Injira
SAIDIA WAZEE TANZANIA

SAIDIA WAZEE TANZANIA

Tanzania

Uru rupapuro ruragaragazwa mu rurimi rw'umwimerere Igiswayire. Edit translations

MIRADI KWA WAZEE

SAIDIA WAZEE TANZANIA (SAWATA MARA)
28 Kamena, 2012 at 09:57 EAT

Ukiwa mzee, watu huamini kuwa huwezi tena kufanya kazi yoyote. Tofasiri rahisi ya uzee, “ni kupungukiwa uwezo wa kufanya kazi”. Je, ni kweli kuwa wazee wenye Afya njema (hasa wa umri wa miaka 60 hadi 75), hawawezi kufanya kazi hata ile ya kusimamia kazi ndogo ndogo? Toa maoni yako!

fikiri mvugaro kutoka mwela theatre group (Temeke DSM)
12 Nyakanga, 2012 at 09:56 EAT

Hasante sana kwa mada yako na kutoa fursa katika kuchangia mada hii ya Wazee ni kweli unavyosema sisi vijana wa sasa ni tofauti kabisa na vijana wazamani ambao sasa ni wazee kumekuwa na vitendo vya unyanyasaji,ubaguzi kwa wazee utafikiri hawa wazee hakuwa vijana au sisi  vijana hatutazeeka .

mimi japo ni kijana lakini nimepata mchango mkubwa sana kwa wazee mpaka nimefika hapa nilipo, ninasema wazee wanamchango mkubwa na wanafanya kazi kubwa kwa sababu wazee wanamaono ambao kama ingekuwa ni kulipia basi ungelipia kwa pesa nyingi sana na hata kama ungekuwa na hizo pesa wenda ungekosa maono hayo

ukiangalia vijana wengi kutokana kuadaiwa na ujana wanajikuta wanakuwa na watoto ambao mzigo huo wa watoto uwapelekea wazee .

si hivyo kijana anapopata matatizo hasa ya magonjwa makubwa na kutengwa na ndugu na malafiki ukimbilia kujiuguza kwa wazee ila wazee hawa mchango wao haujilikana ndani ya jamii na malipo yao uishia katika kusimagwa na kutengwa

wazee katika kulitumikia taifa ndio walikuwa kipaumbe katika kufanya matambiko ya kijadi lakini pia tunawategemea katika kujua historia ya miji,vijiji na mambo mbalimbali bila ya gharama yoyote

mwisho napenda kuishia kwa kusema wazee si kwamba wanaweza kufanya kazi ndogogo la wanafanya kazi kubwa sana kiasi kwamba hatuna mshahara wa kuwalipa   


Andika ubutumwa

Tumira abandi mu kiganiro