Chama cha Skauti Zanzibar leo tarehe 17/3/2018 kimemuapisha Skauti mkuu wa chama cha skauti Zanzibar katika ukumbi wa Kilimanjaro Super star Nursery uliopo Mwanakwereke Mjini Zanzibar
Mlezi wa Chama Cha Skati Zanzibar Mheshimiwa Balozi Ali Karume ambae pia ni Waziri Wa Vijana Utamaduni Sanaa na Michezo, akisaini hati ya skauti Mkuu Mheshimiwa Makame Mshimba Mbarouk katika hafla iliyofanyika katika ukumbi wa kilimanjaro Super Star Zanzibar
Nae mlezi wa Chama hutubia Maskauti waliohudhuria katika Mkutano huo
Skauti Mkuu Akimuapisha Kamishna Mkuu wa Chama Cha Skauti Zanzibar
Kamishna Mkuu wa Chama Cha Skauti Zanzibar akiapishwa na skauti Mkuu
Chama cha Skauti Ulimwenguni kilianzishwa na Muengereza aitwae Sir Baden Powell (BP) tangu mwaka 1907 huko Uingereza katika kisiwa cha Brown Sea,
Uskauti uliingia Zanzibar mwaka 1912 miaka 5 tu baada ya kuanzishwa na Sir Baden Powell.
Chama cha Skauti Zanzibar kilianzishwa Mwaka 1912 kabla ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar, baada ya Mapinduzi ya Zanzibar 1964 Mheshimiwa Rais wa kwanza hayati Abeid Amani Karume akaisitisha kuendelea kufanya kazi na kuona kwamba ni sehemu ya ukoloni kwani uskauti huo umeletwa na Waingereza.
Hata hivyo mwaka 1992 Mheshimiwa Rais wa Awamu ya tano Dr Salmin Amour Juma alipokwenda Magila Mkoani Tanga katika jamboree na kuwaona vijana wa Skauti, Mheshimiwa Rais alikuwa na shauku ikiambatana na furaha baada ya kuwaona vijana wa skauti katika mkoa huo, Ndipo akaamua Uskauti huo uwepo na visiwani Zanzibar ili vijana nao waweze kujifunza ubunifu, uzalendo na ukakamavu.
Kutokana na kauli hio ndio kwa mara ya pili uskauti ukafufuliwa na kuundwa kamati maalum ya kufufua Uskauti Zanzibar, chini ya wizara ya vijana katika Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa wakati huo,
Sura ya kwanza ya uskauti ndipo ilipoanza kuonekena baada ya kuanzishwa kundi la majaribio katika skuli ya Msingi Mwembeladu, hadi kufikia mwaka 2000 Zanzibar kulikua na makundi 15 na Wanachama 150, hadi sasa mwaka 2017 kuna makundi 36 na Wanachama 300 Unguja na Pemba.
Vijana wengi hapa Zanzibar wameshindwa kuwa wazalendo wa taifa lao na kukosa kujiamini pindi wanapoamua kufanya maamuzi sahihi yanayohusu maisha yao, nakujikuta wanaingia katika vikundi viovu,
Kwakua jamii kubwa ya Wazanzibar haina ufahamu na elimu ya kutosha kuhusu SKAUTI , hivyo tumeona ipo haja ya Kuunganisha Makundi yote ya Skauti na kuueneza uskauti katika maeneo mengine ya Zanzibar na kua na usimamizi mzuri wa skauti ili kuweza kuisaidia jamii iliyotuzunguka.
Kupitia kuanzishwa kwa Uskauti imefanya vijana kuwa wakakamavu, weledi na wazalendo katika taifa lao katika kubuni mbinu mbali mbali za kuondoa changamoto miongoni mwao na wananchi kwa ujumla,
Chama cha Skauti Zanzibar ni chama hiari, na wala hakifungamani na vyama vya siasa nchini wala hakina chembe ya ubaguzi wa rangi dini wala jinsia, pia huchangia elimu na Malezi kwa vijana kwa kupitia njia ya ‘Uskauti’ ambapo humjenga kijana kimwili, kiakili, kimtazamo, kijamii, kiimani ili waweze kujitegemea na kuwajibika na kumfanya kijana kujifunza mengi kwa vitendo kama Kusaidia jamii katika Majanga, kutoa huduma za jamii katika siku kuu za kitaifa, Uokozi, na kusaidia jamii katika ujenzi wa Taifa letu
Chama cha Skauti Zanzibar leo tarehe 17/3/2018 kimemuapisha Skauti mkuu wa chama cha skauti Zanzibar katika ukumbi wa Kilimanjaro Super star Nursery uliopo Mwanakwereke Mjini Zanzibar
Mlezi wa Chama Cha Skati Zanzibar Mheshimiwa Balozi Ali Karume ambae pia ni Waziri Wa Vijana Utamaduni Sanaa na Michezo, akisaini hati ya skauti Mkuu Mheshimiwa Makame Mshimba Mbarouk katika hafla iliyofanyika katika ukumbi wa kilimanjaro Super Star Zanzibar
Nae mlezi wa Chama hutubia Maskauti waliohudhuria katika Mkutano huo
Skauti Mkuu Akimuapisha Kamishna Mkuu wa Chama Cha Skauti Zanzibar
Kamishna Mkuu wa Chama Cha Skauti Zanzibar akiapishwa na skauti Mkuu
kamishna mkuu akiapishwa
Wanachama Wa Chama Cha Skauti
Meneja wa NMB akiwapa somo baadhi ya Maskauti#
habari ndugu maskauti na wapenzi wa blog hii salam na pongezi kwa Uongozi wa CHUCHU FM kutusapoti katika kuendesha harakati za Skauti hapa ZANZIBAR kwa kurusha kipindi Maaalum katika kituo chenu cha Redio AHSANTE
UONGOZI WA CHUCHU FM
MULHAT DORCE KWA USHIRIKIANO WENU MZURI MULIOTUPA KATIKA SIKU HII YA LEO YA 22/2/2014 SIKU YA MUNZILISHI WA SKAUTI DUNIANI
NISIKU AMBAYO SKAUTI WETU WALIAZIMISHA KWA KAMBI NA KUTEMBELEA MAKUMBUSHO
Chama cha skauti Zanzibar kinatoa salaam na pongezi kwa SKAUTI MKUU mteule mama MWANTUMU BAKARI MAHIZA kwa kuteuliwa kwa Skauti Mkuu Hii ni Mara ya kwanza katika Chama hicho kupata skauti mkuu wa kike Tangia kuanzishwa kwake.
Chama cha skauti Tanzania kimekuwa kikiyumba kutokana na kuna matatizo mbali mbali ambayp yanakikabili chama hicho.
Matumain yetu Uteuzi wa mama Mahiza wa weza kuwa ni dawa kwa chama hicho na kurejesha heshima na uhai wa chama hicho.
kwani chama cha Skauti Tanzania kimekuwa kikinuka kwa sifa mbaya kama wasafirishaji wa dawa za kulevya,watoto pamoja na uuzwaji wa eneo la skauti HQ
naamin wazi kwa pamoja twa weza jenga chama chetu cha skauti Tanzania kwapoja maskauti wa ZAnzibar tunasema karibu sana katika shughuli za skautI