Envaya

/TYNF/post/53: Kinyarwanda: WIWWW2IzDwxvGqTPaIcCdAmK:content

Base (Igiswayire) Kinyarwanda

MUHUTASALI WA KIKAOO CHA USAIHILI WA WAWEZESHAJI KUTOKA KATA SABA ZA MANISPAA YA TABORA.

Kikao kilifunguliwa mida ya saa tatu asubuhi na mratibu wa mradi wa pamoja tuwalee kwa kuwakaribisha wafanyakazi wa shirika la Aict pamoja na Muwezeshaji kutoka pact tanzania, watendendaji wa kata saba za manispaa pamoja na afisa usitawi wa jamii manispaa ya tabora. Baada ya hapo muwezeshaji kutoka AICT pamoja tuwalee alisoma maada za kikao hicho kilichotanguliwa na kuuelezea maana nzima ya mpango wa worth, na baadaye zoezi la usaili.

AGENDA ZA KIKAO.

1.  Maana nzima ya mpango wa worth

2. Usaili wa wawezeshaji kutoka kata saba za manispaa ya Tabora.

3. Mengineyo.

Maana nzima ya mpango wa worth

Worth ni mpango wa dhamani ambao unalenga kuwainua wanawake kielimu na kiuchumi katika ngazi ya kaya au familia. Mpango huu unalenga zaidi kuwasaidia akina mama wanaoishi katika mazingira hatarishi na mpango huwa hautoi kianzio chochote kwa wanavikundi isipokuwa ni elimu tu kwa wanavikundi ni jinsi gani wataweza kujiunga na kujipatia kipato chao wenyewe, pasipo kutegemea msaada wowote ule. Worth kama mpango maalumu huwa una vyao vyake vya mapato ambapo mapato hayo yanatokana na makubaliano ya wanachama wenyewewe. Wanachama wa vikundi wawo wenyewe huuda vikundi na kuchagua uongozi wao wenyewe ambapo uongozi huwa na, Mwenyekiti wa kikundi, Katibu, mtundha hazina na mtdibiti wa fedha. Ambapo sasa kama kikundi hukubalia wao wenyewe kuwa kima chao cha chini kitakuwa shilingi ngapi kutegemeana na kipato na makubaliano ya wanachama. Mwezeshaji toka pact alienze kwa kiima kuwa vyazo vya mapato huwa vipo vya aina mbili kupitia kwa wanachama wenyewe ambavyo ni, akiba ya hiari na akiba ya lazima huwa kama mtaji wao kwa wanavikundi.

Akiba ya hiari hapa ni kwamba mwanchama mwenyewe anatoa pesa yeyote anayoona anaweza kuotoa kuiwekeza kwenye kikundi na kwa kuja kijitabu maalumu. Hapa mwanacha atakuwa anajua idadi ya pesa yake pia ana uhuru wa kuichukua pindi aihitajipo,

Akiba ya lazima. Kikundi hapa hupanga akiba ya lazima kwa kila mwanakikundi mabapo kila kikundi wakutanapo pesa hivyo hukusanywa na kuandikwa kwenye kujitabu maalumu kama akiba ya mwanachama. Na huo ndo huwa mtaji wao na pesa zote huhesabiwa mbele ya kikundi na wanavikundi hukopeshana pesa hiyo kw awamu kadiri ya mpango mzima na matakwa ya kikundi hussika,

Muwezeshaji toka pact pia alisisitisa watendaji wa mtaa wahusike sana na pia waujue mpango mzima wa worth na mtaalaum wa au msimamizi wa worth kutoka Aict alisisitiza pia kuwa watendaji wanao nafasi kubwa sana katika kusisitiza pia kuhamasisha wamama wanatoka mazingira hatarishi wajiunge na mpango huu wa worth.

2.Usaili wa wawezeshaji kutoka kata saba za manispaa ya Tabora.

Suala zima ririkuwa ni usaili wa hawa wawezeshaji wa katani katika kuhamasisha wamama wanaishi katika mazingira hatari. Mtalaamu wa au msimamizi wa mambo ya Woth kutoka shirika la AICT alitanabaisha mbele ya wanakikao kuwa jumla ya watu 60 waliomba kazi hiyo ya uwezeshaji. Lakini usaili wa awali uliofanywa kikamilifu na kwa kuzingatia sifa za vigezo jumla ya watu 21 walipita baada ya mchujo wa awali ambao ndio leo hii tutawafanyia usaili wa mwisho tupate watu saba tu kutoka watu 21. Hivyo basi zoezi la usali lilianza kwa watahiniwa wote 21 kufanya tena mtihani wa awali ambao ulikuwa ni wahesabu hapo watu 14 tu ndoo walikuwa wnatakiwa wawili wawili kutoka kila kata. Kigezo kilikuwa kila mtahiniwa apate juu ya alama thelathini ndoo aende kwenye usaili wa mahojiano.

Baada ya zoezi hili jula ya watu sita tu waliweza kupata alama juu ya thelathini ambapo walingia kwenye usaili wa mahajiano toka kata ya Gongoni, Kiloleni pamoja na mtendeni. Ndani ya mchakato huu aliweze kupatikana mtu mmoja tu toka kata ya Kiloleni aliyefuzu usaili wa mahojiano. Bi salima alionesha ukomavu na uelewa kwani alijibu maswali yake kwa ufasaha sana kuliko wezanke. Hivyo paneli nzima ya usaili ilikubali kuwa katika kata zote tatu mtahiniwa aliyesitahili ni moja ambaye anatoka kata ya kiloleni na walikubaliana kwa kuweka saihihi katika karatasi husika,

3. Mengineyo.

Wajumbe wote wlipendekeza watendaji wapewe japo nakala zinazoelezea maana ya worth ili iwe rahisi kwao kuielimisha jamii juu ya mpango mzima huu. Pia Mtendaji wa kata ya T/reli alipendekeza mpango huo pia ujumuishe hata watu ambao hawapo katika mazingira hatarishi lengo ni kuwainua wote kiuchumi na kipato.Pia wajumbe wote walikibaliana kwa kupitia watumishi wa shirika kuwa kata hizo sita mabazo ni kitete, malolo, Ipuli, Mtendeni T/reli pamoja na Gongoni itabidi watu waombe upya tena ambapo usaili wa wali tena utakuwa tarehe 4/09/2012

Hitimisho.

Kikao kilifunguwa na mtaalamu wa mambo ya worth kutoka shirika la aict kwa kuwapongeza na kuwashukuru wajumbe wote waliofika kwa ajiri ya zoezi zima la usaili na kwa ushirikiano wao mkubwa waliouonesha katika zoezi hilo.

 

 

 

(Not translated)

Kugirango ugire icyo uhindura kubyo wasemuye, ugomba kwinjira mu rubuga Injira · Iyandikishe