Log in

Translations: Kiswahili (sw): User Content: WI000A6DE225D52000001405:content

« Previous   ·   Next »
Base (Swahili) Kiswahili
TAARIFA YA MTANDAO WA VIJANA MANISPAA YA TEMEKE KWA KIPINDI CHA UTEKELEZAJI CHA OKT-DES 2009.

KUTOKA: MTANDAO WA MAENDELEO YA VIJANA MANISPAA YA TEMEKE (TEYODEN)
KWENDA KWA: MKURUGENZI WA HALMASHAURI MANISPAA YA TEMEKE

1.0 UTANGULIZI
Temeke Youth Development Network (TEYODEN) ni Mtandao wa Maendeleo ya Vijana unaoendeshwa na vijana wenyewe miongoni mwa mitandao 19 iliyotokana na programu ya vijana nje ya shule iliyotekelezwa na Halmashauri 19 nchini Tanzania kwa ufadhili wa UNICEF. Mtandao umesajiriwa chini ya ofisi ya Makamu wa Raisi, namba ya usajiri ni OONGO/0170.TEYODEN inasimamia na kuratibu shughuli zake katika vituo 24 vya vijana vilivyopo katika kata 24 za Manispaa ya Temeke.
1.1 Dira ya TEYODEN
Kuwa Mtandao bora wa Maendeleo ya vijana Tanzania unaowezesha vijana kuwajibika vya kutosha katika kubadili tabia hatarishi na kujiletea
katika vituo vya vijana vya kata na asasi wanachama wa TEYODEN.
1.3 Lengo kuu la TEYODEN
Kuchangia juhudi za kuleta maendeleo endelevu na thabiti ya tabia na mienendo ya vijana katika mahusiano yao hususani katika masuala ya ngono ili kupunguza kasi ya maambukizi ya virusi vya ukimwi na kutekeleza mkakati wa kupunguza umasikini ili kufikia malengoya milenia (MDG`s)
2.0 SHUGHULI ZILIZOFANYIKA
• Katika miezi 3-(OKT-DES)ya utekelezaji, shughuli zifuatazo zilitekelezwa:

2.1 Ushiriki wa vijana siku ya UKIMWI duniani tarehe 1/12/2009.
Vijana takribani 300 walishiriki katika maadhimisho ya siku ya UKIMWI duniani .TEYODEN ilipata nafasi ya banda kuonyesha shughuli zake.Shughuli zilizoonyeshwa ni pamoja habari na stadi za maisha ambazo ni muhimu katika kufanya mabadiliko kwa vijana na kujiepusha na maambukizi ya VVU na UKIMWI.

2.2 Ushiriki wa vijana wiki ya vijana tarehe 14/10/2009
Vijana walipata nafasi ya kushiriki katika maadhimisho ya wiki ya vijana ambapo shughuli za msingi katika siku hii ilikuwa ni kuwasisitiza vijana kujiepusha na maambukizi kupima na kujua afya zao.Jumbe mbalimbali kuhusu UKIMWI zilitolewa kupitia ngoma maigizo na muziki wa kizazi kipya.

2.3 Mjadala wa vijana centre 1.
Kama ilivyo kawaida kwa vijana wa TEYODEN kufanya midahalo kila jumamosi mbili katika mwezi.katika kipindi cha taarifa vijana walifanya midahalo 4 na wastani wa vijana 96 walishiriki katika midahalo hiyo.

2.4 Vikao mikutanona warsha za kuoneza uwezo wa vijana na watendaji wa TEYODEN.
Katika kipindi chautekelezajitaarifa hii viongozi wanachama na walengwa wa TEYODEN walipata nafasi ya kushiriki shughuli mbalimbali kaaifutavyo:-

1.) Kiongozi mmoja(katibu) kutoka TEYODEN alipata nafasi ya kushiriki katika kikao cha wadau cha kupitia moduli ya stadi za maisha( 29/12/2009-1/1/2010) iliyofanyiwa marekebisho ya mwisho kabla ya kupigwa chapa na kuanza kutumika.Katika hiki yaliangaliwa mapungufu ya oduli hiyo ili kuendena sawa na mkabala wa stadi za maisha.

2.5kufanya matamasha 3 kwa ushirikiano wa asasi ya FEMINA
TEYODEN kwa kushrikiana na asasi FEMA tulifanikiwa kuendesha matamasha 3 katika kata za Somangila, Mbagala na Azimio.

1.) Lengo la matamasha haya lilikuwa ni:-
Kuwezesha vijana wengi zaidi katika kata zilizopendekezwa kupata nafasi ya kutafakari kwa kina shughuli za ujasiriali ni jinsi zinavyoweza kumuepusha na maambukizim ya V.V.U na UKIMWI.
2.) Shughuli na zilizotumika katika matamasaha hayo:-
Shughuli za maigizo ngoma na muziki wa kizazi kipya

3.) Mafanikio
Vijana walipata nafasi ya kipekee katika kutafakari VVU na UKIMWI na jinsi ya kujiepusha nazo kwa njia ya kujishughulisha na shughuliza uzalishaji mali.Takribani vijana 1500 walijitokeza katika matamasha hayo.

3.0 KAZI ZILIZOPANGWA KUFANYIKA MWAKA 2010
3.1 TEYODEN imepanga kufanya shughuli zifuatazo katika mwaka 2010
1.) Kutekeleza mradi wa kuamsha ari uwajibikaji na ushiriki wa vijana katika shughuli za maendeleo na za kijamii.

4.0 HITIMISHO
TEYODEN inaamini kuwa mabadiliko kwa vijana yatakayochangia maendeleo ya vijana yanawezekana kama vijana wanapewa uzito unaostahili katika kupanga, kutekeleza, kufuatilia na kutathmini shughuli za maendeleo. Viongozi wa TEYODEN na vijana siku hadi siku wamekuwa wakiongezewa uwezo katika kuhakikisha wanatekeleza majukumu yao ipasavyo.Hivyo tunawashauri wadau kutumia fursa hii adimu kwa kuwatumia ili kutatua matatizo ya vijana.vijana tukijiwezesha na kuwezeshwa tunaweza.
(Not translated)

In order to edit translations, you need to log in. Log in · Register