Base (Swahili) | English |
---|---|
Kikundi hiki kimeundwa na wanawake walio athirika na Virusi vya ukimwi. Baada ya kugundua hali zetu mbaya za kiafya mwaka 2006 ndipo tulipo amua kuanzisha kikundi hiki. Mwezi February tarehe 9 mwaka jana ndipo tulipo pata usajili wa kuwa NGO rasmi. Kwakuwa kikundi chetu kilikuwa ni kichanga, hatukujua namna sahihi ya kupata ruzuku. Hivyo tukakubaliana na shikrika linalo fanya kazi na wa athirika TANOFA kuwa tuchangie kiasi cha shilingi laki tano alafu baada ya mwezi watupe mkopo wa milioni mbili tufanyie kazi alafu marejesho yataanza baada ya miezi miwili toka mkopo utakapotolewa. Lakini mkopo haukutolewa na fedha tulizowapa hazijarejeshwa mpaka sasa. Kwa sasa tatizo letu kubwa ni kwamba tumeshindwa kulipa kodi ya pango, kwahiyo ofisi zetu tumezihamishia katika nyumba ya mwenye kiti wa shirika letu Bi DORA MWALUKO. Tunajihusisha na miradi tofauti ili kupata kujiwezesha. Habari zaidi naomba usome kipengele cha miradi. |
This group is made up of women who are infected with HIV / AIDS. After discovering our bad health condition in 2006, we decided to start this group. February 9 last year we got registered as an official NGO. Because our group was new, we didn't know the correct way to get grants. So we agreed with an organization that does work with infected people, TANOFA, that we may give them 500,000 TSh then after a year they give us 2,000,000 TSh for doing work. But it wasn't like this because we gave money and it was not returned. For now, our big problem is that we have failed to pay rent, so we have moved our offices in the house of our organization's chairman, Mrs. Dora MWARUKO . We are concerning ourselves with different projects in order to enable ourselves. For more news, I ask you read the projects section. |
Translation History
|