Envaya

BAJETI YA TANZANIA NA MATUMAINI YA WANANCHI

Nashir Pontiya (Mtwara-Tanzania)
17 Juni, 2011 16:03 EAT

Hivi ni kweli uchumi wa Tanzania unaendeshwa na Vileo tu? Kwani kila bajeti utaona na kusikia Sigara na Bia juu,inakuwaje hapa?

[ujumbe umefutwa]
Hagulwa Msusu (Dar es salaam)
18 Juni, 2011 21:10 EAT (ilihaririwa 26 Machi, 2012 08:06 EAT)

Hivi ukweli upo wapi?hii posho ya wabunge,ni kweli wataacha kupokea? ni kweli itatumika kwa manufaa ya umma?nikweli mjadala huu wa posho ya wabunge utafikia ukingoni kwa muafaka na manufaa ya umma?kazi kwetu wananchi.

Nashir Pontiya (Mtwara-Tanzania)
19 Juni, 2011 09:06 EAT (ilihaririwa 26 Machi, 2012 08:06 EAT)

Kwa jinsi ninavyoona na mikwara mingi inayowekwa na Spika wa Bunge kwa wale wote wanaokataa kupokea Posho zao ni vigumu sana wabunge wetu kuacha kupokea Posho,kwani nimegundua Wabunge wengi wametolea macho sana hizo Posho,Lakini hata muda mwingine najiuliza kitu kimoja hivi hata hizi Posho wabunge wetu wakiziacha hivi ni kweli zitapelekwa kwa mafungu ya maendeleo ya Halmashauri na hata zikipelekwa huko zitafanyakazi zilizokusudiwa?

itony (Dar es salaam)
19 Juni, 2011 13:47 EAT (ilihaririwa 26 Machi, 2012 08:06 EAT)

kwa kweli hili ni tatizo kubwa sana. Hizi posho sio kwamba jamaa hawazitaki kweli ila wanajaribu kufikisha ujumbe kwamba wanapo panga kiasi cha hizi posho, basi waangalie na kiasi ambacho huenda kwenye mifuko ya maendeleo. Sio mfuko wa maendeleo una bilioni moja lakini posho bilioni 900


Ongeza Ujumbe Mpya

Karibisha watu kushiriki