Envaya
Parts of this page are in Swahili. Edit translations

Waswahili hunena "Hayawi, hayawi, sasa yamekuwa" Ni ukweli usiopingika wala kufichika kwamba hakuna njia ya mkato ili kufikia katika mafanikio kwenye jambo lolote. Nadiriki kusema hivyo kutokana na ukweli kwamba Mtandao wa Asasi za Kiraia Mkoa wa Lindi (LANGO) kama ambavyo unajulikana kwa jina maarufu umepitia katika changamoto lukuki tangu kuanzishwa kwake katikati ya mwaka 2007. Moja wapo ya changamoto kubwa ni; kuanzishwa na kujiendesha kwa kutumia raslimali fedha chache ilizokuwa inakusanya kutoka kwa wanachama wake ambao mara nyingine ililazimu kuwafuatilia na vitabu vya stakabadhi katika mikutano, warsha na matukio mengine yanayofanana na hayo ili kuwabana wawakilishi kutoka katika Mitandao ya wilaya wanachama ili angalau walipe kiasi fulani cha deni linalodaiwa mtandao wao na LANGO. Hali hiyo naamini baadhi ya wana asasi hawakufurahishwa nayo lakini kimsingi hakukuwa na jinsi wala namna ya kuufanya mtandao huu usonge mbele kama si kufanya hivyo ikizingatiwa kwamba LANGO ndio Mtandao wa Mkoa wa Lindi wenye hadhi sawa na Mitandao ya Mikoa mingine kama vile; UNGO (Morogoro), RANGO (Rukwa), ANGONET (Arusha) n.k.

Kwa niaba ya Bodi ya Usimamizi ya LANGO na mimi binafsi tunafarijika kupata mwaliko wa kuhudhuria Mafunzo ya Usimamizi wa Ruzuku (MYG) toka The Foundation for Civil Society (FCS) baada ya kuandika mara mbili tofauti kuomba ruzuku pasipo mafanikio. Kwa mantiki hiyo napenda kuwaasa wana asasi wenzangu kwamba hakuna mafanikio yanayokuja kama mvua pasipo kutumia jitihada na maarifa na kutokata tamaa. Ni vyema asasi changa na zilizoanzishwa karibuni kujifunza kutoka kwa LANGO kwani ukiomba ruzuku si lazima upate mara moja kwani kila mzunguko kuna AZAKi nyingi kutoka kona zote za nchi ambazo huomba kwa FCS. Ni vyema tujifunze kuwa wabunifu na kuwa wadadisi wa nini hasa kinachotakiwa kufanyika ambacho huwa hatukifanyi na hivyo kupelekea maandiko yetu kutopendekezwa kufadhiliwa na FCS, hakika inawezekana timiza wajibu wako!!!!

June 11, 2011
« Previous Next »

Comments (3)

Nachukua nafasi hii kuipongeza taasisi ya The Foundation for Civil Society (FCS) kwa kutuunganisha na mfumo huu wa kompyuta wa Envaya ambao umekuwa wenye manufaa makubwa kwetu wana AZAKi. Nashauri FCS iendelee kutuwezesha katika masuala mbalimbali ambayo yatatuwezsha kujengeka kiuwezo na kupelekea sekta ya AZAKi kuimarika, kuaminika na kukubalika zaidi na Jamii, Serikali na Wabia wa Maendeleo.
June 11, 2011
Wana AZAKi tujipange vilivyo katika kuhakikisha kwamba kila Mtanzania anashiriki kikamilifu katika mchakato wa mapitio na kutungwa kwa Katiba Mpya. Uzoefu unaonesha kwamba watu walio vijijini hupitwa na michakato mingi ya Kisera na Maendeleo, lakini kwa hili la Katiba tuhakikishe kwamba tunafanya kila tutakaloweza ili kuwafikia watanzania wote wakiwamo wa vijijini na makundi yaliyokatika hatari zaidi ya kuathirika na umaskini.
June 11, 2011
Haji Hamisi (UDSM) said:
katiba ni jambo zuri na la busara kwa wana AZAKI kulisimamia na kuhakikisha kila raia ndani ya mkoa wa Lindi au out of the region ikiwezekana anafahamu mapunguvu ya katiba iliyopo na ni nini hasa kinatakiwa kuwepo katika katiba mpya, na sio kupelekwa na upepo wa interest binafsi ya mtu, kikundi au chama cha siasa. nafahamu mazingira ya Lindi hasa vijijini watu hawashiriki katika uamuzi wa mambo mbalimbali yanayo wahusu, so ni changamoto kwa wana AZAKI kuhakikisha watu wanakusanyika na kuweza kuelimishwa kuhusu katiba.
July 18, 2011

Add a comment

Your name:
Your location:
Your email:
(optional)
Your email address will not be published.