BRECKINGNEWS>BAADA YA HALI YA HEWA KUCHAFUKA TUNDUMA, OMARY NUNDU ATOKEA MCHANA HUU
Taarifa zilizoufikia mtandao wa Indaba zinasema, waziri wa uchukuzi Omary Nundu atazungumza mchana huu na madereva wa magari yanayosafiri kati ya Tanzania na nchi zingine kupeleka na kuleta mzigo maarufu kama Transit.
Mkutano huo ni matokeo ya kugomewa kwa jitiohada zote zilizofanywa na viongozi wa mkoa wa Mbeya ambapo mkuu wa mkoa wa Mbeya John Mwakipesile jana alimtuma mkuu wa wilaya kupeleka ujumbe wa kuwataka wasitishe mgomo huo wakati mambo yao yakishughulikiwa, lakini wakati mkuu huyo wa wilaya akisoma barua hiyo alipofikia mwisho akataja imesainiwa na Mkuu wa mkoa wa Mbeya John MWAKIPESILE ghafla wakalipuka kuzoea,
Awali walikuwa wakipiga makofi kwa kila kipengere kilichosomwa, lakini ilipofika hatua ya kusoma aliyeandika waraka huo basi hali ikawa siyo, jambo linaloashiria kuwa walihisi hizo zilikuwa ni porojo za kuwatuliza na si ujumbe kutoka kwenye mamlaka za juu kama walivyotaka.\
Omary Nundu amelazimika kufika leo hii baada ya gari moja lililokuwa likiendeshwa na mtanzania mwenye asili ya somalia kuzuiwa na madereva wenzake likiwa barabarani na kisha wakachomoa funguo na kutokomea nazo, hivyo kuzuia shughuli za barabra kuu ya Tunduma -Mbeya.
Imeelezwa kuwa gari hilo linatumia passwords ama mzingo katika kuliwasha ambapo pia ni lazima funguo iwe halisi ambapo vibonyezeo vyote vipo kwenye funguo hali ambayo ililazimu polisi kuwa wapole kwani walishaanza kubutua mabomu.
Kilicjhotufikisha hapo ni matokeo ya serikali kuchukulia juu juu mgogoro huo ambapo ilionyesha kuto kuupa uzito unaostahili katika kushughulikia zmalalamiko waliyoyatoa madereva yakihusisha haki zao pamoja na baadhi ya kero ambazo tayari zimeanza kupatiwa ufumbuzi.
Madereva hao walianzisha changamoto hiyo tangu July 17 baada ya kuandika barua kwenda kwa waziri mkuu lakini ikakosa majibu kwa kipindi chote hatua ambayo wakaamua kuchukua maamuzi lakini wakionyana wenyewe kutokujihusisha na uharibifu wa mali.
Hata hivyo taarifa zilizozagaa jana zilianza kuonyesha hofu kubwa baada ya kudaiwa baadhi ya madereva hao wametegesha petroli kulipua magari ikiwa polisi wangetumia mabomu ama kuanzisha operesheni ya FFU, hatua hiyo iling,amuliwa na idara za Inteligensia ambapo magari ya zima moto yaliandaliwa jana kukabili hali hiyo wakati magari ya washa washa yalipokuwa yakizunguka na kutoa tahadahari jana jioni.
Mtaendelea kuelezwa kinachoendelea kupitia blog hii
CHUO CHA MIPANGO DODOMA KUWA NA JENGO REEFU KULIKO YOTE MKOANI DODOMA
![]() |
| Ukumbi wa Mwalimu Nyerere uliopo Chuo cha Mipango Dodoma kama nilivyouona nikiwa kwenye mazingira hayo jana |
![]() |
| Nani kakwambia darasa linaangalia utu uzima, hapa naelekezwa namna ya kuboresha logical frame work! ama kwa kiswahili mnaita Bao Mantiki |
![]() |
| Hapa wazee wangu hawa wa Chuo cha Mipango wakisukuma draft kwa burudani zao wakati wa mapumziko getini, raha kweli! |
HII NI DODOMA, MAKAO MAKUU YA TANZANIA
![]() |
| Hapa ni Anglican cathedral |
![]() |
| Msikiti Mkubwa uliopo Dodoma karibu na eneo la Chako ni chako, nimeukubali mandhari zake hasa masaa ya jioni |
![]() |
| Ndege ikitua katika uwanja wa ndege wa Dodoma kama nilivyoinasa nikiwa katika harakati za kuelekea chuo cha mipango |
![]() |
| Mnara uliopo karibu na ofisi za TAMISEMI wenyewe tunaita round about |
HAYA AKINA MAMA BIDHAA MPYA MNATANGAZIWA
WADAU VIATUZIII HAOOO WAMESHUSHAAA MAMBO NI YALE YALE YA FUNGA KAZI ZA VIATUUUUZIII unyayooooo AMBAPO SASA MABIHARUSIII NA MASHORIII WOOTE WANAOTHAMINI MIGUU YAO...KUTINGA KIATU CHA VIATUZI NI SAWA NA KUUKATIA INSURANCE MGUU WAKO KWANIIII NI VYA UKWE'E hudhuriki MBALI NA VIATU KUNA CLUTCHZ ZILE STYLE MPYA (ENVELOPE CLUTCH) NA BILA KUSAHAU VITUPIOOOOO (ACCESORIEZ)
KUONA ZAIDI MAMBO ZAIDI DUMBUKIA BLOGUNI
WANAPATIKANA:: SEA VIEW PLOT NO.10
MAWASILIANO:: 0715 850855
MABLOCKING COLOR KIBAO....KAJIBLOKUENIHIZI HAPA NDO ENVELOPE CLUTCH....umeona ee kitu cha bahasha hapo kati
IGP MWEMA AZINDUZ UVAAJI HELMETI NA KAMPENI YA KUSALIMISHA SILAHA
Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, IGP, Said Mwema (katikati) akivishwa helmeti baada ya Taasisi ya Helmet Vaccin Initiative Tanzania, kukabidhi msaada wa helmeti 500 kwa jeshi hilo, wakati wa hafla ya uzinduzi wa uhamasishaji jamii kuvaa kofia hizo wakipanda pikipiki, Dar es Salaam leo katika Makao Makuu ya Jeshi la Polisi. (PICHA NA RICHARD MWAIKENDA)
IGP Mwema akikata utepe kuashiria uzinduzi huo
Mkuu wa kitengo cha Polisi cha Maboresho, Lucas Kusima akielezea kuhusu maboresho mbalimbali yaliyofanywa na jeshi hilo
Mkuu wa Oparesheni wa Jeshi la Polisi, Kamishna Paul Chagonja akifafanua mbamo mbalimbali hasa kuhusu oparesheni iliyotangazwa leo na IGP, Mwema ya kusalimisha silaha zinazomilikiwa isivyo halali
Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, IGP, Said Mwema (katikati) akiangalia wakati Balozi wa Hiari wa Uvaaji wa Kofia nchini, Ritta Poulsen (kulia kwake) baada ya Taasisi ya Helmet Vaccin Initiative Tanzania, ilipokabidhi msaada wa helmeti 500 kwa jeshi hilo, wakati wa hafla ya uzinduzi wa uhamasishaji jamii kuvaa kofia hizo wakipanda pikipiki Dar es Salaam leo. (PICHA NA RICHARD MWAIKENDA)
Mkuu wa kitengo cha upelelezi wa makosa mtandao, Kasala, akielezea jinsi wanavyopambana na uhalifu huo
Sehemu ya waandishi wa habari na baadhi ya maofisa wa jeshi la polisi wakisikiliza
IGP Mwema akimkabidhi mtangazaji wa EAST AFRICA RADIO, David gumbo kitabu kinachoelezea sheria za umiliki wa silaha mbalimbali nchini
IGP Mwema akijibu maswali mbalimbali wakati wa uzinduzi wa kuanza kuhakiki silaha nchini, uvaaji helmeti na uhamasishaji jamii kutii sheria bila kusurutishwa
Kamishna wa Polisi, Clodwin Mtweve akisisitiza jambo katika mkutano huoELIAKIM CHACHA MASWI ACHUKUA NAFASI YA JAIRO, WADAU WA TAMISEMI WAMLILIA
![]() |
| BW. ELIAKIM CHACHA MASWI |
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI Kufuatia Katibu Mkuu wa Nishati na Madini, Bwana David K. Jairo, kupewa likizo kwa muda, Katibu Mkuu Kiongozi, Bwana Phillemon L. Luhanjo, amemteua Bwana ELIAKIM CHACHA MASWI, kuwa KAIMU KATIBU MKUU, Wizara ya Nishati na Madini kuanzia leo tarehe 22 Julai, 2011. Bwana MASWI, kwa sasa ni Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa.Imetolewa na Premi Kibanga,Mwandishi wa Habari wa Rais Msaidizi,Ikulu.Dar es salaam.22 Julai, 2011
Katika mazungumzo ya hapa na pale kuzungumzia mabadiliko hayo wadau wengi wa TAMISEMI wameonekana kumlilia bwana Maswi kutokana na misimamo yake na utendaji wake ambao uliwezesha halmashauri za wilaya kuchakarika hapa na pale kuhakikisha kuwa zinajiimarika kwa kutenda vyema katika huduma zake kwa wananchi.
wanaeleza kuwa jamaa alikuwa mkali pale anapobaini uzembe na pia hakuwa na lugha za kuficha ficha kwenye makosa na alikuwa akiwafikishia ujumbe moja kwa moja wahusika pasipo kusikiliza majungu hatua ambayo wapiga majungu walikuwa wakiongopa kupiga hodi TAMISEMI kwenda kuchonga umbeya usio na uthibitisho. Kila lakheri Maswi katika ofisi mpya tunakuombea kila lililozuri! Mungu atakuangazia majukumu yao na uongozi wako utukuke!
MAANDALIZI YA SIKU YA MASHUJAA MBEYA YAENDELEA KUPAMBA MOTO
| Askari wa JWTZ wa kikosi cha 44 KJ wakiwa mazoezini kwenye mnara wa kumbukumbu ya mashujaa jijini Mbeya |
| Bendi ya jeshi la Magereza wakiongoza gwaride |
| Ukumbusho wa askari waliokufa vitani 1939 1945 |
| Wanajeshi wakiendelea na mazoezi |
| Mnara huu wa majina ya Mashujaa waliokufa vitani upo katikati ya jiji la mbeya sijui kama nao wataukumbuka kuufanyia usafi maana umezungukwa na nyasi KUTOKA BLOG YA MBEYA YETU |



































































