumbele,hususani katika maeneo ambayo yanakaliwa na wakazi waliokaribu na mifereji ya kupitisha maji ili kuepuka utupaji wa taka ovyo katika mifereji hiyo hali ambayo hupelekea izibe na kuleta harufu mbaya na mlipuko wa magonjwa kama kipindupindu,kuhara na ugonjwa wa matumbo.Tuendelee kupeana hekima za kiafrika kwa kusema tunza mazingira ili yakutunze.
ANTON MWITA KITERERI
|
Further investigation of flood-affected areas is needed. After the floods occurred on 12.20.2011 leaving more than 1,800 families have no homes being, loss of property and deaths of people over 41, it is noted that there is a need to make an inquiry was faithful to identify more harm attained due to the fact that there are people with more houses were invalid but not zikubainika. Tests conducted by jeanmedia revealed that many areas were strained by the floods could not identified in the process of identifying the affected areas, which led a complaint with the leaders of the grassroots levels, especially chairmen of local government, officials and councilors, to kutokufuatilia house containing a hazardous due to floods . Local residents from different areas of the city of Dar es Salaam have said that their houses with their own zilisombwa and water but the wonderful services has been introduced by some people nchi.Wameeleza that till now no any leader of government who tried to give even the pole of words which shows kutokujaliwa they get problems, except when the only choices seem to have cared. Citizens of these areas Kimara kilungule, Ubungo Rombo, gide, Bangu and have continued to express a child's rattle almost all areas and revised drainage impact kubomokewa received by the house and loss of vessels ndani.Kutokana the situation, requested the government to re-evaluate to identify areas that have found effects to reduce the discomfort that can occur days later. It is good and we believe that lisemwalo exists and if it exists then laja, so before more harm it happens we have to deliberate steps should be taken to ensure that homeless people and their belongings are kept salama.Elimu of environmental protection should be given priority, especially in areas where yanakaliwa and residents were close to passing water drainage to avoid dumping of waste disposal in the canals which leads izibe to bring the smell and the outbreak of diseases like cholera, diarrhea and sickness African matumbo.Tuendelee give wisdom to say to keep the environment yakutunze. ANTON METERS KITERERI |
Translation History
|