Base (Swahili) | English |
---|---|
Kwa Usafiri huu kweli!Hii ni hali halisi katika Wilaya ya Kondoa ambako matumizi ya matrekta madogo (Power tiller) sasa yanatumika kubeba abiria na mizigo badala ya kufanya kazi za kilimo. Haishangazi wala kusikitisha kwani kulingana na hali halisi ya maisha; huu ni ubunifu. Watoto wa Sikuhizi!!
Kwa kuzingatia mabadiliko ya kiuchumi na taaluma; tunakipimaje kizazi hiki cha Sayansi na Teknolojia? Miaka kadhaa iliyopita tuliwasikia watoto na vijana wengi wakishirki kwenye michezo kadhaa ikiwemo ile ya kombolela, sambi, kuruka kamba, kubembea na mingine mingi. Hivi sasa ni nadra sana kwa watoto wa marika ya miaka 5-16 kuwasikia wakijihusisha na michezo hiyo kutokana na teknolojia. Swali muhimu la kujiuliza hapa ni je! mabadiliko haya yanatupeleka kwenye tamaduni gani? Kama watoto wataisaha michezo hiyo iliyo tukuza na kujikuta kuwa na maadili mema kwa jamii ikitoweka; tutavuna nini kwenye tamaduni za kimagharibi? Watafute watoto wa siku hizi na uwaulize swali dogo tu juu ya michezo wanayoipenda kwa sasa! Majibu utakayo kutana nayo ni pamoja na Kucheza gemu kwenye kompyuta, kuangalia TV nk. Wito wangu ni kwamba; tunapofurahia mabadiliko ya taknolojia; tukumbuke tulikotoka ili tusije kuwa watumwa wa teknolojia.
Dodoma Kavu; Inalimika, Inafugika.Pamoja na Mkoa wa Dodoma kusifika kwa ukame; Mkoa huu ulio katikati ya Nchi ya Tanzania wakazi walio wengi wanaishi kw kutegemea kilimo na ufugaji. Ni dhahiri kwamba Mkoa huu ni wa wafugaji na wakulima. Ila ninachokizungumzia hapa ni maisha ya wakazi wake waishio mjini hasa katikati ya mji ndani ya Manispaa ya Dodoma. Ukiwa katika Manispaa ya Dodoma si jambo la ajabu kukutana na watumishi wa nyumbani hsa wanaume wakiwa na matoroli yakiwa na majani ya mifugo hasa ng'ombe licha ya kuwa mbuzi, kondoo, nguruwe na kuku wanafugwa kwa wingi. Mkazi wa Mtaa wa Chidachi aliyefahamika kwa jina moja la Daniel akisukuma toroli lenye majani ya ng'ombe kama alivyokutwa na mpiga picha wetu. Kilimo: Shuhuli za Kilimo katika Mkoa huu zinaendeshwa katika Wilaya zake zote hasa ikizingatiwa kuwa ardhi ya Dodoma inasifika kwa kuwa na mbolea inayojitosheleza kwa mazao ya aina mbalimbali ya nafaka ikiwemo mahindi, ufuta, alizeti, mtama, uwele, mbaazi, karanga nk. Kama ilivyo kwa ufugaji, ndani ya Manispaa ya Dodoma wakazi wake wamekuwa wakijihusisha na kilimo cha mazao mbalimbali katika maeneo ya viwanja vilivyo wazi ambavyo wamiliki wake bado hawajaanza kuvijenga nk.
Kilimo cha Mahindi katika Kata ya Mkonze Manspaa ya Dodoma Mkonze. Lucas Mkasanga Miaka 14; Darasa la Tatu!
Lukas anasikitishwa na kuchelewa kwake kujiunga na elimu ya msingi kutokana na kile alichodai ni kutengana kwa wazazi wake hali iliyo mfanya akaishi na bibi yake mzaa baba Wilayani Kondoa kwa kipindi kirefu. Kwa mujibu wa maelezo ya Lucas; baba yake ni mpishi wa shule ya Sekondari Bihawana iliyoko katika kata hiyo ya Mbabala. Aliongeza kuwa sasa anaishi na mama yake wa kambo ambaye anamshukuru kwa kumpeleka shule ili afikie malengo yake ya kuja kuwa Mwalimu hapo baadae.
Lucas anaeleza changamoto zilizopo shuleni kwake kuwa ni pamoja na uhaba wa vitabu ambapo hivi sasa kitabu kimoja kinatumiwa na wanafunzi wanne hadi sita. Kuhusu adhabu shuleni anasema kwamba hilo ni jambo la kawaida kwa wanaofanya makosa shuleni japo amewatetea walimu wake kuwa si wachapaji sana. Lucas alihitimisha mahojiano yake kwa kuiomba Serikali iangalie namna ya kuboresha mazingira ya kujifunzia na kufundishia hasa kwa kuongeza vifaa muhimu mashuleni kama vile vitabu, vifaa vya michezo na kusikiliza matatizo ya walimu ili wawe na moyo wa kuwafundisha kwa bidii. Kijana huyu anaelezea mafanikio yake kitaaluma kuwa ni mazuri darasani ambapo anashika nafasi ya kwanza kati ya wanafunzi 94 wa darasa lake. Wakati huo huo kamera yetu ilimnasa kijana mmoja ambaye jina lake halikufahamika mara moja akiwa na lundo la madaftari ya wanafunzi wenzake akiyapeleka nyumbani kwa mwalimu kwa ajili ya kusahihisha kazi za wanafunzi. Kwa mujibu wa maelezo ya baadhi ya wanajamii walieleza kuwa kutokana na idadi kubwa ya wanafunzi na uhaba wa walimu katika shule hiyo; walimu wana lazimika kufundisha vipindi mfululizo na baadaye kwenda kusahihisha kazi hizo wakiwa nyumbani. Jambo la kujiuliza hapa ni je! kwa hali hii ya mwalimu kujikuta wakifanya kazi za shule muda wote yani nyumbani na shuleni; jamii. serikali na wadau wengine tunafanya nini ili kuwawezesha walimu kumudu maisha yao ya kila siku? Maria (11) na Video za Usiku.Maria Yohana (11) ni mwanafunzi wa darasa la pili katika shule ya Msingi Mwenge iliyoko katika Kijiji cha Mbabala A Manispaa ya Dodoma. Maria ni miongoni mwa watoto ambao hawanabudi kuokolewa kutoka katika hatari ya kukumbwa na balaa la mmomonyoko wa maadili kutokana na yeye mwenyewe kukiri kujihusisha na utazamaji wa video hasa nyakati za usiku. Ilikuwa majira ya saa kumi na mbili na nusu (12:30) za jioni nilipo kutana na mtoto huyu kwenye eneo la vilabu maarufu kama Makondeko; maria alikuwa akisubiri picha iliyoanza saa 8 mchana iishe ili aingie picha ya pili inayoanza saa moja hadi saa mbili na nusu usiku. Kwa maelezo ya Maria; kiingilio katika nyumba hiyo ya video ni sh. 100 kwa watoto. Hata hivyo yeye anamudu kulipa kiingilio kwa kuomba kwa wazazi wake au vijana (majirani zake) anao wafahamu. Kwa Maria ambaye ni mtoto bado; hajatambua fika hatari iliyo mbele yake; lakini kwa wazazi na jamii inayomtazama Maria akiingia na kutoka katika chumba hiki cha video katikati ya kilabu cha pombe kuna jambo nadhani wanaliona kwa Maria.
Baadhi ya wazazi walioongea na mwandishi wetu alieleza masikitiko yake juu ya serikali ya kijiji cha Mbabala kulifumbia macho suala la wengi wa watoto wa kijiji hicho kuangalia video katika nyumba hiyo iliyoko katika eneo la kilabu. "Kuna wakati mwingine huyu mtu anaonyesha picha mbaya za X hadi usiku na watoto wa shule za Sekondari na hawa wadogo wote wanaangalia" alisema mmoja wa wakazi wa eneo hilo. Eneo la Makondeko ni eneo pekee lenye mkusanyiko mkubwa wa watu na shughuli mbalimbali zikiwemo za kibiashara katika Kijiji cha Mbabala A. |
For this Transportation true!This is the reality in Kondoa District where the use of small tractors (Power tiller) is now used to carry passengers and cargo instead of working in agriculture. It is not surprising nor sad because according to the realities of life, this is creative. Nowadays children! In line with economic changes and professionalism, we kipimaje this generation of Science and Technology? Several years ago we heard that many young children and shirk on several games including the kombolela, sambi, jump rope, swing and many others. Right now it is very rare for children 5-16 years of age to hear the engaged and games due to technology. Important questions to ask here is how! this change takes us into what cultures? If children will isaha games which glorify and find a moral community disappearing, we will reap what the western culture? Look for children these days and just ask a small question about their favorite games now! Answers you'll meet it includes gemu Playing on the computer, watching TV etc.. My appeal is that, we pofurahia taknolojia change, remember where we came from in order not to be slaves to technology. Dry Dodoma; Inalimika, Inafugika.Although Dodoma Region Notable droughts; This region is in the middle of the country majority population live kw depending on agriculture and livestock. It is obvious that this region are pastoralists and farmers. But I chokizungumzia here are living a life of its residents in exactly the center of town within the municipality of Dodoma. Being in Dodoma Municipality is a wonderful thing to meet domestic servants HSA men with a wheelbarrow having leaves livestock mainly cattle despite being a goat, sheep, pigs and chickens are raised in abundance. Chidachi Street resident was known by one name Daniel pushing a wheelbarrow as he leaves the cow vyokutwa with our photographer. Agriculture: Shuhuli of Agriculture in this region have operated in all its districts considering the land of Dodoma inasifika inayojitosheleza to be fertilized to produce various types of cereals including maize, sesame, sunflower, millet, sorghum, peas, nuts etc.. As with livestock, in the municipality of Dodoma residents have been involved in the cultivation of various crops in areas of Vacant plots whose owners have not yet started kuvijenga etc.. Maize farming in County Mkonze Mkonze Manspaa Dodoma. Lucas Kasanga 14 Years: Third Grade!
Lukas is disappointed with the delay in joining his primary education from what is claimed separation from his parents made the situation he lived with his wife, the father father Kondoa District for a long time. According to the statement of Lucas, his father is the cook of the secondary schools located in the county Bihawana the Mbabala. He added that he now lives with his foster mother, whom he thanked for sending school to achieve its goals to become teacher in the future. Lucas tells her that the school challenges include a shortage of books where the current textbook used by four to six students. About punishment at school says that it is common for offenders to school, though he defended his teachers were not very publishers. Lucas concluded his interview by asking the government to look at how to improve learning and teaching environment, especially by adding the necessary equipment to schools such as books, sports equipment and listen to the problems of teachers to be encouraged to train hard. Boy explains his success as a good academic classroom where he holds first place among 94 students of his class. Meanwhile our cameras ilimnasa young man whose name was not immediately likufahamika with heap registers his fellow students to drive home teacher for the correct function of... |
Translation History
|