Envaya

/m-e-d-1-1/post/107582: English: WIgkcGMIGPRqsWbNUigp3tQ5:content

Base (Swahili) English

MED YAANZISHA MFUKO WA ELIMU YA SEKONDARI CHIDACHI  

Na. Barakaely Christopher

Shirika la Marafiki wa Elimu Dodoma (MED) kwa kushirikina na wananchi wa kata za Kikuyu Kusini na Mkonze Manispaa ya Dodoma wameanzisha mfuko wa kuwalipia ada na michango mingine wanafunzi wote watakaofaulu mtihani wa darasa la saba na kujiunga na elimu ya sekondari kutoka shule ya msingi Chidachi.

Lengo la mfuko huo ni kuwahamasisha wanafunzi wa shule ya msingi chidachi kuongeza juhudi kwenye masomo yao na kuwa na uhakika wa kuendelea na elimu ya sekondari.

Muasisi wa mfuko huo Bw. Davis Makundi ambaye pia ni Mlezi wa shule ya Msingi Chidachi na Mratibu wa Shirika la Marafiki wa Elimu Dodoma (MED) alianza kampeni ya kuanzisha mfuko huo Septemba mwaka jana katika mahafali ya nne ya darasala la saba ambapo mgeni rasmi alikuwa Meneja wa Benk ya Posta Tanzania Bw. Emmanueli Gyumi aliyemwakilisha Mkurugenzi Mkuu wa Benki ya Posta Tanzania.

Katika mkutano huo wazazi wa wanafunzi wa shule ya msingi Chidachi uliofanyika shuleni hapo wameomba mfuko huo uanze haraka na kuazimia kuwa wazazi wote wenye watoto katika shule hiyo wahusike kuchangia uendelevu wake ili kupunguza mzigo wa kusomesha watoto pasi na uhakika kutokana na kipato duni walichonacho. Akaunt ya Mfuko huo itafunguliwa katika Benki ya Posta Tanzania Tawi la Dodoma.

Katika mkutano huo wazazi walipokea jumla ya madawati 15 na seti moja ya bendi ya shule vyote vikiwa na thamani ya zaidi ya sh. 1,200,000 fedha ambazo zimetokana na michango ya wadau wa elimu, wazazi na wanafunzi kupitia kazi za mikono kwenye somo la Elimu ya Kujitegemea (EK).

Mwalimu Mkuu wa Shule ya hiyo Bi. Ashura Mhoji alieleza kuwa shule yake imekuwa ikifanya vizuri kwa kufaulisha wanafunzi kwa kati ya 80% hadi 100% kutokana na mwamko na ushirikiano uliopo baina ya walimu, wazazi, wanafunzi na wadau mbalimbali wa Elimu. Aidha alilishukuru shirika la MED kwa mchango wake mkubwa ambao limekuwa likitoa mara kwa mara katika shule hiyo. MED katika mkutano huo imechangia kiasi cha sh. 150,000 kwa ajili ya madawati na mfuko wa Elimu.

 

MED marks SECONDARY EDUCATION FUND CHIDACHI

And. Christopher Barakaely

Organization of Friends of Education Dodoma (MED) for superstition and citizens of the county of Kikuyu Africa and Mkonze Municipal Dodoma have set up a fund to pay fees and other contributions all students who passed the test of seventh grade and join secondary education from primary school Chidachi .

The objective of the Fund is to motivate students of primary school chidachi increase efforts on their studies and be sure to continue with secondary education.

Founder of the fund mr. Davis groups who also is Lord of primary school Chidachi Coordinator Organization of Friends of Education Dodoma (MED) began a campaign to establish the fund in September last year at the graduation of four darasala seven where the guest of honor was the Manager of Benk Tanzania Posts Mr. Emmanuel Gyumi who appeared for the Director General of the Tanzania Postal Bank.

During the meeting the parents of students of primary school Chidachi held the school have asked the fund to start soon and planning that all parents with children at the school get involved donate their sustainability in order to reduce the burden of educating children without assurance from the income poor they had. Akaunt the fund opened at Tanzania Postal Bank Branch of Dodoma.

During the meeting the parents had received a total of 15 desks and one set of all labels for school band worth more than Shs. 1,200,000 cash contributions that stems from education stakeholders, parents and students through the work of the hands on the subject of Education for Self-Reliance (ESR).

Head Teacher of the School of the Bi. Ashura Interviewer explained that his school has been good for pupils achieving between 80% to 100% due to the awareness and cooperation existing between teachers, parents, students and stakeholders of education. Either he thank MED agency's role which has given regularly at school. MED at the conference contributed a total of shs. 150,000 for desks and Education Fund.


In order to edit translations, you need to log in. Log in · Register

Translation History

Google Translate
February 17, 2013
MED marks SECONDARY EDUCATION FUND CHIDACHI – And. Christopher Barakaely – Organization of Friends of Education Dodoma (MED) for superstition and citizens of the county of Kikuyu Africa and Mkonze Municipal Dodoma have set up a fund to pay fees and other contributions all students who passed the test of seventh grade and join secondary education from...