Log in
MASASI YOUTH DEVELOPMENT GROUPS NETWORK

MASASI YOUTH DEVELOPMENT GROUPS NETWORK

Masasi, Tanzania

Parts of this page are in Swahili. Edit translations
UTAMBULISHO MASAYODENni shikalisilo la kiserikali na lipo wilaya ya Masasi mkoa wa Mtwara.Shirika lilianzishwa rasmi tarehe 18/5/2002 liliundwa na vikundi 34 vya vijana toka kila kata za wilaya ya Masasi. Masayoden ilisajiliwa tarehe 13/6/2003. namba ya usajili ni S .O.NO 11980 .Shirika linafanya shughuli za vijana ngazi ya wilaya. Lengo kuu ni kupambana na umasikini na vvu/ukimwi wilaya ya masasi. MASAYODEN ni mwanachama wa shirika Mwamvuli la NGOs Masasi (MANGONET). Masayoden inamahusiano mazuri na vijana, watoto jamii wa jinsia zote. Vilevile serikali Halmashauri ya wilaya ya Masasi na mashirika mengine ya ndani na nje ya wilaya ya masasi. Masayoden imewahi kufanya kazi na UNICEF, 2002-2006 UNDP 2005 CONCERN 2006-2007. MUHTASARI Masasi ni Wilaya yenye eneo la mraba KM.4429.9 Wilaya hii ni karibu asilimia 23% ya eneo la Mkoa wa Mtwara ina tarafa 5 kata 34 vijiji 156 na vitongoji 905. Kutokana na sensa ya 2002 ina wakazi 304211. ikiwa na KE 159142 na ME148069. Inakadiriwa kuwa na kiwango cha 2.1% ya ukuaji wa uzazi. TATIZO Kuongezeka kwa kikwazo vinavyo kwamisha upatikanaji wa mitaji ya kuanzisha na kuendesha Biashara hasa zile ndogo na za vijijini wilaya ya Masasi. UHAKIKA WA TATIZO Wilaya ya Masasi ni kati ya Wilaya zenye idadi kubwa sana ya vijana wasiokuwa na shughuli maalumu na vijana wanayoishi katika mazingira magumu. Kuongezeka kwa tatizo la vikwazo vinavyokwamisha upatikanaji wa mitaji ya kuanzisha na kuendesha Biashara .Imeleta athari kwa vijana kama zifuatazo: (i) kupungua kwa ustawi wa vijana (ii) Kuongezeka kwa vijana wanayoishi mitaani na vijiweni (iii) Kuongezeka kwa uvutaji bangi na unywaji wa pombe (iv) Kuongezeka kwa maambukizi ya VVU/UKIMWI kwa vijana (v) Kuongezeka kwa watoto yatima na wanayoishi katika mazingira magumu (vi) Kuongezeka kwa utegemezi katika familia LENGO KUU: Kutokana na malengo ya kitaifa 2025 na mpango wa kitaifa wa mkakati wa kukuza uchumi na kuondoa umasikini Tanzania (MKUKUTA) wenye vipengere vitatu (3) . Shirika la Masayoden likishirikisha na chama cha kuweka na kukopa Masasi vijana SACCOS kuchangia katika kipengele cha kwanza (i) cha kukuza uchumi na kuondoa umasikini wa kipato kwa watanzania. LENGO LA MAHUSUSI Kupunguza vikwazo vinavyokwamisha upatikanaji wa mitaji ya kuanzisha na kuendesha Biashara hasa zile ndogo na za vijijini kwa vijana wilaya ya Masasi ifikapo Dec 2015. WALENGWA VIJANA MIKAKATI Kutoa mafunzo ya ujasiliamali Kuendesha majukwaa ya vijana Kuboresha ofisi ya Masayoden/Masasi Vijana Saccos MATOKEO Kuongezeka kwa uelewa juu ya mbinu, ubunifu uboreshaji wa bidhaa na ufuatiliaji wa masoko Kuongezeka kwa kipato kwa vijana Kupungua kwa vijana wanaoishi mitaani na vijiweni SHUGHULI Kuendesha mafunzo ya elimu ya ujasilamali kwa vijana Kuendesha majukwaa ya vijana kila kata Kuboresha ofisi ya Masayoden na Masasi Vijana Saccos MAFANIKIO Kuongezeka kwa ajira katika sekta binafsi Kuongezeka kwa mapato katika serikali za mitaa kwa kukusanya kodi kutokana ongezeko la uzalishaji mali. Kuongezeka kwa ustawi wa vijana Vijana wengi kujishughulisha katika shughuli mbalimbali za kiuchumi na maendeleo MUDA WA UTEKELEZAJI JULLAY…..........SEPTEMBER 2011 ENEO LA UTEKELEZAJI WILAYANI NA KWENYE KATA NJIA ZIKAZOTUMIKA Majadiliano Kazi za vikundi WALENGWA WENGINE Serikali Jamii CBOS MAHITAJI Vijana Wataalamu Fedha
May 26, 2011
« Previous

Comments (5)

Salumu said:
madhumuni ya masayoden
kuimarisha mfumo wa mawasiliano ya vijana kwa kuhusu ukimwi
kuwa mtetezi wa vikndi vya vijana masasi ili vipate kuwakilishwa katika nyanja zote na hoja zote za maendeleo
kuratibu ushirikiano na taasisi mbalimbali za ndani na nje ya nchi
kulinda na kudumisha utamaduni wa watu wa masasi kwa faida ya vizazi vijavyo
kuhifadhi kumbukumbu mbalimbali za shughuli za utamaduni zinazofanywa na vikundi wanachama.
kubuni miundombinu ya kiuchumi kwa maendeleo ya viajana
kuwa shirika mama au shirika mwamvuli la vikundi vya vijana katika wilaya ya masasi na kurtibu mambo ambayo yanavihusu vikundi hivyo kiwilaya.
June 2, 2011 (edited October 5, 2011)
Salumu (katibu) said:
DIRA YA MASAYODEN
Umaskini katika wilaya ya masasi unapigwa vita na unatoweka
KAULI MBIU YA MASAYODEN
Ajira kwa vijana, ambapo vijana katika wilaya ya masasi wanahamasishwa kuanzisha vikundi vya uzalishaji mali ambavyo vitaanzisha na kuendeleza miradi ya kiuchumi sambasamba na kuupiga vita ukimwi
June 2, 2011 (edited October 5, 2011)
Salumu (katibu) said:
tunaomba mashirika mengine tuwasiliane kupitia anwani yetu ya envaya
June 2, 2011
mwandae mchungulike (liwale-lindi) said:
ongera sana masayoden mimefurahishwa na hii tasisi na Mimi nimefurahishwa na Leo 11/8/2015 nimetembelea na kubadilisha mawazo na Katibu mtendaji bwana Salumu nipo tayari kushirikiana nanyi katika kusambaza habari mtandaoni kwangu www.liwaleyetu.blogspot.com
August 11, 2015 (edited August 11, 2015)
azizi ahmadi (masasi) said:
KAZI NJEMA
November 6, 2015

Add a comment

Your name:
Your location:
Your email:
(optional)
Your email address will not be published.