Envaya

HALI YA UGONJWA WA UKIMWI TANZANIA.

NG'ONYE JOHN (Mkurugenzi wa Taasisi ya Kupambana na Ukimwi Kitangari.)
2 Juni, 2011 11:27 EAT

Ugonjwa wa UKIMWI bado ni tatizo katika nchi yetu ya Tanzania,lakini baadhi ya wananchi wengine wanaonesha kuridhika kuwepo kwa Ugonjwa huu eti kwasababu ya kupatikana kwa tiba ya miti shamba kama ambavyo babu Mchungaji Ambilikile wa Loliondo anavyotibu kwa Kikombe.Kuridhika kwao hudiriki kusema sasa ugonjwa huu umepata dawa ya kutibu.Ninachopenda kueleza kwa wenzangu ni kwamba tusiache kuchukua tahadhari kwa kisingizio kwamba Dawa imepatikana.Ushauri. Kwa waratibu wote wa UKIMWI wa wilaya Tanzania, Je,Mnaonaje kama kila mwezi kutoa taarifa ya hali ya maambukizi mapya na hali ya Ukimwi na kuweka kwenye mbao za matangazo ili watu waone hali ilivyo kuhusu Ugonjwa huu wa UKIMWI?

victory Agency Tz Trust (TEMEKE)
8 Juni, 2011 12:08 EAT (ilihaririwa 26 Machi, 2012 08:06 EAT)

Ugonjwa huu bado ni tishio  katika nchi yetu ya Tanzania,tunachotakiwa kufanya ni kuendelea kuhamasisha jamii kujikinga na ugonjwa huu.

DR PETER KIBACHA (DAR ES SALAAM)
8 Juni, 2011 12:10 EAT (ilihaririwa 26 Machi, 2012 08:06 EAT)

@NG'ONYE JOHN (Mkurugenzi wa Taasisi ya Kupambana na Ukimwi Kitangari.): 

Vizuri sana John;Nafikiri watu wanahamu kubwa ya kupata dawa ya ugonjwa huu;hasa wale ambao wameshaathirika ndio maana watu wengine (siyo babu wa loliondo) wanatumia njia ya kujipati  fedha wakijua kwamba dawa haitibu lakini watu watanunua na pesa itapatikana kwa biashara hiyo.)angalia jinsi vikombe vilivyoongezeka   hivi karibuni),mara cha bibi,mara cha nani;siwalaumu hii yote ni kwa sababu ya umasikini wa muda mrefu na bado  wana hamu ya kufikia malengo yao au maisha bora.

Hivyo ni vizuri tufanye utafiti  kwanza kabla ya kukubaliana na jambo nyeti kama hili la dawa ya ukimwi.

Kwa ujumla kwa maoni yangu maabukizi yamepungua hasa kutokana na watu kuhamasika kutumia kinga lakini kutoa taarifa kila mwezi inakuwa ngumu kwani watanzania wa sasa tumepoteza uzalendo kila mtu awe mtumishi wa uma au la anataka ajipatie kipato kwa lolote anlofanyo hajali wananchi wenzake.

Nashauri watu wenyewe pamoja na taarifa wajithamimi na kujilinda dhidi ya ugonjwa juu

emma wa ngusero (arusha)
18 Mei, 2012 14:22 EAT

Hii ni Kitangali ya Mtwara Newala au Kitangali nyingine?

saidi john (via email)
23 Mei, 2012 09:34 EAT
Asante kwa swali lako, Hii ni Kitangari ya Mtwara iliyopo wilaya ya Newala. Hakuna nyingine.Usifananishe na Kitangiri.

Ongeza Ujumbe Mpya (Ficha)

Jina lako:
Mahali ulipo:
Email yako:
(sio lazima)
Anwani yako ya email haitachapishwa.