Envaya

/UVIKITWE/post/97782: Kinyarwanda: WI0001550FF3D19000097782:content

Base (Igiswayire) Kinyarwanda

UVIKITWE GROUP, kupitia ufadhili wa The Foundation For Civil Society, imefanikiwa kutekeleza mradi  wa uelimishajirika kwa vijana kuhusu athari za matumizi ya dawa za kulevya na uhusiano wake na maambukizi ya VVU/UKIMWI. Mradi huu umetekalezwa katika wilaya ya Bagamoyo  ndani ya kata sita ambazo ni Vigwaza,Chalinze,Ubena,Msata,Miono na Kiwangwa. Mradi huu umeweza kuwafikia vijana tisini (90) wanaotumia na wasiotumia dawa za kulevya.

Mafanikio ya mradi

  • Kuanzishwa na kusajiliwa kwa CBOs  kumi (10) zinazo toa elimu hii kwa jamii.
  • Vijana wapatao  12  waliokuwa wanatumia dawa za kulevya , wameweza kujitambua na kuachamatumizi ya dawa za kulevya
  • Vijana wanne  4 wameweza kuteuliwa na kuingia kwenye kamati za ukimwi za kata na kuwakilsha kwenye kamati za WODC ngazi ya kata

Changamoto tulizokutana nazo.

  • Mahitaji  ya jamii husika kuwa juu kuliko uwezo wa taasisi
  • Uhitaji wa elimu ya stadi za maisha kwa jamii yote, kama nyenzo ya kuleta mabadiliko ya tabia.
  • Wilaya ya Bagamoyo kuwa njia kuu ya kuingiza dawa za kulevya kutoka  Zanzibara, ambako ndiyo njia kuu ya kuingizia dawa za kulevya kutoka nchi za nje.B

 

 

 

 

 

 

Picha za baadhi ya vijana wa kata za mradi waliohudhuria mafunzo ya elimurika kuhusu athari za matumizi ya dawa za kulevya  na uhusiano wake na maambukizi ya VVU/UKIMWI.

(Not translated)

Kugirango ugire icyo uhindura kubyo wasemuye, ugomba kwinjira mu rubuga Injira · Iyandikishe