Base ((ururimi rutazwi)) | Kinyarwanda |
---|---|
UTANGULIZI Mwela theatre group tawi la vuga ni kikundi cha vijana cha kujitolea kilichoanzishwa tarehe 28/1/2010.ni muunganiko wa vijana kutoka katika vijiji vya Kidundai, Kiluwai,Vuga Kishewa na Bazo wakaunda Dira ya pamoja ya kuwa na jamii iliyoelimika na inayopenda kujifunza bila kikomo. Mwela theatre group ilipata mafunzo ya kujengewa uwezo toka mradi wa uimarishwaji wa asasi mradi uliofadhiliwa na The foundation for civil society na kuendeshwa na Chama cha maendeleo ya kiuchumi na kijamii vuga (CHAMAKIVU) mradi ambao mwela uliweza kuwapa ujasiri na kuweza kujiimarisha zaidi katika masuala ya utendaji kazi wake katika shirika MALENGO YA SHIRIKA
MHUTASARI Muhutasari wa mradi huu ni kuhakisha vijana wazee na wanawake wanashiriki katika kutoa maoni ya Katiba kwa kutumia haki zao za kimsingi za kikatiba ili kuleta mabadiliko yatakayokwenda sanjari na maendeleo kwa kupata mahitaji ya msingi ya vijana,wazee na wanawake. Mradi uliwafikia watu 110 me 50 na ke 60 toka katika vijiji vya Kiluwai na Kidundai toka kata ya Vuga wamefahamu faida za kushiriki katika utoaji wa maoni ya Katiba na kuchangia utoaji wa maoni hayo. Mradi huu umesaidia kutoa dhana potofu kwa vijana,wazee kuwa Katiba ya Nchi imeshatengenezwa. Shughuli za mradi huu zilikuwa kuendesha mikutano ya siku 3 kwa vijana wazee na wanawake walitoa maoni yao na walifahamu faida za kutoa maoni kwa njia ya mijadala njia hii ilisaidia vijana,wazee na wanawake kutoa maoni yao na wameonesha maisha halisi ya jamii yetu na mitazamo hasi katika jamii yetu juu ya masuala ya kushiriki katika kutoa maoni ya katiba hivyo njia hii ilisaidia kuibua mijadala na iliwapa fursa kuchangia na kutoa maoni mazuri HISTORIA YA MRADI Vijana wazee,na wanawake wa vijiji vya kiluwai na kidundai ambao walikosa utambuzi juu ya kutoa maoni yao na wengi hawakupata fursa ya kushiriki kikamilifu katika kuchangia marekebisho ya katiba pya Tulifanya mahojiano na baadhi ya vijana,wazee na wanawake 35% walikuwa hawafahamu lolote kuhusu masuala ya marekebisho ya katiba na kusema kwambao wao wamesahaulika katika mambo mengi ya maendeleo na kusema kuwa fursa nyingi zinapelekwa vuga bazo 25% walikuwa wanasikia tu kama kunamarekebisho ya katiba lakini walikuwa hawajui kuwa wao wana nafasi gani ya kushiriki na watashiriki vipi katika kutoa maoni ya katiba 20%walikuwa wanafahamu kama kunamarekebisho ya katiba lakini walikuwa hawana rasimu hiyo ya katiba hivyo walikuwa hawaelewi nini wachangie na nini wasichangie 15% walikukuwa hawana taarifa na hawakuhitaji kujisumbua na masuala marekebisho ya katiba kwa sababu waliamini kuwa katiba imeshatengenezwa hivyo ni janja tu ya kuweka mazingira ya kula pesa Kutokana na hali hiyo vijana,wazee na wanawake hawa dhahili kabisa kulikuwana kunahitajika kuwawezesha kuwa na maeneo na nafasi huru za kujadili masuala mbalimbali ikiwemo uwajibikaji,ushiriki na ushirikishwaji wao katika masuala muhimu ya marekebisho ya katiba .Lakini pia kupata nafasi ya kujadili changamoto za maisha na jinsi ya kukabilina na changamoto hizo.na ufumbuzi na majawabu ya maswali yao ni wao kushiriki katika kutoa maoni ya katiba LENGO KUU LA MRADI Ushiriki mzuri wa vijana,wazee na wanawake katika marekebisho ya katiba LENGO MAHUSUSI Kuongeza ushiriki wa vijana,wazee na wanawake katika marekebisho ya rasimu ya katiba MATOKEO YA AWARI Vijana,wazee na wanawake walifahamu umuhimu wa kutoa maoni ya rasimu ya katiba Vijana,wazee na wanawake walifahamu rasimu ya katiba na ibara zake Vijana,wazee na wanawake walifahamu kutoa maoni ni haki yao ya kikatiba MATOKEO YA KATI Vijana,wazee na wanawake walijua jinsi ya kujiunganisha na kujenga timu ya kuingia katika vijiji na kuchukua maoni na kuyatuma tume ya katiba Waliweza kutoa hoja nzito zenye kujenga ushirikiano wa pamoja na mahitaji yao na kuyapendekeza katika rasimu ya katiba WALENGWA Vijana wa mashule na nje ya shule Watoto wa mashule na nje ya shule wanawake NJIA TUNAZOTUMIA Semina Midahalo Mikutano na mikutano ya hadhara Matamasha Kupitia vijiwe vya vijana Nyumba hasi nyumba Kutumia michezo MAONI SIKU YA KWANZA UTANGULIZI BARAZA LA MAJADILIANO YA RASIMU YA KATIBA MPYA Mweyekiti wa Asasi ya MWELA Theater Group alifungua mkutano mnamo saa2:30 asubui kwa kuwakaribisha washiriki. Alifanya utambulisho wa wageni akiwemo MUWEZESHAJI, MCHUKUA DONDOO pamoja na washiriki wote wa baraza la majadiliano kutoka asasi ya MWELA ambao ndio walioshughulikia maombi ya Ruzuku kutoka The Foundation for Civil Society na kibali cha majadiliano haya toka Tume ya Katiba hii. Baada ya maelezo haya, alimkaribisha Muwezeshaji ili atoe maelezo mafupi yanayohusu majadiliano haya. MAELEZO YA MUWEZESHAJI Muwezeshaji aliwafahamisha washiriki juu na umuhimu wa kuchangia katika Katiba hii na taratibu zinazotakiwa kufuatwa
Muwezeshaji aliweza kuwagawa washiriki katika makundi ambayo yalikuwa makundi matatu, washiriki waliweza kushiriki kikamilifu katika makundi yao na Baada ya muda wa mijadala kumalizika, washiriki walirudi kwenye mjadala wa pamoja na kutoa hoja zao kama ifuatavyo; MADA; 1 Aina ya muungano(sura ya 6 ya rasimu) 2 Mambo ya muungano(mambo saba ya muungano yaliopendekezwa) 1 AINA YA MUUNGANO:- Mshiriki wa kwanza -Amependekeza kuwa na serikali moja Sababu: Inaleta amani kwani kila kitu kiko chini ya serikali moja Pia gharama za serikali zitakuwa mahali pamoja Wanakikundi walitoa ufafanuzi katika eneo la gharama kutokana na kuwa na serikali moja kutasaidia makusanyo ya pamoja na kugawa kwa pamoja tofauti na sasa ambapo tunagawana nchi mbili ambapo zanzibari ni ndogo sana tofauti na Tanzania bara Mshiriki wa 2 Amependekeza muungano wa serikali moja Sababu:mabalozi hawatakuwa watatu wala wawili bali mmoja Muungano wa serikali nyingi ni gharama Uraia utakuwa mmoja kwa pande zote Mshiriki wa 3 Amependekeza muungano wa serikali moja Sababu:maliasili zilizipo zitatumika kwa pande zote Watanzania bara hawatakuwa wageni Zanzibar bali watu wote watakuwa kitu kimoja Mshiriki huyo alitaka kiboreshwe kipengele cha tatu ambacho kinaeleaea uraia na uhamiaji mchiriki alitoa hoja kuwa mpaka sasa Zanzibar wanavitambulisho vyao na Tanzania bara wanavitambulisho vyao kitu ambacho kikiachwa kinaleta mgawanyo katika muungano Mawazo ya washiriki wengine ya meuwiana na mapendekezo ya hapo juu MAONI YA SIKU YA PILI NA YA TATU UTANGULIZI Mwenyekiti aliwakaribisha washiriki ukumbini mnamo saa 3.12 na kuwashukuru wajumbe na kuwatakia majadiliano mema kisha alimkaribisha mwezeshaji. Mwezeshaji naye aliwakaribisha washiriki kwa kuwataarifu kuwa tunaandelea kuwasilisha maoni ya siku ya kwanza kutokana na aina ya muungano na mambo saba ya muungano. Mwezeshaji aliwapa washiriki fursa ya kujadili vipengele vilivyomo katika katiba ili baada ya majadiliano watoe maoni yao Washiriki walipata chai 4:00 baada ya chai washiriki walirudi ukumbini na mwezeshaji akaendelea kuwashirikisha wanavikundi kutoa maoni yao pia tulipata waandishi wa habari toka gazeti la Habari leo,Mwananchi,Tumaini. MAONI Mshiriki:I, alipendekeza kuwa wananchi wawe na haki ya moja kwa kufanya uchaguzi wa kisheria kuhusu suala la madaraka ya ni yaani yani kuwe na ukomo Sura ya saba, ibara ya 74 Mshiriki:IIAlishauri kuwepo na katiba tatu yaani kuwe Sura ya pili katiba ya serikali ya Zanzibar Ibara ya II katiba ya Tanganyika na katiba ya Tanzania bara Mshiriki III . Alipendekeza kuwa spika na naibu spika wasichaguliwe na bunge ila wateuliwe na Raisi na kuthibitishwa na bunge Sura ya tisa ibara 128 Mshiriki IV: alipendekeza kuwa wafanyakazi wa makampuni wapewe haki zao bila kujari umri wao wanapostaafu. Sura ya 4 ibara 35 Mshiriki V: alipendekeza kuwa vikwazo vya elimu viondolewe -kuwajengea wanafunzi maabara -kujenga hostori kwa serikali -walimu wajengewe nyumba karibu na shule -kuwajari walimu -kuwaongezezea vifaa mashuleni Sura ya kwanza ibara 41 Mshiriki VI:Alipendekeza kuwa katika elimu,elimu hisiyo rasmi ipewe kipaumbele ili kuboresha vipaji vya vijana na watu wazima hasa katika suala ubunifu ili elimu ya Tanzania iwe ina msaidia mtanzania. Sura ya kwanza ibara ya 41 Mshiriki VII:Alipendekeza kuwa vyanzo vya mapato viwe na ushuru wa pande zote mbili yaani kuwe na ushuru wa Tanzania bara na ushuru wa Tananzia wa Tanzania visiwani Sura ya nne ibara 212 Mshiriki,IX:Alipendekeza haki za wazee zitekelezwe na kupatiwa huduma nzuri wanazostahiri Sura ya 1 ibara 47 Mshiriki X: Alipendekeza kuwa ushiriki uzingatie uwiano wa washiriki wa muungano katika bunge la jamhuri wa muungano wa Tanzania kuwakilishwa na watu wenye ulemavu Mambo ya muungano ibara 7 Mshiriki XI:Alipendekeza kuwa endapo Raisi atakuwa amefanya kosa lolote ashtakiwe kama raia wengine Sura ya 1, ibara 83 Mshiriki XII: Alipendekeza kuwa madeni ya nchi yafahamike kwa wananchi kwa kupitia vyombo habari na mikataba iwekwe wazi Sura ya 4 ibara ya 215 Mashiriki XIII:Alipendekeza kuwa taifa liingilie kati suala la mavazi ili kulinda hadhi ya Taifa, kipengele cha utamaduni kifafanuliwe ili ziwabane vijana katika kudumisha utamaduni wao Sura ya 1, ibara 43 Mashiriki XIV: Anapendekeza kuwa watoto wazaliwapo wapate cheti cha kuzaliwa mahali alipozaliwa kuepuke usumbufu Sura 2 ibara 42 Mshiriki XV: Alipendekeza limetolewa kuwa uhuru wa habari uwe na mipaka ili vyombo vya habari visitoa taarifa zinazopotosha wanachi. Mashiriki XVI: Alipendekeza kuwa Mawaziri wachaguliwe kama wanavyochaguliwa wabunge na Raisi Sura 4 ibara 30 Mashiriki VIII: Alipendekeza kuwa katika mfumo wa ajira usizingatie udhoefu bari mtu achaguliwe moja kwa moja kutoka chuoni bila kujari udhoefu Sura ya 4 ibara ya 35 Mshiriki XVIII: Alipendekeza serikali imarishe mazingira kuhusu watoto wa mitaani hadi hadi ngazi ya kijiji Sura ya 4 ibara 42 Mshiriki XIX:Alipendekeza kuwa wananchi washirikishwe katika kura za maoni kwa kupitia vyama vyao na matokeo yaishimiwe kikatiba kwa mgombea aliyepata kura nyingi Sura ya saba ibara ya 74 Mshiriki XXI:`Alitoa mapendekezo kuwa kiswahili kiwe lugha ya Taifa hata katika mikutano ya kimataifa na endapo kuna wasio kijua kuwa na wakalimani Sura ya 1,ibara ya 4 MshirikiXXII:Mahakama iwe na porisi jamii ili atoe elimu kwa wananchi juu ya haki zao na kuwepo na ukomo wa ajira katika majaji badala la miaka 70 iwe 60 kama wafanyakazi wengine Sura ya 10 ibara ya 155 Ibara ya 75 hadi 79 Madaraka ya Raisi Sifa Ukomo Kwamba makamu wa raisi ndio atakaye chukua majukumu ya raisi Kitu ambacho wananchi wananyimwa fursa ya kumchagua mtu wanaemtaka inawezekana kuwa raisi ameshirikiana na makamu wa raisi hivyo kuinasababisha ubovu kuendelea Maswali -Katiba ni nini -Faida za kushiriki katika katiba -Je rasimu hii ndio katiba -Kuna tofauti gani kati ya katiba ya zamani na rasimu hii -Je katiba hii ikikamilika mtatuletea kama mlivyotuletea wakati huu wa kuajadiri -Kwa nini hamjatoa mafunzo ya kujua jinsi ya kusoma ibara katika katiba -Wasiojua kusoma na kuandika watachangiaje -Kwa nini hakuna rasimu iliyochapwa kwa lugha ya wasiona CHANGAMOTO Uelewa wa washiriki kuhusu rasimu ya katiba ni mdogo Washiriki kutoudhuria katika muda muwafaka washiriki wamedai posho kinyume na masharti ya mkataba wetu na mfadhili kutoamini kwamba kinachofanyika ndicho walichoelezwa kudhani kuwa katiba ni mambo ya siasa na kusababisha ushiriki mdogo wa baadhi ya wananchi MAPENDEKEZO Kufanya mafunzo uhamasishaji jamii juu ya kufahmu vifungu na ibara mbalimbali katika katiba Mikutano na vikundi na mashirika yasio ya kiserikali na kutafuta wafadhili kwa mgongo wa tume Ruzuku itolewe kwa wakati Muda uongezwe katika majadiliano Viongozi wa serikali wasiangalie mabaraza yao tu wawe na hali ya kuunga mkono shughuli za kitaifa kwa maslai ya Taifa
SHUKRANI Mwela theatre group makao makuu DSM tunawashukura kwa kutupatia msaada wa kitaalamu tangia uandishi wa mradi,utekeleza na uandishi wa taarifa kwa kuhakisha tunatekeleza mradi kwa ufasaha kama mkataba unavyosema
Tunawashukuru The foundation for civil society kwa kutupaitia Ruzuku na kuonesha uaminifu kwetu kuwa tunaweza kutekeleza mradi huu na tumeitumia vizuri fursa hiyo
Tunawashukuru waandishi wa habari wa gazeti la habari leo,mwananchi,gazeti tumaini na Redio huruma
Tunawashukuru viongozi wa vijiji na kata kwa kutuhakikishia usalama na kutupatia maeneo ya kufanyia shughuli zetu bila bughudha yoyote
Tunawashukuru walimu na wanafunzi wa shule ya kiluwai kwa kushirikiana na sisi muda wote na kutuvumilia kutokana na mijadala iliyokuwa ikifanyaka shuleni hapo
Tunawashukuru wananchi na washiriki wote wa kijiji cha kiluwai na kidundai kwa kuonesha moyo wa kuwa nasi bega kwa bega mwanzo mwa uandishi wa mradi huu utekelezaji wake mpaka tulipofikia
HITIMISHO Serikali itoe fungu na kuwashirikisha vikundi na asasi za kiraia katika masuala makubwa kama haya ya kitaifa tangia mwanzoni ili kuongeza tija na ufanisi katika jamii na kuleta maendeleo ya Taifa letu
UTANGULIZI Mwela theatre group vuga ni shirika lisilo la kiserikali lenye nia ya kuikomboa jamii kwa njia ujasiliamali ili waweze kujikomboa katika suala la uchumi na kuweza kutatua matatizo yoa yenyewe katika kujua na kuifahamisha jamii dhana ya ujasiriamali ujasiliamali kama somo limetokea kupendwa sana katika eneo la mradi na kuwa kivutio kwa washiriki na hata wale ambao wamesikia mafunzo hayo yakiendeshwa lakini hawakupata fursa ya kushiriki lakini pia nao wamevutiwa kwa kiasi kikubwa ila kutokana na mradi huu wa ujasiriamali kukosa mfadhili na mwela kuamua kuendesha wao wenyewe kwa michango yao bila ufadhili umeona kuchukua watu wa chache na hivyo kuacha malalamiko kwa baadhi ya watu kutokana na utafiti mdogo tuliofanya tumegundua kuwa faida za kiufundi za ujasiriamali kwa wananchi kunaumuhimu mkubwa kwani ujasiriamali unaweza leta mabadiliko wa ukuwaji wa kiuchumi katika jamii kwani utawawezesha hata wale ambao wamekosa elimu ya msingi,sekondari na vyuo wanaweza wakajikwamua kiuchumi. Inakadiliwa mnamo mwaka 1700 ndio zana ya ujasiriamali ilipogunduliwa lakini mpaka leo bado sehemu nyingi hasa za vijiji bado kunachangamoto nyingi kutokana na watu wengi hawajajua somo ili la ujasirimali Mwela vuga inaamini ujasirimali ni zaidi ya dhana ya biashara tunaamini mjasirimali ni mtu ambaye anaweza kutoa jambo/wazo jipya ambalo litaweza kumpa faida Masoma haya ya ujasiriamali yamewafanya kinamama hawa kuwa:
walengwa wa mradi wanawake 60 toka katika vijiji vya Bazo,Vuga,Kiluwai na Kidundai toka Kata ya Vuga Jimbo la Bumbuli wilaya ya Lushoto
Malengo ya mafunzo
matokeo
MAONI Ujasiriamali ni kiungo muhimu katika kukuza,kuendeleza ni njia mbadala ambayo inaweza kuongeza nafasi za ajira na kipato na kuongeza uchumi na kupunguza umaskini ni wajibu wa serikali,asasi na tasisi mbalimbali kujitolea katika kuwasaidia watu maskini ambao wengi wao tunaishi vijijini Changamoto za wajasiriamali
Jinsi tulivyokabiliana nazo mtaji tuliweza kuwafahamisha kuwa mtaji ni kitu chochote ambacho mjasiriamali anawezatumia katika kuzalishia au kufanyia jambo Fulani kwa ,lengo la kupata faida kuondoa mtazamo wao wa mwanzo wa kuwa mtaji ni fedha tu na kuwaelewesha kuwa mtaji umegawanyika katika sehemu kuu zifuatazo fedha,nguvu kazi,elimu na utaalamu fursa wajasiriamali wengi hawatambui fursa zilizopo na ivyo kuwajengea uwezo wa kutambua fursa au kugundua fursa na uwezo wa kuchambua na kuchanganua fursa zilizopo ubunifu tuliwajengea uwezo wajasiriamali kuwa na ubunifu na ndio hasa dhana ya mjasiriamali unatofautisha mtu mmoja na mwengine hata kama wote wanafanya jambo linalofanana na kuwajengea uwezo wa kufikiri ya jinsi gani watafanya jambo jipya tofauti na linalofanywa na watu wengine lakini wao wafanye tofauti mawasiliano wajasiriamali wengi uwa wanashindwa kuendelea kutokana na kuwa na mawasiliano mazuri na wateja wao mawasiliano huunganisha watu pamoja na usaidia kupata taarifa mbalimbali muhimu katika biashara mawasiliano uboresha biashara na kumfanya mjasiriamali afanikiwe katika ujasiriamali wake MAHITAJI
SHUKRANI
ITIMISHO
tunaomba wadau wa maendeleo tunawaomba muje Vuga tushirikiane juu ya miradi mbalimbali ya kijamii kwani kunachangamoto nyingi na wafadhili wengi hawajafika hivyo tunashindwa kukabiliana navyo kutokana na kukosa rasimarimali za kutosha
|
(Not translated) |
Kugirango ugire icyo uhindura kubyo wasemuye, ugomba kwinjira mu rubuga Injira · Iyandikishe