Log in

Translations: English (en): User Content: WI000D1369304D0000096515:content

« Previous   ·   Next »
Base (Swahili) English
MWENYEKITI WA CCM MBEYA AKIRI CHAMA CHAKE NI LEGELEGE KIMEZAA SERIKALI LEGELEGE:
soma+maghembe.JPG
 WAZIRI WA KILIMO CHAKULA  NA USHIRIKA PROF.JUMANNE  MAGHEMBE  AKIJIBU HOJA ZA WAKULIMA NA WAKUU WA WILAYA NA VIONGOZI WA HALMASHAURI ZA MBOZI, MBEYA VIJIJINI, ILEJE NA RUNGWE JANA ALIPOSHAMBULIA NA VIONGOZI WENZAKE WA SERIKALI WALIOKUWA WAMEGEUZA KIKAO HICHO KUWA CHA KWAO WAKATI WAKULIMA WA KAHAWA NDIYO WALITAKIWA KUTOA HOJA.

5-2.JPG

 KATIKATI ANAYEONESHA MGONGO NI WAZIRI MAGHEMBE ALIPOZUILIWA NA WAKULIMA WA WILAYA YA MBOZI ASIINGIE UKUMBINI KWA MADAI KUWA WALIOKUWA WAMEANDALIWA NA HALMASHAURI YAO WALIKUWA NI WAFANYABIASHARA NA WALA SI WAKULIMA.

1-7.JPG
MMOJA WA WAKULIMA AKIWA ANAELEZA JAMBO KWA WAANDISHI WA HABARI WALIOKUWEPO MBOZI JANA NA KWAMBA WAO WANATAKA KUUZA KAHAWA MBIVU KATIKA SOKO HURIA ILI KULETA USHINDANI WA BEI KATIKA ZAO HILO LAKINI WANAZUILIWA NA HALMASHAURI HIYO HUKU IKIRUHUSU BAADHI YA VIKUNDI VYA WALANGUZI KWA MANUFAA YAO.

DSC01353.JPG
 MKUU WA MKOA WA MBEYA ABBAS KANDORO ALITOA NENO LA BUSARA NA WAZIRI MAGHEMBE ALIINGIA KWENYE UKUMBI KUJIBU KERO YA KAHAWA

DSC01356.JPG
RC KANDORO ALITOA PENDEKEZO KWA WAKULIMA HAO ILI KURUHUSU WAINGIE 10 UKUMBINI HUMO.

wakulima.JPG

wadau.JPG




·       Waziri waghembe aambiwa Wizara imemshinda

·       Serikali Mbeya yajitenga, yasema isiingiliwe

·       Wakurugenzi wajitoa, wawaachia wanasiasa




MWENYEKITI wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wilaya ya Mbozi mkoani hapa Aloyce Mdalavuma ambaye ni muhanga wa kura za maoni za  Ubunge katika uchaguzi Mkuu 2010, amesema kuwa chama chake ni legelege ndiyo maana kimeunda Serikali legelege 

Hayo aliyasema jana katika kikao cha pamoja kati ya Waziri huyo, Mkuu wa mkoa wa Mbeya Abbas Kandoro, wakuu na wakurugenzi wa wilaya za Mbozi, ileje, Mbeya Vijijini na Rungwe, wafanyabiashara na wakulima wa zao la Kahawa.

Mdalavuma alisema kuwa, wakulima wilayani Mbozi wamekosa pembejeo msimu wa mwaka 2010-2011 na Serikali imekaa kimya jambo ambalo linamkumbusha kauli ya kwamba chama legelege huunda Serikali legelege.

‘’Ndugu waziri, umekuja hapa tukifikiri kuwa utazungumzia mustakabali wa uuzaji na ununuzi wa kahawa mbivu na upatikanaji wa pembejeo lakini tunashangaa hakuna majibu ya namna hiyo na hii nakumbuka kauli isemayo chama legelege huzaa serikali legelege’’alisema Mdalavuma huku wadau wakiguna na Prof, Maghembe akishika tama.

Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo ya Mbozi Erick Ambakisye alimtisha Waziri Maghembe kuwa endapo anguthubutu kutekeleza kanuni za wizara yake zinazoruhusu kununua kahawa mbivu wilayani humo ambayo wakulima wanaitaka wakati Halmashauri haihitaji atakuwa tayari kwenda kwa Rais Jakaya Kikwete ili waziri huyo achunguzwe.

Alisema kuwa anavyomfahamu Waziri huyo, anaamini kuwa wizara hiyo ya Kilimo chakula na Ushirika imemshinda na Jimbo lake pia limemshinda ndiyo maana wananchi wake hawana uchumi imara.



Kwa upande wao, wakulima zaidi ya 400 waliofika katika ukumbi wa Halmashauri hiyo ya Mbozi walimzuia Waziri Maghembe kuingia ukumbini hapo kwa madai kuwa waliokuwa ndani ya ukumbi walikuwa  ni wafanyabiashara ya kahawa na wala si wakulima na ndiyo maana wao kama wakulima halisi walikataliwa na viongozi wa Halmashauri kuingia ukumbini.



Baada ya hali hiyo ya vuta nikuvute huku Afisa usalama wa wilaya hiyo akijaribu kuwasukuma wakulima hao ili Waziri aingie ndani na kuzungumza na  ‘’wakulima maalum’’ waliokuwa wameandaliwa bila mafanikio huku asijue kuwa kulikuwa na wakubwa zake katika msafara huo, ndipo Mkuu wa mkoa wa Mbeya Abbas Kandoro alitumia busara ya kuwataka wateue wawakilishi.

Wakulima wengi walisema kuwa taarifa aliyokuwa amepewa na viongozi wa Mkoa wa Mbeya iliyosema kuwa uuzaji wa kahawa mbivu inawaingizia hasara siyo ya kweli bali ililenga kuwanufaisha watu wachache wakiwemo vigogo wa Halmashauri zinazolima zao la kahawa mkoani Mbeya.

Mkulima Abrahamu Nzowa alisema kuwa, wakati Serikali na baadhi ya watendaji wa Halmashauri hizo zikiwa zinaipiga vita biashara hiyo hasa kampuni ya Lima Ltd inayonunua zao hilo kwa bei kubwa kuliko vikundi ambavyo viongozi hao wanamanufaa navyo, vikundi vinaendelea kuwanyonya wakulima hali ambayo wamesema inaleta kutoelewana miongoni mwao.

Aidha walisema kuwa kwasababu kahawa  ni mali yao hawataacha kuuza kahawa hiyo mbichi kwa kampuni ambayo itakuwa inanunua kwa bei nzuri licha ya wilaya na mkoa kukataza kuuza kahawa hiyo.

Mkuu wa mkoa wa Mbeya Abbas Kandoro alimweleza Waziri Maghembe kuwa msimamo wa Serikali ya mkoa wa Mbeya ni kwamba haitaki kusikia uuzaji na ununuzi wa kahawa mbivu mkoani hapa mpaka pale wakulima watakapoandikishwa na kutambulika.


‘’Sisi kama mkoa wa Mbeya tuliazimia katika vikao halali vya wadau wa mkoa na kwamba hatutaki biashara ya kahawa mbivu na kwasababu hapa hakuna wakulima walioandikishwa hawa wote si wakulima halali kisheria hivyo mpaka hapo tutakapokamilisha zoezi la kuwaadikisha ndipo tutakapochukua maoni yao’’ alisema Kandoro kwa kujichanganya.


Akizungumza na waandishi wa habari nje ya ukumbi huo baada ya kuogopa hoja za Wakuu wa wilaya, wenyeviti wa Halmashauri za wilaya hizo Nne huku wakurugenzi wote wakikataa kuzungumzia suala hilo lililochukuliwa kisiasa zaidi, Waziri Maghembe alisema kuwa hatengui kanuni zenye baraka za Wizara bali anachotaka bei ziboreshwe kwa wakulima.


‘’Mimi sijatengua kanuni za Wizara na Bodi ya kahawa juu ya ununuzi wa kahawa m,bivu bali nilichokuwa nasema ni kwamba lazima wilaya zisimamie sheria na kuhakikisha bei kwa wakulima wa kahawa zinasimamiwa na kulipwa vema lakini Serikali ya mkoa nyie mmeisikia haitaki biashara hiyo’’ alisema Waziri Maghembe.


Alisema licha ya hayo yote kila mfanyabiashara wa kahawa ama mnunuzi ni lazima awe na leseni ya biashara na haruhusiwi kununua kahawa kwa mkulima ambaye hajaandikishwa ili kudhibiti ukwepeji mapato ya Serikali kupitia biashara hiyo kama ilivyo sasa wilayani humo.


Kwa upande wake Mkurugenzi wa bodi ya kahawa nchini Adolph Kumbulu na mwanasheria wa Wizara ya kilimo walisema kuwa ununuzi wa kahawa mbivu umeongeza tija ya ubora wa kahawa Tanzania kutokana na ubora wa usindikaji wake tofauti na usindikaji unaofanywa na wakulima.


Hali hiyo ya mkanganyiko wa uuzaji na ununuzi wa kahawa mbivu (Cherry) imeleta utengano wa baadhi ya wakulima ambapo Serikali hasa vyombo vya usalama vinatakiwa kuliangalia kwa umakini kutokana na hali ilivyo ya wananchi kujengeana chuki ikiwa ni pamoja na kuijengea chuki Serikali.


Ubora wa kahawa upo katika ngazi nne ambazo ni P1,P2,P3 na Ponds, ambapo P1 inatoa madaraja Nane ambayo ni AA, A, B, PB, C, AF na F ambapo madaraja yanayouzwa nje ya nchi ni AA,A,B, PB na daraja C. 

 Habari na pastor kalulunga
CHAIRMAN OF CCM'S PARTY IS MBEYA confess already fragile KIMEZAA already fragile Government :
soma+maghembe.JPG
MINISTER OF AGRICULTURE FOOD AND FELLOWSHIP PROF.JUMANNE Maghembe Responding to OF FARMERS AND GREAT LEADERS OF THE DISTRICT AND THE BOARD OF Mbozi, Mbeya Rural, Rungwe and Ileje ALIPOSHAMBULIA YOUTH AND GOVERNMENT LEADERS Fellow Torrential WAMEGEUZA session to them AT THE RATE OF COFFEE FARMER YES They had to move.

5-2.JPG

Middle ANAYEONESHA gongo Maghembe ALIPOZUILIWA MINISTER AND FARMER'S DISTRICT Mbozi ASIINGIE claiming that the compound have been produced Torrential AND THEIR BOARD WAS NOT NOR businessmen and farmers.

1-7.JPG
He explains one of the farmers having SOMETHING FOR Journalists WALIOKUWEPO Mbozi YOUTH AND THAT SELL THEIR COFFEE Want ripe to bring OPEN MARKET COMPETITION IN THEIR PRICE BUT WANAZUILIWA HILO AND BOARD THAT SOME GROUPS while allowing for their benefit of smuggling.

DSC01353.JPG
THE REGION'S MBEYA Abbas KANDORO He SENSIBLY AND MINISTER'S WORD Maghembe Entered HALL IN RESPONSE TO COFFEE nuisance

DSC01356.JPG
RC KANDORO She suggested farmers to let some of them 10, wherein the compound.

wakulima.JPG

wadau.JPG




· Minister Maghembe be answered Ministry imemshinda

· The Government Mbeya yajitenga, says isiingiliwe

· Directors Commitment, let the politicians




Chairman of the Revolutionary Party (CCM) Mbozi district of the province who are here Aloyce Mdalavuma muhanga the opinion of the parliamentary vote in 2010 general elections, has said that his party is already fragile government is already fragile sense kimeunda

That spoke yesterday at a joint meeting between the minister, General Abbas Kandoro Mbeya region, district heads and directors of Mbozi, Ileje, Mbeya Rural and Rungwe, traders and farmers of the coffee crop.

Mdalavuma said that farmers often lack input Mbozi district season in 2010-2011 and the Government which linamkumbusha gone silent statement that the party forming the government already fragile already fragile.

''Dear Minister, you have come here if we thought it was going to talk about the future of the sale and purchase of coffee ripe and availability of inputs, but we are surprised there are no answers like that and this I remember a statement saying the party already fragile bears government legelege''alisema Mdalavuma with stakeholders if they complain and Prof, Maghembe He held lust.

Chairman of the Board of Mbozi Erick Ambakisye he threatened that if the Minister Maghembe anguthubutu his department to implement the principle of allowing the district to buy ripe coffee that farmers have urged the council does not need will be ready to go to President Jakaya Kikwete to minister achunguzwe.

He said that he vyomfahamu minister, believes that the Ministry of Agriculture and Cooperatives and State imemshinda his limemshinda also why its citizens have a strong economy.



For their part, farmers in more than 400 have arrived in the hall of the council that the Mbozi prevented Minister Maghembe into court there on charges that were inside the hall were the traders of coffee and not the farmers and that is why they like the farmers net were rejected by officials of the Board enter the courtyard.




In order to edit translations, you need to log in. Log in · Register

Translation History

Google Translate
January 22, 2012
CHAIRMAN OF CCM'S PARTY IS MBEYA confess already fragile KIMEZAA already fragile Government : ...