Hii ndio ndoto kubwa kwa kila mmoja wetu anayetaka kuwa na mafanikio. Na usianze kujiuliza maswali ya watu walioshindwa maisha. kwa mfano wao hujiuliza maswali kama 1.ningwekeza lakini sina fedha za kutosha.
2. wakuwekeza niwe mimi mhuu haujawaona wakuwekeza ni kina Mengi n.k
3. siku nikiajiliwa nitawekeza .....
4. ukiwekeza utapata hasara .... Wewe ukitaka kuwekeza wekeza kwenye vitu ulivyo navyo kwa mfano unaweza kuwekeza kwenye Fedha, kwenye kipaji chako, kwenye ujuzi wako, kwenye muda wako n.k fanya wewe usingoje kuwa mtu wa kuangalia mambo yanatendeka na si wewe unayeyafanya yatendeke funguka.
Kila binadamu ameumbwa akiwa na uwezo wa kuwa na mafanikio, Jambo ambalo linawatofautisha watu walio fanikiwa na masikini ni uwezo wa kuamua na kuchagua, kwanini nimesema hivyo maisha yetu hakika na ule uwezo wa kuchagua na kuamua unataka kuwa na mafanikiao au la ... mfano yule aliyeamua kuwa na mafanikio na yule aliyeamua kutokuwa na mafanikio wote wako sawa kwa maamuzi yao hayo na kila mmoja atapata Heshima juu ya uamuzi wake alioamua.
Bila maono ni sawa na kukesha ukimuomba Mungu akuepushe na malaria baada ya kuchoma chandurua.
Tuwaulize kwanza mahitaji yao ,Ndipo tuwasaidie by Michael Charles. mwenyekiti wa kikundi.