| Base (Swahili) | English |
|---|---|
Madarasa ya elimu ya awali bado kizungumkuti
Hili ni darasa la awali lililopo katika kijiji cha Mkali B, kilichopo wilaya ya Nyasa, mkoani Ruvuma. SERIKALI imefanya kosa kubwa la kiufundi kuhusu uamuzi wake wa kuanzisha madarasa ya elimu ya awali katika shule za msingi nchini. Kupitia Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Serikali iliagiza kila shule ya msingi kuwa na darasa la elimu ya awali, lakini ikasahau kuziwezesha shule hizo kirasiliamali na hata kutoa mwongozo wa uendeshaji wake. Jukumu hilo sasa liko chini ya wazazi wenyewe kupitia kamati za shule na walimu wakuu wa shule za msingi. Uchunguzi wa hivi karibuni wa Mwananchi katika shule za kata ya Liuli iliyopo wilaya ya Nyasa, mkoani Ruvuma, umebaini kuwapo kwa mazingira ya kusikitisha katika yanayoitwa madarasa ya elimu ya awali. Hata walimu wanaofundisha watoto hao ni wa kuokota, huku wakiwa hawana mafunzo maalumu ya ualimu kwa watoto. Baadhi ya walimu ni vijana waliohitimu kidato cha nne na kupata daraja sifuri. Hawa ndio watu waliokabidhiwa jukumu la kuwapika watoto kwa minajili ya kuwaandaa kuingia darasa la kwanza. Wadau wa elimu wanasema bado Serikali haijaipa elimu hiyo msukumo unaostahiki kama inavyofanya katika madaraja ya elimu ya msingi, sekondari, elimu ya juu na ufundi. Kwa mfano, mdau wa elimu na Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Mkali iliyopo wilayani Nyasa, Erasmus Haule, anasema bado Serikali haijatangaza elimu hiyo kuwa ni ya lazima, jambo linalosababisha wazazi kutohamasika kusomesha watoto wao katika madarasa ya elimu ya awali. ‘’Hakuna sheria inayowabana wazazi kupeleka watoto katika shule za awali. Kuna siasa hapo na ndio inayofanya elimu hii ikose nguvu,’’anasema. Aidha, kwa sababu ya Serikali kutojiingiza moja kwa moja katika uendeshaji wa elimu hiyo kama ilivyo katika madaraja mengine ya elimu, wazazi wamebebeshwa mzigo wa kujenga madarasa na kulipa mishahara ya walimu. Kwa kukosa uwezo wa rasilimali, wazazi wameshindwa kujenga madarasa hayo, hivyo kuponea madarasa yanayotumiwa na wanafunzi wa shule za msingi. Hata posho za walimu, japo ni ndogo bado inabidi wazazi washikane mashati kuchangia. “Tatizo kubwa ni namna ya kuwalipa walimu, Tunaiomba serikali ilichukue darasa la awali kama ilivyo kwa darasa la kwanza, isiwaachie wananchi, ‘’anasema Diwani wa kata ya Liuli, Charles Chawila. |
Early education classes still kizungumkuti
This is the first class existing in the village of Bright B, based Nyasa district, Ruvuma region. Government has made a technical mistake about his decision to set up classes in pre-primary schools in the country. Through the Ministry of Education and Vocational Training, the Government required every primary school had grade education, but ikasahau kirasiliamali enable these schools and even to guide its operations. Responsibility now lies under the parents themselves through school committees and head teachers of primary schools. Recent investigations of the Citizen in the county school district Liuli existing Nyasa, Ruvuma Region, has revealed the existence of the sad circumstances in the so-called early education classes. Even teachers who teach these kids are picking up, with no special training in the teaching of children. Some of the teachers are young qualified Form Four and get the grade zero. These are the people who kuwapika given to children in order to prepare them to enter first grade. Education stakeholders say the government is still not that inspiring education ijaipa eating like they do in the classes of primary, secondary, higher and technical education. For example, a member of the education and Head Teacher Primary School severe discrepancy Nyasa district, Erasmus Haule, says the government still does not ijatangaza that education is compulsory, which causes kutohamasika parents educate their children in early education classrooms. '' There is no law inayowabana parents to send children to school before. There are there and the politics that makes this knowledge be without power,'' he said. In addition, because the government than not engaging directly in the operation of such education as in other education classes, parents have entrusted the burden of building classrooms and paying teachers' salaries. With the inability of resources, parents have been unable to create these classes, so escaped the classes used by pupils of primary schools. Even allowances of teachers, although it is smaller still have parents contribute washikane shirts. "The main problem is how to pay teachers, government Tunaiomba ilichukue original class like first class, isiwaachie citizens,'' he said Liuli ward councilor, Charles Chawila. |
Translation History
|
