Injira

/LANGO/post/24551: Kinyarwanda

BaseKinyarwanda
Nachukua nafasi hii kuipongeza taasisi ya The Foundation for Civil Society (FCS) kwa kutuunganisha na mfumo huu wa kompyuta wa Envaya ambao umekuwa wenye manufaa makubwa kwetu wana AZAKi. Nashauri FCS iendelee kutuwezesha katika masuala mbalimbali ambayo yatatuwezsha kujengeka kiuwezo na kupelekea sekta ya AZAKi kuimarika, kuaminika na kukubalika zaidi na Jamii, Serikali na Wabia wa Maendeleo.(Not translated)Hindura
Wana AZAKi tujipange vilivyo katika kuhakikisha kwamba kila Mtanzania anashiriki kikamilifu katika mchakato wa mapitio na kutungwa kwa Katiba Mpya. Uzoefu unaonesha kwamba watu walio vijijini hupitwa na michakato mingi ya Kisera na Maendeleo, lakini kwa hili la Katiba tuhakikishe kwamba tunafanya kila tutakaloweza ili kuwafikia watanzania wote wakiwamo wa vijijini na makundi yaliyokatika hatari zaidi ya kuathirika na umaskini.(Not translated)Hindura
katiba ni jambo zuri na la busara kwa wana AZAKI kulisimamia na kuhakikisha kila raia ndani ya mkoa wa Lindi au out of the region ikiwezekana anafahamu mapunguvu ya katiba iliyopo na ni nini hasa kinatakiwa kuwepo katika katiba mpya, na sio kupelekwa na upepo wa interest binafsi ya mtu, kikundi au chama cha siasa. nafahamu mazingira ya Lindi hasa vijijini watu hawashiriki katika uamuzi wa mambo mbalimbali yanayo wahusu, so ni changamoto kwa wana AZAKI kuhakikisha watu wanakusanyika na kuweza...(Not translated)Hindura
Waswahili hunena "Hayawi, hayawi, sasa yamekuwa" Ni ukweli usiopingika wala kufichika kwamba hakuna njia ya mkato ili kufikia katika mafanikio kwenye jambo lolote. Nadiriki kusema hivyo kutokana na ukweli kwamba Mtandao wa Asasi za Kiraia Mkoa wa Lindi (LANGO) kama ambavyo unajulikana kwa jina maarufu umepitia katika changamoto lukuki tangu kuanzishwa kwake katikati ya mwaka 2007. Moja wapo ya changamoto kubwa ni; kuanzishwa na kujiendesha kwa kutumia raslimali fedha chache ilizokuwa...(Not translated)Hindura