Base ((unknown language)) | English |
---|---|
KATIBA YA KIKUNDI CHA KISESA WOMEN NETWORK Utangulizi: Chama cha KISESA WOMEN NETWORK ni miongoni mwa vyama/ vikundi vya hiari vya watu wenye ulemavu/ waishio katika mazingira hatarishi. Kikundi hiki ni kati ya vikundi vinavyotokana na makundi maalum.
Aidha watu wanaotokana na makundi maalum, wanazo changamoto nyingi, ambazo zinawafanya wasikubalike haraka kwenye jamii, kiasi cha kunyanyapaliwa na hata kutopata huduma za Afya, Elimu na hata ustawi kiasi cha kuwafanya waishi chini zaidi ya kiwango cha umaskini.
Uhuru, Haki na Usawa umeelezwa vizuri kwenye katiba ya nchi. Uhuru huo ndio unaotoa fursa ya kila kundi lenye lengo fulani na vikwazo fulani kuungana kwa pamoja kuifikia jamii ili kupunguza au kuondoa vikwazo vilivyopo. Na kuhitaji uundwaji wa Kikundi/Chama KISESA WOMEN NETWORK.
SEHEMU YA KWANZA.
1. Jina la Chama - KISESA WOMEN NETWORK 2. Makao Makuu : Makao makuu ya kikundi yatakuwa Kisesa – Jiji la Mwanza Wilaya ya Magu DIRA : kuhakikisha kwamba jamii inashirikishwa na kushiriki katika jahudi za kuondoa utegemezi/ umaskini wa wanawake wenye ulemavu, yatima, wajane na wanawake waishio katika mazingira magumu.
4. MADHUMUNI: Madhumuni ya uundwaji wa kikundi ni kufanya yafuatayo:- a) Kuinua maisha ya wanawake wenye ulemavu, yatima, wajane na waishio katika mazingira magumu. b) Kutoa elimu ya staili mbalimbali za kuyamudu maisha (ujasiliamali) c) Kujenga moyo wa kujiamini. d) Kujenga na kuboresha mahusiano na mashirika mengine ya kiserikali na yasiyo ya kiserikali yanayosaidia wanawake. e) Kulinda haki na maslahi ya wanawake wenye ulemavu, yatima, wajane na waishio katika mazingira magumu kiafya ki-elimu, kijamii na ustawi wa akina mama . f) Kuelimisha Umma juu ya matatizo ya kisayansi ya wanawake wenye ulemavu, yatima, wajane na waishio katika mazingira magumu. g) Kuhakikisha na kudumisha heshima na haki za binadamu kwa wanawake waishio katika mazingira magumu. h) Uanzishaji wa SACCOS i) Kushirikisha wanawake katika masuala ya uatawala bora, haki za binadamu, demokrasia na vita dhidi ya rushwa. j) Wanawake kujikinga na maambukizi mapya ya virusi vipya vya ukimwi k) Kuhakikisha wanachama wanapata ufahamu wa kutosha juu ya kushiriki na kushirikishwa katika kuchanganua changamoto kadhaa zinazowakabili katika kuelekea kujiondolea umasikini wa mawazo na kipato n.k.
SEHEMU YA PILI
UANACHAMA. (i) Kutakuwa na aina tatu za uanachama: a) Uanachama wa kawaida – mwanamke mwenye ulembavu, mjane au anayeishi katika mazingira magumu , yatima.
b) Uanachama wa kushirikishwa – mtu yeyote ambaye si mwanamke ambae kukipenda kikundi na kupenda kukichangia kikundi kwa hali na mali .
c) Uanachama wa Heshima – mtu yeyote au chama ambacho kitakuwa na umuhimu mkubwa kwa kikundi katika kufanikisha malengo ya kikundi .
ii) Kuomba Uanachama: Mtu yeyote ambaye hakuwa mwanachama mwanzilishi katika kifungu cha kwanza (a) na (b) atatambulika kwenye kikundi kuwa wanakikundi kwa kujaza fomu maalum ya maombi na kuipeleka kwa mratibu wa kikundi ambaye ataiwakilisha kwa uongozi kwa ajili ya maamuzi ya mwisho.
iii) Kiingilio: a) Kutakuwa na kiingilio cha uanachama ambacho kitatafasiliwa na uongozi . b) Kutakuwa na Ada ya kila mwanachama kwa mwaka ambayo itaamualiwa na uongozi.
2. KIKOMO CHA UANACHAMA Uanachama unaweza kukoma:- a) Kwa kujitoa mwenyewe baada ya kutoa taarifa ya siku tisini (90) b) Kwa kuachishwa kutokana na utovu wa nidhamu na kutokua muadilifu. c) Kuwa kichaa na kuthibithishwa na daktari au kufariki dunia. d) Mwanachama ambaye amejiondoa au ameachishwa na amepona kichaa akitaka kujiunga tena ni lazima aombe upya kwa kufuata taratibu za sehemu ya pili kifungu cha kwanza namba (a) na (b) ya katiba hii baada ya miaka 2.
3. HAKI ZA MWANACHAMA: Kila mwanachama atakuwa na haki zifuatazo:- a) kushiriki katika shughuli zote za chama kulingana na taratibu zilizowekwa. b) Kuhudhuria na kutoa maoni yake kwenye vikao/ mikutano ya kikundi. c) Kuchagua na kuchaguliwa viongozi wa kikundi na kuwa mkweli na kuwa na utayari wa kukosolewa na kuachia au kupata madaraka. d) Kuwa na moyo wa kujitolea kusikilizwa kujitetea na kutoa maelezo yake mbele ya vikao halali vya kikundi. e) Kuwa mwaminifu kutumia ujuzi wake kwa manufaa ya chama. f) Mwanachama wa kushirikishwa na mwanachama wa heshima ataruhusiwa kugombea uongozi au kupiga au kupigiwa kura.
4. WAJIBU WA MWANACHAMA. Wajibu wa kila mwanachama utakuwa kama ifuatavyo:- a) Kutetea, kutekeleza sheria na kanuni za katiba hii ili kutekeleza kwa vitendo Madhumuni ya kuanzishwa kikundi hiki:- b) Kuwa tayari kukosea, kukosolewa na kutumia kipaji kuendeleza kikundi. c) Kutunza, kuthamini, kulinda mali na kubuni njia bora za kuendeleza kikundi. d) Kuwa tayari kujielimisha kwa bidii na kwa uwezo wake wote na kutumia elimu hiyo kwa fadia ya kikundi. e) Kushauri Uongozi kwa busara katika kusimamia mipango yote ya maandeleo au ya uendeshaji kwa manufaa ya kikundi.
SEHEMU YA TATU. 1. UONGOZI: Kutakuwa na viongozi wafutao:-
2. SIFA YA UONGOZI. Kiongozi yeyote sharti awe na sifa zifuatazo:-
3. MIIKO YA UONGOZI: Kwa kiongozi yeyote ni mwiko:-
SEHEMU YA NNE 1. Uendeshaji wa Chama / Kikundi:- Kutokana na:-
2. Mkutano mkuu: Ni chombo chenye maamuzi ya mwisho katika uendeshaji wa kikundi majukumu yake ni:-
3. Kamati ya uongozi ya kikundi. Kutakuwa na kamati ya uongozi ya kikundi ambayo itakuwa na wajume wafuatao:-
4. Kazi za kamati ya Uongozi: Kamati ya Uongozi itakuwa na kazi zifuatazo:
5. Kamati Tendaji Kutakuwa na Kamati tendaji ambayo itaundwa na:-
6. Kazi za kamati Tendaji
SEHEMU YA TANO. 1. UONGOZI WA CHAMA. Kutakuwa na viongozi wakuu wa kikundi wafuatao ambao watachaguliwa kila baada ya miaka mitatu (3)
1.1. Kazi ya Mwenyekiti wa kikundi:-
1.2. Kazi za Katibu
1.3. Kazi za Mweka Hazina:-
1.4. Watia saini akaunti za kikundi. Kutakuwepo na watia saini katika akaunti za benki ambazo ni (i) Mwenyekiti, Mratibu na Mweka Hazina.
SEHEMU YA SITA.
1.1. Mlezi wa kikundi: Kutakuwa na mlezi wa kikundi atakayeteuliwa na kamati ya uongozi na kuthibitishwa na mkutano mkuu wa kikundi.
1.2. Kazi mlezi wa kikundi:- Atakuwa ni mishauri muelekezi wa kikundi kwa masuala ya maendeleo ya kikundi. Pia atashauri katika kukubali, kutafuta au kuridhia ufadhili.
1.3. Mapato ya Chama. Chama kitapata mapato yake kutokana na:-
KUKOMA / KUFUTWA KWA KIKUNDI. Pindi kikundi kitakapositisha shughuli zake au kufutwa basi miliki zote za mali zitagiwiwa kwa vyama vya kiraia vyenye madhumuni sawa na kikundi.
|
(Not translated) |